Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

Hon. Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

MHE. KENETH E. NOLLO: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nashukuru kwa kunipa nafasi hii ili niweze kuchangia katika Wizara hii ya Ujenzi. Nilitaka nichangie katika maeneo mawili. Kwanza nichangie kuhusu bandari yetu ya Dar es Salaam na vile vile nitachangia kuhusu suala zima la barabara. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, bandari yetu ya Dar es Salaam ni bandari inayohudumia nchi sita katika ukanda wetu huu, lakini bandari yetu hii imekuwa na changamoto nyingi kwa maana ya efficiency ya vitu vinavyokuja kuweza kutoka sasa kwenda kwenye nchi wanazotegemea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Benki ya Dunia, inasema nchi majirani wanaotumia Bandari ya Dar es Salaam, kwa ujumla wanapata hasara ya dola milioni 830 collectively kutokana na; niite ni uzembe unaotoka kwenye bandari yetu, kwa maana ya kuchelewa kwa muda wa vitu kutoka na hata urasimu usio wa lazima pamoja na udokozi unaofanyika bandarini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, World Bank wanasema bandari yetu ukilinganisha na bandari washindani katika ukanda wetu, ya kwetu inaonekana iko expensive kwa vigezo vyote hivyo. Vile vile wanasema Tanzania ikiamua kusimamia bandari yake, inaweza kuondoa loss ya shilingi almost bilioni 175 ambayo ni total loss kwenye economy pamoja na loss ya revenue tunazozikosa kwenye bandari yetu. Kwa hiyo, ninachotaka kusema kwa wenzetu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, ipo haja kubwa sana ya kusimamia bandari yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia, sijui kuna kigugumizi cha nini? Tumeona nchi kama Singapore wanatumia bandari na viwanja vya ndege, wameendelea, sisi tunataka tupate miujiza ya aina gani? Pamekuwa na mizengwe mikubwa sana kwenye bandari yetu. Kwa hiyo, nataka Wizara hii na Mheshimiwa Waziri anasikiam hebu wakijite kwa ajili ya kuiboresha bandari yetu kwa kuondoa tu urasimu ambavyo ni vitu vya kawaida. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikija kwenye suala la barabara, Wizara hii imeonekana kufanya kazi nzuri kwa kutumia agency ya TANROADS, lakini hawapati fedha ya kutosha. Kwa miaka mitano mfululizo, bajeti hii haijaongezeka, lakini kazi walioifanya ni kubwa. Sasa tunategemea miujiza gani kama chombo hiki kinachotusaidia kwa kuunganisha nchi yetu katika barabara, lakini bado wanapata fedha kidogo? Kwa hiyo, hili tuliangalie, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi iongezewe fedha za kutosha na hata bajeti yenyewe basi iweze kutekelezwa kwa kiasi kikubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, alipokuwa kwenye kampeni pale Manyoni, aliahidi kutengeneza barabara kwa kiwango cha lami kutoka Manyoni kuja Itigi - Heka - Sanza - Chali kwenye Jimbo langu la Bahi Kijiji cha Chali; na barabara hii ni muhimu sana, maana yake ukija Halmashauri ya Manyoni na Bahi, tunaitegemea sana kwa maana ya shughuli za kiuchumi katika Mji huu wa Dodoma. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, barabara hii ikitengenezwa kwa kiwango cha lami kama nilivyotaja, kuanzia Manyoni - Itigi - Heka kuja - Chali Igongo - Chali Makulu - Chali Isanga, unakuja unatokezea Chipanga unakuja Mpalanga – Bihawana, utakuwa umetengeneza link kubwa sana ambayo itachochea uchumi katika Mkoa wa Dodoma. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo mengi barabara zimeonyeshwa, lakini kuna vitu vingine ambavyo ukiangalia huwezi ukaelewa.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)


MHE. KENETH E. NOLLO: Naunga Mkono hoja Ahsante sana.