Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika azma ya Serikali kuwa nchi ya viwanda na hatimaye kuwa na uchumi wa kati lazima Serikali ije na mkakati wa kulitumia Shirika la Viwanda Vidogo Vidogo (SIDO) kwa mapana zaidi. Kwa hali ilivyo sasa hivi SIDO ina ofisi na kutoa huduma kwenye Makao Makuu ya Mikoa tu na Mikoa mingine haina, hali hii inafanya wananchi wanaotaka huduma kufuata huduma za SIDO Makao ya Mkoa ambako ni mbali. Lazima SIDO iwezeshwe ili iweze kufuata watu na kuwapa huduma huko wanakoihitaji. SIDO isogeze huduma katika Wilaya, Kata na hata vijijin na kwenye miji mingine midogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bado mazingira ya kufanya ama kuanzisha biashara katika nchi yetu siyo rafiki kwa wafanyabiashara na wawekezaji. Mwananchi akitaka kufanya biashara hapo hapo anafuatiliwa na TRA na vyombo vingine vya utozaji kodi. Kwa wawekezaji vilevile mwananchi huyu mara hii amepata wapi mapato au faida ili alipe kodi wakati mtaji amekopa na anatakiwa aanze kurejesha? Serikali itengeneze mazingira rafiki kwa kuwawezesha wananchi wafanye biashara na uwekezaji kwa uhuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili tuweze kuwa sustainable kwenye viwanda lazima pia wanasiasa na private sector waaminiane. Sasa hivi bado kuna kutokuaminiana kati ya wanasiasa au Serikali kwa upande mmoja na sekta binafsi kwa upande mmoja. Serikali iweke mazingira ya kuaminika kwa sekta binafsi ikiwa ni pamoja na kuwa-assure wawekezaji wa nje na wa ndani kwamba waliwekeza mali yao itakuwa salama, haitataifishwa ama mazingira ya uwekezaji yasiwe yanayobadilika badilika sana kuashiria risk kubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.