Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanda vya Moshi Mjini na Kilimanjaro kwa ujumla ambavyo vimefanywa maghala na vingine havifanyi kazi kwa ufanisi. Naishauri Serikali itekeleze ahadi ya Rais wakati wa kampeni kuwanyang‟anya wawekezaji ambao hawajaweza kutimiza malengo ya awali yaliyotarajiwa katika viwanda vilivyobinafsishwa. Mahusiano ya kisekta ni muhimu sana (forward and backward interlinkage). Naishauri Serikali iwekeze katika Agro Processing Industries (value added) ambavyo vitaongeza thamani ya mazao yetu ya kilimo. Pia nishati lazima iwe ya uhakika na ya bei rahisi ili viwanda vyetu vizalishe kwa bei nafuu kwa maana ya kuwa cost effective.
Vilevile ni lazima miundombinu ya reli iimarishwe ili iweze kubeba mizigo ya viwandani. Hatuwezi kutegemea barabara katika kusafirisha mizigo ya viwandani. Aidha, lazima Serikali iimarishe taasisi za kifedha financial institutions ili ziweze kutoa mitaji kwa wawekezaji wadogo, wakubwa na wa kati. Mikopo ikiwa na riba kubwa haiwezi kusaidia wawekezaji ndani wala wa nje. Nashauri Serikali iwe na mkakati wa kuacha kukopa mikopo mikubwa kwenye taasisi za fedha ili wawekezaji binafsi waweze kukopa kwa riba nafuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, masoko ni muhimu sana katika kuhakikisha uwepo wa viwanda, nashauri mambo yafuatayo katika masoko:-
(a) Serikali ifanye jitihada za kuimarisha soko la ndani kwa kuongeza fursa za vipato kwa wananchi. Mataifa yanayokua kwa kasi kiuchumi kama China, India na mengineyo yamefanikiwa kuimarisha soko la ndani hivyo bidhaa zao wanazozalisha zinapata walaji wa ndani ya nchi na ziada ndio inauzwa nje. Kuimarika kwa soko la ndani kunavihakikishia viwanda uhakika wa kupata faida kwa bidhaa zinazozalishwa. Mojawapo ya mkakati wa kusaidia soko la ndani ni kuongeza uwezo wa kununua (purchasing power) kwa wananchi kwa kuhakikisha vipato vizuri vya mtu mmoja mmoja na wananchi kwa ujumla.
(b) Masoko ya nje lazima yatafutwe kwa kuanzia nchi jirani. Jambo hili litafanyika kwa kujifunza vizuri bidhaa ambazo tunaweza kushindana na jirani zetu. Pia ni vizuri wananchi wetu wasaidiwe jinsi ya kuingia kwenye ushindani na wananchi wenzetu katika masoko mbalimbali ya nchi jirani.
(c) Masoko yataimarishwa kwa kuziimarisha sekta za utalii, madini na Halmashauri zetu na sekta binafsi. Sekta ya utalii imekuwa kwa haraka katika nchi yetu, hivyo ni vizuri ikatumika katika kutoa ajira ambazo zitaongeza kipato cha wananchi na baadaye kupanua soko la ndani. Pia sekta ya utalii itafanya hivyo hivyo.
Aidha, Serikali ikizitumia Halmashauri zetu vizuri kwa kuimarisha sekta ya wajasiriamali wadogo wadogo kwa maana sekta isiyo rasmi itatengeneza kundi la watu wenye mitaji ambao wanaweza kuwekeza kwenye viwanda vidogo vidogo, viwanda vya kati na hata baadaye wanaweza kuunganisha mitaji na kuwekeza kwenye viwanda vikubwa. Zaidi ya hayo sekta binafsi inatakiwa itengenezewe mazingira rafiki ya kufanya shughuli zake ili iweze kuajiri wananchi wengi zaidi hivyo kuongeza kipato cha wananchi na kwa maana hiyo kuongeza nguvu ya kununua yaani purchasing power.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali lazima iwekeze katika teknolojia kwa kuimarisha mifumo yetu ya elimu na vyuo vya sayansi na ufundi.