Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuweza kuchangia hoja iliyopo mbele yetu. Najua muda ni mchache sana lakini nitajitahidi. Naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri kwa maandalizi ya bajeti hii, lakini sambamba na hilo naomba nitoe ushauri kwamba, pamoja na kwamba Serikali imeweka vipaumbee vyake katika Fungu la 52 pamoja na Fungu 53, naomba nitoe ushauri ufuatao:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la kuimarisha huduma ya chanjo, naomba niishauri Serikali kwenye hii issue ya chanjo ya ugonjwa wa ini ni kwamba chanjo hii ili ukitaka kuchanja inabidi utoe shilingi 20,000 pale unapokwenda kupima halafu baadaye inabidi utoe Shilingi 10,000, Shilingi 10,000, Shilingi 10,000 kwa ajili ya dozi. Naomba Serikali ione ili kusudi wale wananchi wa pembezoni waweze kuweza kuchanja chanjo hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine nataka nizungumzie kuhusiana na wanawake ambao wanakwenda kujifungua. Taarifa zinaonesha kwamba imeonekana kwamba wanawake wengi wanajitahidi kwenda kujifungulia kwenye kliniki na hospitali, lakini bado kuna wale wachache ambao bado wanajifungua kwa waganga au wakunga wa jadi. Nashauri elimu iendelee ili kusudi watoto wawe salama na akinamama wawe salama, ni vizuri wakaenda kujifungulia katika hospitali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile napenda nizungumzie suala la magonjwa ya kuambukiza ikiwemo Malaria, Kifua Kikuu na hasa UKIMWI nijikite zaidi kwenye UKIMWI.

Mheshimiwa Naibu Spika, wenzangu wengi sana wamezungumzia kuhusu hili suala la UKIMWI na inaonyesha kabisa kwamba kundi kubwa ambalo liko kwenye hatari ya kuambukizwa UKIMWI ni hawa Watoto kuanzia miaka 14 mpaka 24. Takwimu zinaonyesha kwa mfano katika Mkoa wa Njombe kwamba maambukizi yako kwa asilimia kama 11.3 kwamba hawa Watoto wenye umri kati ya miaka hiyo 14 na 24 katika wale vijana 10 wanaopimwa wa kike wanaonekana kwamba wanamaambukizi makubwa sana. Kwa hiyo, ina maana kwamba Watoto wa kike 8wanapata maambukizi katika 10. Kwa hiyo, nilikuwa nashauri akinababa hebu muwaonee huruma hawa Watoto, kwasababu inaonekana kwamba mmeacha kwenda kwa akinamama watu wazima mnawafuata hawa Watoto. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kwa wale wa baba ambao wanakwenda kuwadanganya hawa Watoto hebu waacheni hawa Watoto hebu waacheni hawa Watoto wasome wafikie malengo yao. Kwa hiyo nilikuwa naomba nishauri. Lakini sambamba na hilo wenzangu wamezungumza kuhusiana na suala zima la kwenda kupima UKIMWI tunaendelea kuhamasisha wanaume waende wakapime Ukimwi kwasababu kama hawa Watoto wa kike wadogo wanakuwa hawana maambukizi haya maambukizi mapya wanayapata wapi? Ina maana kwamba wanayapata kwa wale akina baba ambao hawajapima Ukimwi. Kwa hiyo nilikuwa naomba nishauri kwamba akina baba bado waendelee kujitokeza kupima Ukimwi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo jingine nililokuwa nataka kuzungumzia ni kuhusiana na huduma za uzazi wa mpango. Ni kwamba inaonyesha kwamba katika hotuba imeonyesha kwamba katika hotuba inaonyesha kwamba kuanzia Julai 2020 hadi Machi, 2021 inaonesha takwimu za akinamama ambao wamepata uzazi wa mpango ni 4,926,183 kati ya akinamama 13,841,830 sawa na asilimia 36. Hii bado ni asilimia ndogo kwa hiyo nilikuwa naiomba Serikali pia iwekeze sana kwenye suala zima la uzazi wa mpango ili kusudi tuweze kupanga mipango yetu ya maendeleo vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nilikuwa naomba nizungumzie kuhusiana na huu mpango kazi wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na Watoto MTAKUWA wa mwaka 2017 hadi 2018, 2021/2022. Najua azma nzuri sana ya Serikali kwa ajili ya mpango huu nikuhakikisha kwamba ukatili unapungua au unakwisha kabisa. Lakini tatizo linakuja kwamba hivi vikundi vya MTAKUWA katika ngazi ya vijiji na kata havipati pesa. Kwa hiyo, nilikuwa naomba Serikali ione Wizara ya Afya pamoja na TAMISEMI washirikiane kuona kwamba zinapangwa bajeti ili kusudi huku katika ngazi za vijiji na kata vikao hivi viweze kukutana kuweza kufanya mikutano yao ili kupinga suala zima la ukatili. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, najua muda siyo Rafikiā€¦

NAIBU SPIKA: Imeshagonga kengele Mheshimiwa.

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Naibu Spika,ahsante sana naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)