Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Hon. Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Rais wa Awamu ya Sita ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mama Samia Suluhu Hassan wakati anawaapisha Mawaziri katika hotuba yake alisema haya maneno, naomba ninukuu. ‘Competitiveness ya TTCL iangaliwe vizuri kwa sababu hili ndilo shirika letu na tunategemea lishindane na mashirika mengine ya private sector. Kwa hiyo, competitiveness hiyo ikoje? Tuangalie vizuri tutoe nini, tuache nini, turekebishe ndani ya TTCL ili shirika lisimame vizuri’. Mwisho wa kunukuu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiiangalia nukuu hii ina maana nzito na kubwa sana katika mustakabali wa maendeleo pamoja na ushindani wa Shirika letu la TTCL. Imesemwa hapa na baadhi wa Wabunge kwamba kila mwaka mashirika binafsi ama mashirika shindani na TTCL yanawekeza kati ya milioni 100 dola mpaka milioni 150. Lakini, shirika letu la TTCL linawekeza sifuri. Halafu tunategemea hapa uwepo ushindani ama uwepo ufanisi wa biashara katika shirika letu hili la TTCL na mashirika haya mengine shindani ya simu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, imagine shirika giant kama Vodacom kila mwaka linawekeza milioni 100 lakini kashirika ketu ka-dwarf kanawekeza sifuri. Kwa hiyo, hapa ule ushindani tunaoutafuta hatuwezi kuupata. Imesemwa hapa teknolojia inakua kila leo na inakua kwa kasi kubwa sana. Kwa maana hiyo, tunapozungumzia teknolojia uwekezaji wake unahitaji fedha nyingi na unahitaji fedha ya kutosha. Sasa tunaambiwa Shirika letu la TTCL ndani ya miaka 10 halijawahi kufanya huo uwekezaji. Mara ya mwisho shirika hili liliwekeza mwaka 2001. Sasa tuangalie kutoka mwaka 2001 mpaka leo 2021 hapa katikati teknolojia ime-change kwa kasi na kiasi gani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesisitiza tena, akina Vodacom wanawekeza kiasi kikubwa lakini sisi ndani ya miaka 10 mfululizo tumewekeza sifuri, sifuri. Sasa kwa kuwa sasa hivi Tanzania tumekuwa tunaelewa sana masuala ya mpira hapo ukifanya ulinganifu yaani uichukue ndondo cup iende ikacheza kule Barcelona. Ama uichukue Simba iende ikacheze na Arsenal. Juzi wamecheza na Kaiza wamefungwa goli nne, sasa pata picha iende ikacheze na Barcelona, majibu na matokeo hapa wote tunayo kwamba itachezea kipigo cha mbwa koko. Kwa hiyo, ninatoa mfano huu kujaribu kuonesha kwamba Arsenal ndiyo giant hawa Vodacom halafu Simba ndiyo hii ndondo cup ninayotolea mfano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ama hakika hatuwezi kupata tija inayotafutwa. Kwa hiyo ushauri wangu kwa Serikali, Serikali toeni mtaji ipeni TTCL. Malalamiko yote yanayolalamikiwa hapa na pia katika hotuba ya Mheshimiwa Rais ilisema kwamba wawekezaji binafsi wanawekeza
sehemu zenye mvuto wa kibiashara. Kule ndani ndani, interior wenyewe huwa hawawekezi, ni shughuli yetu Serikali kuwekeza. Kwa sababu hiyo, tuna kila sababu Serikali kuipatia mtaji TTCL ili iweze kuwekeza kwa ufanisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili TTCL iweze kusimama, mtaji wake wa awali tu inahitaji bilioni 800 za Kitanzania, huo ni uwekezaji wa awali wa mwanzoni kabisa. Inawezekana kwamba fedha hizi zinaonekana kuwa nyingi kwa sababu tunazo huduma muhimu za kijamii kama afya, elimu na maji pengine sasa Serikali inapata ugumu na ukakasi kupeleka fedha hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanini tusiwaruhusu sasa waende wakakope? Kwa muda mrefu nikiwa mjumbe wa hii Kamati, ushauri tuliokuwa tunaishauri Serikali iruhusuni TTCL iende ikakope concession loan, mkopo wa gharama na masharti nafuu ili iweze kuwekeza ifanye kazi shindani na kazi yenye tija kama ambavyo tayari imeshatanguliwa kusemwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wamesema hapa Waheshimiwa Wabunge kwamba TTCL inaidai Serikali na Wizara fedha nyingi tu za kutosha na ukiangalia ripoti ya CAG ya mwaka 2019/20 katika ukurasa wake wa 337 inasema kwamba TTCL ilipaswa ilipwe zaidi ya shilingi bilioni 15. Hii ni kutokana na huduma ya mkongo. Lakini ripoti ya Kamati imetuambia mpaka hivi leo tayari imeshafika dola za Kimarekani milioni 68. