Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Jacquline Andrew Kainja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. JACQUELINE K. ANDREA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi hii niweze kuchangia Wizara hii ya Afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, moja kwa moja mchango wangu niuelekeze kwenye Universal Health Coverage kwa maana ya Bima ya Afya kwa Wananchi Wote, ambayo tuliinadi katika Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi kwamba Watanzania wote wapatiwe bima ya afya. Hata hivyo, tukiambatanisha na Sera yetu ya PPP - Public Private Partnership ili kuweza kuondoa changamoto na matatizo ambayo yanalikumba Taifa letu la upungufu wa dawa na vifaa tiba.

Mheshimiwa Naibu Spika, kabla sijaifafanua hiyo bima ya afya pamoja na Sera yetu ya PPP, naomba niishauri Wizara kuangalia explorer option ya kutokutunza dawa za wagonjwa wa nje au hospitalini tunasema outpatient, ili kuondoa mkanganyiko ambao unatokea kwamba Wizara inatoa taarifa kwamba kuna wizi wa dawa na upotevu wa vifaa tiba. Tukiimarisha bima yetu ya afya kwa wananchi wetu wote, bima ambayo ina tija ambapo mwananchi akienda private sector atapata huduma zote na akiingia hospitalini za Serikali atapata huduma zote. Kwa kufanya hivi inaweza ikatuondolea mkanganyiko huo wa kuona kwamba watoa huduma za afya pharmacist, doctors wanaiba dawa au vifaa tiba.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tuangalie sisi kama Wizara au Serikali kazi yetu ni kutoa huduma au tunahitaji tufanye business? Hii ni katika eneo hili la upotevu wa dawa na upungufu wa dawa na vifaa tiba. Naongea hivyo kwa maana tunaona kwamba private sector zinafanya vizuri ukilinganisha na vituo vya afya na zahanati za Serikali. Private sector anachojali ni kuangalia ana-provide service nzuri kwa mgonjwa au kwa mteja wake, hakuna suala la dokezo, hakuna kwamba dawa imeisha lazima niandike dokezo kwa Mganga Mkuu Mfawidhi au kikao cha management kiweze kupitia zile taratibu zote.

Mheshimiwa Naibu Spika, unaweza ukaenda private sector kununua dawa hata kama hana, anakuambia subiri naenda store lakini kiuhalisia sio kwamba anaenda store anaenda kuangalia duka la jirani ili aweze kum-maintain huyu mgonjwa. Kwa hiyo, tuiangalie ni namna gani hii bima ya afya ikifanya kazi vizuri na tukajitahidi kuwa tuna-store dawa kwa ajili ya inpatient kwa maana ya wagonjwa ambao wamelazwa hospitali lakini wale wagonjwa ambao ni outpatient wapate bima yenye tija ili waweze kwenda nje kwenye private sector waweze kuhudumiwa, bima ambayo itakuwa na tija kwa maslahi ya mwananchi na sio kwa maslahi ya labda system, Serikali au Wizara. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, unakuta kama Serikali au Wizara tunakuwa na mzigo mkubwa ku-store dawa ambazo wakati mwingine ni brand. Unakuta kuna dawa ambazo ni brand ziko pale hospitali na tukiangalia kiuhalisia yale mafungu yetu matatu ambayo ni ya exemption kwa maana ya wazee, watoto na mama wajawazito zile brand ambazo tumezi-store pale hospitali kwa maana tumefungua duka la dawa la hospitali siyo yale makundi yanapata zile dawa na bado hatuweki kwa wingi unaotakiwa kumfanya yule mgonjwa akifika pale apate dawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile clinicians anapata shida anapokuwa ana-prescribe medicine, labda anataka ampeleke mgonjwa kwenye third generation ya antibiotic, kwa sababu dawa zilizoko pharmacy ni first generation inabidi ampatie hiyo iliyopo. Tunajua kiuhalisia sisi Watanzania wote huku majumbani ni madaktari, before hujaenda hospitali umeshajitibu sana huku nyumbani. Kwa maana umeshaji-diagnosis wewe mwenyewe umeshakuwa mfamasia, ukisikia tumbo linauma unakunywa dawa metronidazole tunatengeneza resistance kubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, unapokwenda kwa daktari tumeweka essential drugs ambazo ziko hospitali pale kwamba sisi kama hospitali au kama Wizara tumeweka item zetu ni 30 hizi hapa tukipungua chini ya hapo tutasema kwamba dawa hakuna lakini kama Wizara inapoenda kufanya supervision inakuta zile essential drugs ziko pale tunaambiwa kwamba dawa zinapatikana lakini kiuhalisia tungeweka bar yetu items za essential drugs zifike bar hata kwenye mia tukifika sabini ndio tuseme basi dawa zipo lakini sio tumeweka 30 and then tunasema kwamba dawa hapa zinapatikana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hilo kwenye suala la bima ya afya na kuchanganya na hizi PPP, naomba niende kwenye suala la bima ya afya ya CHF iliyoboreshwa. Hii CHF iliyoboreshwa bado haijawa na msaada kwa wananchi wetu, ina msaada wa kuonana na clinician’s au vipimo. Pia na yenyewe ina vipimo ambavyo haiwezi ku-clear na inampa shida mtoa huduma. Mfano kama kuna sehemu amekosea ku-request wanakatwa makato makubwa zaidi kiasi kwamba unakuta kituo kinarudi nyuma kwenye mapato. Mfano, ame-claim labda Sh.900,000/= lakini anakuja kupewa Sh.90,000/= jambo ambalo linamrudisha nyuma kuendesha shughuli za kituo. Wakati huo hapo kuna exemption za makundi matatu ambayo yanatakiwa yapate free medicine na kituo kinatakiwa kijiendeshe na pesa zote zimelala huku CHF. Nimuombe Waziri aangalie hii CHF basi hata iwe supported na NHIF ili hawa NHIF ambao wamesha-master vizuri kuangalia claim form zao zinakaaje na kama mtoa huduma amekosea wanajua namna gani ya kumwambia kwamba amekosea sehemu hii na hii tofauti na CHF.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niende kwenye suala zima la bajeti. Suala siyo tatizo la bajeti, tatizo pesa hizi hazifiki kwenye vituo kama inavyotakiwa. Kwa hiyo, unakuta kama ni bajeti ya familia kwa mfano umepanga labda familia yangu inatakiwa kula kwa siku Sh.10,000/= baba ameacha shilingi 200 tunategemea nini? Kwa hiyo, haitaweza kufikia malengo, haya matatizo ya dawa na vifaa tiba kukosena yataendelea mara kwa mara. Tutajikuta hatutaweza kutatua tatizo kama kila siku tutakapokuwa tunakaa hapa kujadili bajeti mambo ni yale yale. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongelee vituo vya afya ambavyo wananchi walijenga kwa nguvu zao wenyewe na Serikali kuna wakati imeweka mfuko ikakamilisha lakini majengo bado hayajakamilika. Kwa mfano, Kituo cha Igalula kimekamilika lakini hakina dawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naunga mkono hoja. (Makofi)