Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikushukuru sana kwa kunipa nafasi kuchangia. Namshukuru pia Waziri wa Afya, Mheshimiwa Dkt. Dorothy pamoja na Naibu Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa dakika chache sana nizitumie dakika zangu vizuri. Nataka kuzungumza kwa habari ya chanjo zinazoitwa corona vaccine.

Mheshimiwa Nainu Spika, niseme kwa ufupi kwamba mimi siko kinyume na chanjo za corona, hapana, wala siko kinyume na chanjo yoyote ile. Kwenye mazungumzo yangu, mtu asininukuu kwamba napinga chajo, hapana, kwa sababu tayari Tanzania tulishachanjwa; chanjo ya Kifua Kikuu tayari tulishachanjwa; chanjo ya Surua tayari; chanjo ya Kifaduro tayari; chanjo ya Polio tayari; na sasa hivi kuna chanjo zinaendelea kama chanjo ya Homa ya Ini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, siko kinyume na chanjo kwa sababu tayari chanjo ziko Tanzania na watu wanaendelea kuchanjwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kitu ambacho niko makini nacho sana ni aina ya chanjo inayoitwa chanjo ya corona virus ilivyokuja na study yake. Chanjo hii ni tofauti na chanjo nyingine zote ambazo zimekuwepo duniani. Dunia imekuwa na aina ya chanjo zinaitwa attenuation. Maana yake ni kwamba virus wa corona wanapunguzwa nguvu, wanaondolewa properties, halafu wanaingizwa ndani ya mwili wa mtu, halafu antibodies zina-react, immunity inatengenezwa. Hii ndiyo aina ya chanjo ambayo imekuwepo miaka yote na siku zote. Chanjo hii kukamilika inagharimu miaka minane mpaka kumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, chanjo hii inayoitwa chanjo ya corona ni chanjo ya mwendokasi, miezi miwili, miezi mitatu au miezi minne tayari. Unapojaribu kuuliza kwamba hii chanjo kwa nini imekuwa na haraka sana? Kuna magonjwa mengi kama Malaria na mengine ambayo tungetegemea mfanye haraka haraka kupata chanjo ili watu waokolowe. Wanasema sababu ya kwanza, kwa sababu teknolojia imeongezeka; sababu ya pili, wame-mobilize resources kutoka kwenye makampuni mengi duniani; na sababu nyingine ni kwamba ni kwa sababu ni pandemic, nami sikatai.

Mheshimiwa Naibu Spika, tekhnolojia ya chanjo hii inaitwa MRA. Maana yake, ni aina ya chanjo ambayo wanachukua generic material ya virus halafu wanaingiza kwenye MRA ya mtu, baadaye mtu, wanasema kwamba hataingilia na gene, lakini wanasema wanaingiza kwenye genetical material yaani genetical material za virus zinaingizwa kwenye cell ya mtu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tofauti ya mtu na mnyama ni RMA, DNA na GINOS ambazo ndio genes. Huo ni utu wa mtu tofauti na mnyama. Chanjo hii inaingia mpaka kwenye RNA, chanjo hii inaingia kwenye DNA, kwenye GINOS, kwenye utu wa mtu. Hatujajua baada ya chanjo hii atazaliwa mtu wa namna gani baada ya miaka kumi, baada ya miaka mitano, baada ya miaka sita, hatujajua mpaka leo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, bahati mbaya sana, nifunguke kidogo na hekima yako ikikuruhusu utaniongezea muda kidogo kama ukiisha, kwa sababu hoja yangu ina national concern. Mashirika duniani kwa mfano, Marekani kuna shirika ambalo linaruhusu dawa zianze kupitishwa, linaitwa CDC (Center for Disease, Control and Prevention).

Mheshimiwa Naibu Spika, shirika lingine linaitwa FDA ambayo ni Food and Drug Administration; haya ndiyo mashirika ya Kimarekani yanayo-authorize dawa zote kwa ajili ya matumizi ya binadamu. Chanjo hizi zote unazoziona, hazijawa authorized na mashirika haya. Kuna kishirika kidogo ambacho kinaitwa Emergence Use Authorization.

