Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Hon. Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuchangia Wizara hii ya Mawasiliano. Wenzangu wamechangia zaidi kwenye maeneo mengi ambayo ni mazuri lakini mimi nitachangia katika maeneokama matatu. Kwanza nianze kwa kuipongeza Wizara hii kwa namna ilivyoweza kudhibiti hasa wizi unaotokana na fedha ambazo zimekuwa zikiibiwa kwenye simu za kimataifa. Naipongeza sana Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Wizara imeweza kudhibiti kwa kiwango kikubwa wizi unaotokana na mitandao. Wizi wa ndani kwa sasa hivi umeongezeka kwa kiasi kikubwa na kwa sababu kuna TCRA vile vitengo vya Cibber crime vina uwezo wa ku-tress hawa wezi. Kwa sababu sasa hivi mtu anakuibia kama alivyosema mchangiaji nadhani alikuwa ni wa pili. Watu wanaiba kwa kutumia mitandao na zile simu zinajulikana na wale watu wanaendelea kutumia zile simu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano nikisikia Tigo wamepiga wameniambia hapa ni customer service huwa nakata pale pale sisikilizi chochote, kwa sababu mimi ni mmoja wa wahanga. Nilipigiwa customer service ya Tigo walivyoniambia tu ni customer service nikawaambia kwamba nitawaaminije kama ni ninyi? Wakanipa data zangu zote ambazo nimefanya ile miamala ya mwisho. Kwa hiyo nikawaambia hakuna shida, wakaniambia tumekuongeza kutoka kutuma shilingi 3,000,000 sasa utatuma shilingi 5,000,000 kuna ujumbe unakuja hapo utabonyeza okay. Ujumbe kweli ulikuja nilipo bonyeza okay nikaambiwa nimetuma shilingi 711,000 na kila kilichopo nikabaki na zero balance.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ninavyoamini ni kwamba inawezekana hawa wengine pia ni watumishi wa mitandao hii au ni wale ambao wanafundisha wenzao namna ya kutuibia. Wasiwasi wangu ni kwamba inaweza ikafika mahali kwa advancement hii ya watu wa mitandao, unaweza ukajikuta hujafanya transaction yoyote lakini huko tunakokwenda unaweza ukajikuta unaangalia balance yako kwenye simu hakuna senti tano. Kwa hiyo naishauri Wizara awa wenzetu upande wa polisi ambao tunaambiwa kwamba ndio tuwe tunaripoti tunapotapeliwa, wawe karibu sana na watu wa TCRA ili waweze ku-trace hizo namba ambazo zinafanya wizi huo wa kimtandao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala lingine hili ni la kiusalama mimi na kerwa sana, unapiga simu yako na hili ni mitandao karibu yote. Unapiga simu, kabla haijaanza kuita wewe unapewa matangazo, simu yako inaunganishwa, bonyeza sijui, hash sijui, yanaanza matangazo halafu simu ndio inaita. Sasa mimi najiuliza kama ulikuwa unapiga simu ya emergency labda mtu kavamiwa labda na majambazi,
anapiga simu ili labda Polisi wapokee ile simu, yanaanza matangazao yao ambayo sisi hatujawaomba kama tunataka hayo matangazo kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, matokeo yake wewe wakati unasikiliza matangazo yale, unaweza ukapata hasara, kwa nini wasiendelee na matangazo yao kwa mitindo mingine, lakini mteja yeye akipiga ile simu iite moja kwa moja kuliko kuikawiza kwa sababu ya mambo ya kiusalama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Minara ya Simu; miji inaendelea sana, kwa mfano mimi nime-experience kitu kimoja na ni wengi hapa Dodoma na sasa muda mrefu kunakuwa na shida ya simu zetu wenyewe either kupiga au hata kupatikana. Nahisi ni conjunction ya mitambo yenyewe, yaani kwa maana ya minara. Wakati mji kama Dodoma haujawa Jiji, minara ilikuwa ni hiyo hiyo iliyopo na kama imeongezeka ni michache sana. Sasa matokeo yake kunakuwa na foleni kubwa sana ya simu na meseji. Unaweza ukatuma meseji leo ikawa delivered kesho. Pia unapopiga simu kunakuwa na shida ya kupatikana kwa simu. Kwa hiyo, nawaomba Wizara waweze kuongeza minara hii ya simu ili mawasiliano yaweze kuwa mazuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho, naomba sana Ndugu yangu Waziri Ndugulile, jiografia ya Tabora anaijua, kwa mfano, Jimbo langu la Tabora Mjini linaitwa mjini tu, lakini lina vijiji 41. Vijiji vingi havina mawasiliano ya simu, ukienda kwa mfano, Kata za Ndevelwa, Uyui, Kabila, Ntarikwa, Tumbi hizo ni kata za nje, ukienda Ikomwa ambayo inapakana na Nzega kule mawasiliano ya simu ni magumu sana. Hata hivyo, pale pale mjini eneo la Kipalapala ambapo halizidi kilometa mbili, kuna shida ya mtandao wa simu. Kwa hiyo naomba ndugu yangu Ndugulile atufikirie kupeleka minara mingine ya simu katika maeneo yale ili mawasiliano yaweze kuwa mazuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na naunga mkono hoja. (Makofi)