Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naunga mkono hoja asilimia 100. Manyoni ni Wilaya ya zamani (kongwe) na Wilaya ya kwanza kuwa na Mkuu wa Wilaya Mwafirika. Tatizo kubwa Manyoni hasa Manyoni Mashariki hatuna kiwanda cha kati hata kimoja. Naipongeza Serikali imepata eneo kwa ajili ya Ukanda wa EPZ. Tunaomba tafadhali Serikali itenge fedha kwa ajili kuanza ujenzi wa viwanda ndani ya EPZ area.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali ianze kutujengea kiwanda cha kukamua mafuta ya alizeti (sunflower) kwa kujenga kiwanda cha kukamua mafuta ya alizeti. kwa kufanya hili itakuwa imetoa hamasa kubwa kwa wakulima wetu wa alizeti katika Wilaya nzima ya Manyoni na hata Wilaya jirani za Chemba (Dodoma) na kadhalika. Aidha itatoa ajira kwa wingi kwa Wanamanyoni na maeneo mengine ya nchi. Mwisho viwanda hivi vitaongeza pato la Taifa kupitia kodi, nawasilisha na naunga mkono hoja.