Mheshimiwa Naibu Spika, hiki kishirika kinaidhinisha dawa ambazo ni dharura, ambazo zinatakiwa ziende haraka. Sheria ya hawa Emergences Use Authorization ni kwamba kwa sababu dawa haijafanyiwa utafiti wa kutosha miaka mingi, kwa hiyo, inaruhusiwa emergence kwa sababu ya uhitaji wa dunia. Madhara yatakayowapata wale, liability haziko juu ya hii kampuni, ziko juu ya mtumiaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa najaribu kuwaza, nikiangalia kwa mfano chanjo ambazo ziko tayari zimesharuhusiwa kuanza kwa mfano, kuna chanjo ya kwanza inaitwa Jonhson Johnson, imeruhusiwa na Wamarekani ambayo tarehe 27 Februari, 2021 ndiyo ilikuwa authorized kutumika emergency, lakini kwenye website yao, watengeneza chanyo wenyewe wanasema madhara au side effect ya chanjo hii: kwanza, kushindwa kupumua sawasawa; pili, kuvimba kwenye uso na kwenye throat; tatu, mapigo ya moyo yanakwenda haraka; nne, bad rush kwenye mwili; tano dizziness; na sita, damu kuganda kwenye mwili. Hii ni kwenye website yao. Sasa kama watengenezaji wa chanjo wenyewe wanaonesha kwenye website yao kuna shida hiyo, ni vizuri sasa tuwe makini. Najua Mheshimiwa Rais kwa hekima yake ameunda Kamati inayofuatilia hayo, lakini mimi kama Mbunge nina haja ya ku-discuss na ku-alert kwamba wawe makini wanapochagua aina ya chanjo hizi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nyingine ya pili inaitwa AstraZeneca, ambayo imetengenezwa Oxford kule UK. Yenyewe kwenye website yao wanasema side effect yake ya kwanza ni damu kuganda; na ya pili ni kifo. Ni kifo ndiyo. Wanasema, kwenye kifo hapa, wanaweza kufa watu labda kumi out of hundred, lakini kwenye website yao wanaonyesha kwamba death may occur, lakini dunia bila kufanya research, bila kuwaza watu wanakimbilia kupata chanjo kwa sababu ya fear ya corona.

Mheshimiwa Naibu Spika, nyingine inaitwa Moderna ambayo ni ya USA na nyingine inatiwa Pfizer ambayo ni ya Ujerumani. Kwa ujumla chanjo hizi zote zinaonyesha side effect ni kuganda damu, kushindwa kupumua na kifo.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ni kweli, tukikataa chanjo tunaweza kuwekewa ban ya kusafiri kwenda Ulaya kwa sababu hatujachanjwa. Tunakabiliwa na uchaguzi mbaya sana; tuchanjwe kitu tusichokijua sawa sawa au tusichanjwe tuzuiwe kwenda Ulaya. Naomba sana Wizara ya Afya wajaribu kuangalia kwa makini sana kwenye suala ya chanjo. Waangalie madhara ya sasa, madhara ya siku zijazo na madhara ya Taifa. Jambo hili ni la muhimu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niruhusu kidogo niongeze kidogo. Matatizo tuliyonayo ni kufikiri kila kinachotoka Ulaya kinafaa kwetu; and this is a problem we face. Our colonizers (watawala wetu) walitujengea ufahamu kwamba kikitoka kwao kinafaa. Jana kuna mtu mmoja anaitwa Dkt. Edward Fleming ambaye ni kati ya watu walioshiriki kutengeneza mojawapo ya chanjo, alikuwa ameandika barua kwa Rais wa Marekani, nina rekodi, amesema, anashauri hizi chanjo ziachwe mara moja kwa sababu madhara yake ni makubwa kuliko faifa yake kwa prevention. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naiomba Serikali yangu sikivu pamoja na Wizara ya Afya, before we venture in to what kind of vaccine we should take, tunatakiwa tuwe na wataalam wetu wa hapa. Namba moja, wa-analyse content. Haya majina ya chanjo ni business name, lakini kuna generic name that includes the content, kuna nini ndani ya chanjo, wa-analyse matatizo yatakayotupata sisi tutakaochanjwa na watoto wetu baadaye. Kwa sababu shida ikiingia kwenye DNA na kwenye gene na RNA, ndiyo utu wa mtu. Ina-send message miaka ijayo mtu azaliwe wa namna gani? Madhara yanaweza kuwa siyo leo, but in 20 or 30 years to come tunaweza kuwa na Watanzania wasioweza kufikiri vizuri, wasio na maamuzi mazuri na Taifa letu litashindwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba sana Wizara ya Afya, before we know which method we implement, tufanye due-diligence ya kuifuatilia hii chanjo ni ya namna gani? Pia tusome website.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niongezee jambo moja kwamba anything kule Marekani au kule Ulaya; Ulaya kuna organization inaitwa EMA maana yake ni European Medicine Agents ambayo na yenyewe ina- authorize dawa zote ndiyo zinatumika. Hizi agency zote; agency ya Ulaya na agency za Marekani hazija-authorize zenyewe, zimewekwa kwenye ka-institution kanakoruhusiwa kuwa-authorize emergence kule na matokeo ya kuwa-authorize emergence, huyo aliyetengeneza dawa hana madhara, kwamba ni wewe mwenyewe, utajijua wewe mwenyewe; na wanasema kwamba iwe inatumika huku inafanyiwa uchunguzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni ujinga kuruhusu Taifa zima kuwa experiment ya majaribio, eti kwa sababu tuna haraka ya Corona. I know Corona is dangerous, yes but it is more dangerous for us to allow the all natives, Watanzania wote milioni 50 wachanjwe eti ndiyo tuwe tunaangalia matokea, tunaripoti kwenye hizi institution. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba sana hili suala liangaliwe kwa makini, lifanyiwe kazi na mwisho wa siku kila silaha itakayofanyika juu yetu haitafanikiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)