Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ili uchumi wetu ufikie uchumi wa kati tunatakiwa tuwekeze katika viwanda vyetu vya ndani pamoja na kuvisimamia. Pia tukumbuke viwanda ndio njia pekee inayoweza kutoa ajira kwa vijana walio wengi nchini. Pia kuna vijana wengi ambao hawana ajira, niishauri Serikali iwawezeshe vijana hawa ili wasiwe wanatangatanga kwenda mjini kutafuta ajira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo kuna vijana wengi waliomaliza vyuo na hawana ajira, papo hapo wanaambiwa walipe mkopo waliokopa, vijana hawa watalipaje mkopo kama Serikali yao haijawawezesha kupata ajira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna asiyefahamu kuwa Wilaya ya Lushoto ni ya wakulima wa matunda na mboga mboga. Hivyo niishauri Serikali iweke kiwanda cha kusindika matunda, kwani matunda na mboga mboga vinaharabika hali inapelekea wakulima kupata hasara katika mazao yao hayo na pia wakulima wetu tunawakatisha tamaa kwa kupoteza nguvu zao nyingi shambani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vijana wengi wamejitahidi kujiajiri kwa kufanya biashara lakini wanasumbuliwa sana na watu wa TRA hasa wafanyabiashara wa Jimbo la Lushoto. Maafisa wa TRA hawana elimu ya biashara, halii inapelekea Maafisa hawa kuwa ndio wamepata uchochoro wa kuwanyanyasa wafanyabiashara hawa. Imefikia hatua mfanyabiashara akutane na simba lakini sio Afisa wa TRA. Naomba Serikali iliangalie hili ili wafanyabiashara wale waweze kufanya biashara yao kwa amani na kujipatia kipato chao cha kila siku.