Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

Hon. Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mwongozo wa Spika.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Zuberi Kuchauka.

MWONGOZO WA SPIKA

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba mwongozo wako…

NAIBU SPIKA: Kanuni?

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, Kanuni ya 76. Naomba mwongozo wako kwa sababu hii bajeti tunayojadili ni bajeti muhimu sana na haya tunayowaambia tunaiambia Serikali na Serikali ni mtambuka. Humu ndani tuna Mawaziri sita tu, na Naibu Mawaziri wako saba tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano kama haya mambo ya kutokupeleka fedha kwenye bajeti yanahusu Wizara ya Fedha; kuna mambo mengine ya vibali vya ujenzi, GN na nini, inahusu mambo ya Mazingira na nini. Lakini humu tuna Mawaziri sita tu na Naibu Mawaziri wako saba tu; haya mambo yanakwendaje?

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba mwongozo wako.

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, amesimama Mheshimiwa Zuberi Kuchauka akiomba Mwongozo wa Kiti kuhusu kuwepo kwa baadhi ya Mawaziri hapa na wengine yeye hawaoni, kwa hiyo, anajiuliza yaani haya tunayozungumza je na wao watayachukua kwa uzito wa namna hii?

Waheshimiwa Wabunge, kwanza, kama alivyosema yeye mwenyewe ni kwamba Serikali ni moja, kwa hiyo, anayesikiliza atafikisha huo ujumbe; moja. Lakini la pili, hata mimi wakati nazungumza nimeeleza hapa kuhusu Waziri wa Ujenzi lakini nikasema pia Waziri wa TAMISEMI, najua nini, humu ndani lazima Waziri wa TAMISEMI atapata taarifa kwamba yeye na Waziri wa Ujenzi wanahitajika kwenda Mbeya.

Maana yake ni nini; hapa tulimsoma Mheshimiwa William Lukuvi, kwamba ndiye msimamizi wa Shughuli za Serikali Bungeni, Waziri Mkuu hayupo. Kwa hiyo, madam yeye amekaa pale, uwe na uhakika kwamba shughuli zote za Serikali humu ndani zinao usimamizi. Kwa hiyo ujumbe wataupata kila mtu vile unavyostahili. (Makofi)

Kwa hiyo, hata mpiga sarakasi ujumbe wake utafika kwenye sehemu inayotakiwa kwa sababu miundombinu anayosema hizi ni zile barabara kubwa. Lakini barabara kubwa haziwezi kufanya kazi peke yake bila barabara ndogo ambazo ni za TAMISEMI. Kwa hiyo, wakati wa TAMISEMI Waziri wa Ujenzi na Manaibu wake walikuwa wanasikiliza kwamba hizi barabara wanazozisema Wabunge zinailisha barabara gani kubwa.

Na sasa na yeye anaposikiliza kuhusu barabara kubwa anazoeleza Mbunge yeyote, barabara kubwa au kama hivi tunavyosema ujenzi wa reli na vitu kama hivyo, wao kama Serikali wanafahamu ni barabara zipi zitatakiwa kulishana namna hiyo.

Kwa hiyo msiwe na wasiwasi Waheshimiwa Wabunge michango yenu ndiyo maana huwa mnazungumza na mimi hapa mbele, na ndiyo kazi yangu. Mnazungumza na mimi, ukishazungumza na mimi usiwe na wasiwasi, hata kama Waziri wa Ujenzi hakuwepo hapa ujumbe ataupata. Ahsante sana. (Makofi)