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maana hiyo, tunaweza tukaona ni fedha kiasi gani ambayo TTCL wanaitafuta, Serikali mko mmeishikilia. Kinachoumiza hapa, TTCL inatoa mapato yake ya ndani kwa ajili ya kuendesha na kuhudumia mkonge ambapo taasisi binafsi zinatoa hizi huduma za simu kwa kupitia mkongo huo. Niseme kuwa wanalipa, lakini kile kinacholipwa kinaenda kwenye Wizara, sasa tunamkamua ng’ombe huyu TTCL pasipo kumlisha majani. Kwa maana hiyo, Serikali muda umefika wa kuhakikisha mnatoa hela mnawapa TTCL ili waweze kufanya kazi yenye tija.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia ukiangalia ripoti hiyo hiyo ya CAG inasema TTCL inadai Serikali madeni ya huko nyuma ya miaka 10 karibu bilioni 40. Kwa hiyo, kuna hizi milioni 68, kuna hizi bilioni 40, zote hizi tukiwapatia TTCL angalau watakuwa na sehemu ya kuanzia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia imesemwa hapa naomba nisisitize kwamba taasisi ama mashirika ya umma yanapata huduma kutoka katika shirika letu hili la TTCL lakini kimsingi hawalipi. Wanapata huduma ya Internet, wanapata huduma ya data, wanapata huduma ya simu, hawalipi! Sasa tukitegemea kwamba eti siku moja TTCL ije ifanye maajabu hii TTCL itakuwa tu kama zombie, ilikuwepo, inakufa, tukaifufua kwa sheria tena mpya sijui 2017 tulifanya marekebisho ya sheria, leo tunajaribu kushauri ten ana tena lakini bado Serikali haitaki kupokea ushauri wetu. Ama hakika, hili shirika litakufa tena halafu tutegemee litakuja litafufuka tena huko mbele ya safari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria ya manunuzi, Sheria ya Manunuzi ya Umma tunaiona ni kwa jinsi gani ambavyo ina mchakato mrefu na mgumu. Kwa mashirika kama TTCL na yanayofanana na hayo kama ATCL, hebu sasa Serikali ifike wakati, ifike mahali mtengeneze kanuni mahsusi kwa ajili ya mashirika haya ya umma yanayofanya kazi kibiashara, kwa sababu leo Vodacom wakitaka kununua mitambo mipya, wakikaa tu ile Bodi, wakijadili wakiamua ikionekana inafaa, kesho wanaenda kununua. Lakini, TTCL, ni mchakato utachukua mwezi mzima hata mitatu ili waweze kukidhi mahitaji ya Sheria ya Manunuzi ya Umma ili waweze kununua hiyo mitambo, wafunge mitambo kwa ajili ya kuweza kutoa huduma stahiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho nimalizie na Mkoa wangu wa Pwani. Maeneo mengi ndani ya Mkoa wetu wa Pwani kumekuwa na kusuasua kwa mawasiliano. Ukichukua kwa mfano katika Wilaya ya Mkuranga maeneo ya Sotele, Chamgoni, Kibuyuni pamoja na Mbezi, huku mawasiliano ya simu imekuwa ni changamoto. Lakini pia kwa upande wa wilaya ya Kibiti, maeneo ya kule Delta, Msala kule, Kihomboloni, changamoto kubwa ya mawasiliano. Pia ukichukua kwa upande wa Mafia, visiwa vya Jibondo na visiwa vya Chole, mawasiliano yamekuwa yakisuasua. Hata kule kwa Mheshimiwa Jaffo, maeneo ya Mafizi, maeneo ya Manyani, vikumburu, mawasiliano yamekuwa ya kusuasua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, nakushukuru sana, tunamuomba Mheshimiwa Waziri aje na majibu, pasipo hivyo, jioni tunakusudia kushika shilingi. Naunga mkono hoja. (Makofi)