Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

hon Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nichukue fursa hii kukushukuru kwa kunipa nafasi hii ili niweze kuchangia bajeti ya Wizara ya Ujenzi. Kwanza nilikuwa namwangalia hapa Waziri wa Ujenzi, mara nyingi amekuwa anajishika kichwa, anajishika shavu, kwa kweli tunapaswa tumsaidie.

Mheshimiwa Naibu Spika, kule kwangu Mtwara tuna barabara ya Mnivata ya kilometa 160; Mnivata - Mtwara mpaka Masasi. Barabara ile kwenye bajeti humu tumetengewa shilingi bilioni tatu. Kwa hali ya kawaida ukipiga mahesabu ya kilometa moja kujenga barabara ya lami, lami standard nadhani ni zaidi ya shilingi bilioni moja na something.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hizi shilingi bilioni tatu tunakwenda kutengenezewa kilometa tatu. Barabara hii sasa ina miaka takribani 10. Katika bajeti zote za miaka 10 tumetengenezewa kilometa 50. Naomba kwamba sasa kuna kila sababu, kwa kuwa barabara hii inaunganisha baadhi ya barabara zinazokwenda kwenye wilaya nyingine, pia ni barabara ya kibiashara. Kwa hiyo, tunakosa kufanya biashara zile za kisasa hasa kwa kutumia barabara hiyo kwa sababu barabara siyo nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna barabara ya kutoka Mtwara kuelekea Mahurunga; barabara hii hatujaona kwenye bajeti kama imetengewa fedha. Barabara hii toka imeanza kutengenezwa sasa hivi ina kiwango cha lami kilometa ambazo hazizidi sita au saba, takribani ina miaka zaidi ya 15 na iko TANROADS. Naomba barabara hii sasa itengewe fedha za kutosha ili tuweze kupata barabara ya lami. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii kule inakokwenda ndiyo kwenye mpaka baina ya Msumbiji na Tanzania, lakini kumekuwa kuna matukio mengi ambayo yanatokea, watu wetu, watu wa Idara, watu wa usalama na watu wengine wanashindwa kufika kwa wakati kwenye maeneo hayo, kwa sababu barabara ni mbaya hazipitiki. Tunaomba Serikali mtusaidie kwenye hii barabara. (Makofi)


Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nizungumzie barabara ya Kibiti – Lindi – Mtwara. Barabara hii kwa sasa hivi haipitiki, ni barabara ambayo tayari imeharibika, imekufa kutokana na malori ambayo yanabeba ufuta, korosho, na mahindi yanayopelekwa Dar es Salaam. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, rai yangu kwako, tunayo Bandari ya Mtwara; bandari hii imetumia shilingi bilioni 157 na fedha zile tumeziwekeza pale ili bandari ile ifanye kazi. Nataka nitoe angalizo, leo kuna makampuni yanayoleta mafuta, Serikali imeelekeza kwenye makampuni yanayoleta mafuta kwamba kwa watu wa mikoa ya kusini, itumike bandari ya Mtwara wa kubeba mafuta. Ni kitu gani kinashindikana sasa tukaelekeza kwamba korosho zote za Mtwara zipitie Bandari ya Mtwara; ufuta wote unaolimwa Lindi na Mtwara upitie Bandari ya Mtwara; na mahindi yote yanayolimwa yapitie bandari ya Mtwara? Kuna nini hapa? Naomba kufanya maintenance kwenye barabara yetu ya lami kutoka Mtwara kuja Dar es Salaam a lot of shillings tutazitumia pale. Hivyo maintenance hizi tunazozifanya za kila siku kama tungeamua sasa fedha hizi tuzielekeze kwenye ujenzi wa barabara tungekuwa hatulalamiki hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo barabara ya Mtwara – Kibiti – Lindi, kila ukipita barabara ile, kila baada ya miezi miwili unakutana na shida. Mkandarasi yuko barabarani na anatengeneza barabara ile kwa ajili ya service. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)