Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Hon. Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie kwa kifupi kabisa mambo machache kwenye hotuba hii ambayo imewasilishwa. Naomba nianzie suala la makampuni ya kimataifa ambayo yanafanya kazi katika nchi yetu. Yapo makampuni mengi yanafanya kazi na makampuni au biashara ndogo ndogo, zipo kampuni za tax kama Uber, Taxify na pamoja na nyingine za namna hiyo. Zipo kampuni za booking kwenye mahotel mbalimbali zipo hoteli.com, booking.com na nyingine za namna hiyo. (Makofi)


Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa ninaomba wakati Mheshimiwa Waziri atakua anaenda kuhitimisha atufahamishe ni namna gani wanaweza kupata kodi kupitia makampuni haya haswa yale ambayo hayana ofisi locally ambayo yanafanya biashara na yanakusanya fedha nyingi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeomba pia nigusie kwenye suala la wizi, watu wengi wamegusia suala la wizi ninaomba niligusie kwa sehemu mbili, kuna wizi kwa maana wizi wa software na wizi kwa maana hard ware. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka sasa hivi mtu akiibiwa simu ambayo imeshasajiliwa na IMEI yake hipo kuweza kufuatilia inaonekana ni jambo kubwa sana, wakati teknolojia imeshakwenda mbali sana, simu hizo zinaweza kuzimwa na zisiweze kutumika na kwa bahati mbaya sijaelewa shida inakuwa wapi kwa sababu inabidi uende kwa subscriber wako. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nadhani wizara inaweza kuweka utaratibu kukawa kuna call center moja ambyo ukiibiwa simu regardless na matandao wako ukipeleka taarifa zako pale wanaweza ku-share kwa mitandao yote na wakai-block hiyo simu. Lakini hiyo ya kui- block ni hatua ya mbele zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nilikuwa nadhani njia rahisi ya kukomesha kwa haraka ni kwamba ikishaibiwa simu ikisetiwa call center ya namna hiyo basi hizi IMEI number ikiweza kuwa shared kwenye hiyo mitandao basi waweze ku-trace line nyingine itakayowekwa hata kama ni ya mtandao mwingine anayetumia akamatwe vitendo vya namna hiyo vikiendelea vinakomesha wizi wa simu na baadaye laptop pamoja na vyombo vingine hivi vinavyotumia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hili niwashauri Serikali kama wanaona ni gharama ku-run kitu cha namna hiyo, mimi nadhani kuna vijana wa kitanzania wengi baadhi ni watu nawafahamu wanaweza kufanya kazi hiyo kwa niaba ya Serikali na wengine walishapeleka mpaka maombi wakaambiwa ni mpaka tubadili policy. Sasa unaibiwa simu unaenda kutoa taarifa polisi inabidi kusubiri siku tatu nne na hapo ikishafikia hivyo uwezi kuokoa kitu chochote haswa information zinazokuwa kwenye vyombo vile. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ningeomba hili lifanyiwe kazi tunacho chuo cha Cyber Crime pale CCP kimeanzishwa, ninadhani ni muda sasa kama wataona ni gharama kufanya hivyo tunaweza kupitisha sheria kwamba mtu anaibiwa kifaa cha umeme hicho, kama simu computer au tablet aweze kupewa huduma ndani ya masaa 24, ndani ya masaa 24 maana yake mtu anaweza aka-trace watu walioiba na kupata kifaa chake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niende upande wa software na huu nadhani kidogo watu wengi wamegusia na Mheshimiwa Rais alipokuwa anaongea naye aligusia, kwamba inawezekanaje mpaka sasa tunasajili mpaka line zetu kwa kutumia fingerprint lakini wale wezi wa kwenye mtandao bado wapo na bahati mbaya fedha hizi zinamlolongo au zina cheni kama ukimtumia hawezi kuzitumia bila kwenda kwenye wakala na kuzitoa au kulipia huduma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa inaonekana bado wizi huu unashamiri na watu tunao na teknolojia, walizima zile simu za kichina ndani ya siku kadhaa tu wakaweza kuzizima, lakini kwa sasa hivi hawa watu wanaiba kwa mtandao kila siku wanaweza kuwasha laini hatujui wanasajilije bila kuwa na fingerprint na hatujui kwanini hawawezi kukamatwa mpaka viongozi wa nchi atoe rai kwenye jambo dogo kama hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nilikuwa nadhani ni vizuri wizara wajipange kwa ajili ya hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kabisa naomba kuunga mkono hoja ahsante. (Makofi)