Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi hili niwese kuchangia kwanza kabisa nampongeza Waziri na Naibu waziri kwa hotuba yake nzuri iliyosheheni matumaini ya watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Serikali yangu ya Chama Cha Mapinduzi kwa kutupatia pesa bilioni 5.4 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali za Wilaya, Wilaya ya Busega Bariadi DC na Itilima. Mchanganuo wake kila wilaya tumepata bilioni 1.8 lakini pia tunachangamato ya ukosefu wa vifaa tiba pamoja na madawa. Changamoto hii ni kubwa sana katika vituo vyetu vya afya pamoja na Hospitali za Wilaya wananchi wanatoka vijijini kwenda kutibiwa kwenye Vituo vya Afya wakifika wanakosa madawa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hiyo inasikitisha sana mwananchi akitibiwa anaambiwa kwenda kununua dukani kuna wananchi wengine wana hali duni hawana uwezo wa kununua dawa, naiomba Serikali iweze kutuletea dawa za kutosha katika hospitali zetu. Lakini pia katika vituo vyetu vya afya mkoa wa Simiyu hatuna x-ray mashine, hiki kifaa ni muhimu sana ikiwezekana naiomba Serikali ibaini vituo vyote vya afya nchi nzima ambavyo havina x-ray mashine ili waweze kufunga. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vijana wetu hawa wa bodaboda wanapata ajali, wakienda kwenye kituo cha afya wanapewa tiba ya dharula ambayo ni ya mwanzo kwamba atibiwe halafu baadaye aende katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa. Kwa vile vijana wetu wanaimani potofu wanaendea kwa waganga wa kienyeji hatimaye kidonda kinaoza wengine wasukuma wetu kule anaweza akapata ugonjwa wa TB hajapigwa x-ray anaenda kwa waganga wa kienyeji anatumia dawa za kienyeji akienda kwenye kituo cha afya hamna kipimo cha x-ray anaishia kutumia madawa ya kienyeji anaathirika naiomba Serikali ifanya hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kitu kingine katika vituo vyetu vya afya hatuna umeme mbadala ambao ni jenereta, daktari akiwa anamfanyia mama mjamzito operation umeme ukikatika inakuwa ni shida naiomba Serikili ifanye utafiti katika vituo vya afya vyote ambavyo havina umeme mbadala ambayo ni jenereta ili waweze kufunga. (Makofi)

Mheshismiwa Naibu Spika, lakini pia katika vituo vyetu tuna upungufu mkubwa wa madaktari hasa madaktari bingwa wa magonjwa ya akina mama, sisi akina mama tuna maradhi mengi, ukienda hospitali huwezi ukatibiwa na daktari wa kawaida kuna malazi mengine ambayo unatakiwa umwone specialist wa magonjwa ya wanawake. Sisi Mkoa wa Simiyu tuna mmoja tu ambaye yupo Somanda, na katika Mkoa wa Simiyu tuna Wilaya tano huyo daktari anahudumia wilaya tano unakuwa msongamano mkubwa, daktari anachoka tunaiomba Serikali ituletee madaktari bingwa katika hospitali zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika hospitali yetu ya mkoa, kwanza niipongeze Serikali kwa kutupatia pesa kujenga hospitali yetu ya Mkoa katika hospitali yetu ya mkoa bado haijakamilika hatuna wodi ya akinamama, hatuna wodi ya watoto, na hatuna wodi ya akina baba. Jengo la mama la mtoto bado halijakamilika na pesa ipo sijui tatizo ni nini, Mkandarasi anasuasua sana tunaiomba Serikali waziri akija aje na majibu kwa nini hilo jengo linasuasua na pesa ipo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika hospitali yetu ya mkoa hatuna uzio kabisa, na hospitali ikikosa uzio ni hatari sana hospitali yetu ya Mkoa wa Simiyu iko karibia na barabara ya lami, wagonjwa katika hospitali wanaenda wa kila aina kuna mwingine anaweza kwenda amerukwa na akili anakimbilia kwenye lami anagongwa gari lakini pia uzio unadhibiti hata kuibiwa madawa na vifaa tiba. Naiomba Serikali itupatie pesa ili tuweze kujenga uzio. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naishukuru sana Serikali kwa kutuboreshea hospitali ya Maswa tuna theatre nzuri na tuna wodi nzuri za kulaza wagonjwa lakini tatizo mortuary ni ndogo inachukuwa watu watatu Tunaomba tupatiwe friji ili tuweze kuipanua hiyo mortuary. Lakini pia katika Vituo vya Afya vya Mkoa wa Simiyu hauna friji za kuhifadhi maiti. Tunaiomba Serikali iweze kutuletea friji katika vituo vyetu vya afya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hospitali inayotibu saratani ni moja tu hiko Dar es salaam ambayo ni Ocean Road na wagonjwa wengi wanatoka kanda ya ziwa, tunaomba Serikali iboreshe hiyo hospitali ya Bugando ili kuweze kurahisha matibabu wananchi wanaotoka vijijini kanda ya ziwa watibiwe hapo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana baada ya kusema hayo naunga mkono hoja. (Makofi)