Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maji

Hon. Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maji

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi hii kwa niaba ya Wananchi wa Jimbo la Msalala ili nichangie hotuba ya Wizara ya Maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, moja kwa moja nianze kwa kuipongeza Wizara ya Maji kwa kazi kubwa inayoendelea kuifanya. Pia niishukuru Serikali kwa kuona umuhimu wa sasa wa wananchi wa Jimbo la Msalala kupata maji safi na salama. Pia tutakuwa wachoyo wadhila kuishukuru Serikali kwa fedha nyingi ambazo wametutengea sisi Jimbo la Msalala. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imetutengea kiasi cha Sh.4,600,000,000.00 kwa ajili ya miradi mbalimbali katika Jimbo langu la Msalala. Kwa kweli kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Msalala tunakushukuru sana Mheshimiwa Waziri, tunaishukuru sana Serikali lakini pia tunamshukuru sana Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama yetu Samia Suluhu Hassan. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeweza kutengea kiasi cha shilingi milioni 558 katika mradi wa maji ambao utahudumia Vijiji vya Nduku, Ntobo, Busangi. Niombe baada ya fedha hizi kutoka basi ziende haraka iwezekanavyo ili kukamilisha mradi huu ambao ni changu na utaweza kupunguza tatizo la maji katika Kata hii ya Busangi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Waziri na Serikali haijaishia hapo tu, wameenda kutupatia kiasi cha shilingi milioni 250 kwa ajili ya extension katika mradi mkubwa wa maji. Hata hivyo, kuna mradi mkubwa ambao unaitwa Manguirogi ambao ni joint venture kati ya Serikali na Mgodi, hii ni fedha ya CSR. Namwomba Mheshimiwa Waziri baada ya Bunge hili akubali kuambatana nami ili twende kule tukaangalie ili tuweze kufahamu ni kiasi gani Serikali imeweza kuchangia katika mradi huu lakini pia mgodi umechangia kiasi gani? Fedha hizi ni za CSR na tunatamani sana tuone ili tujue chenji yetu imebaki kiasi gani ili kusaidia kusambaza maji katika Kata za Runguya, Ipinda, Segese na maeneo mengine. Mradi huu unatoka Mangu unaishia Irogi, niiombe Serikali bsi iweze kutenga fedha tena kwa ajili ya kufanya extension katika maeneo ya Ikinda Kata za Lunguya, Nyangarata, lakini na maeneo mengine ili kuweza kusaidia na kupunguza tatizo la maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Kata ya Segese inakua kwa kasi sana kwa sasa na matarijio yetu ni kuhakikisha kwamba tunapata maji ya ziwa ili watu waweze kunufaika. Pia tuna Makao Makuu ya Ntobo ambayo kimsingi tunaenda kuyazindua muda si mrefu, niombe mradi huu unaotoka Nduku kuja Ntobo lakini pia mradi huu unaotoka Mangu kuja Irogi extension iweze kufanyika pia maji haya yaweze kusogea katika Makao Makuu ili ituwezeshe kuwafikishia wananchi miundombinu hii ya maji na tuweze kuwahimiza sasa waweze kuwekeza kwa kiwango cha juu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kuna mradi mkubwa ambao umeshakamilika wa Kagongwa – Isaka. Mheshimiwa Waziri kama anakumbuka alikuja kuzindua na Mheshimiwa Rais alikuja pale na alitaja mbele ya Mheshimiwa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli kwamba kuna chenji imebaki. Pia mradi huu unapita katika Kata ya Mwakata ambayo haina maji. Naomba Waziri aone ni namna gani chenji iliyobaki katika mradi unaotoka Kagongwa kwenda Isaka mnaweza kuzipeleka katika Kata ya Mwakata ili sasa na wakazi wa Kata ile waweze kunufaika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia niipongeze Serikali na Mheshimiwa Waziri kwa kututengea kiasi cha shilingi 1,500,000,000 katika Kata za Jana na Mwalugulu. Ni matumaini yangu kama fedha hizi zitaenda haraka na kufanya uzinduzi wa mradi huu utasaidia sana wakazi wa Kata hizi ili na wao waweze kunufaika na mradi huu wa maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimalizie kwa kusema kwamba kumekuwa na changamoto ya bili za maji, nimwombe Mheshimiwa Waziri wakati anakuja kutembelea mradi huu Mangu - Irogi tupate fursa ya kutembelea wananchi na kusikiliza kilio chao juu ya ongezeko la bili za maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, niishauri Wizara ione namna gani wanaweza wakaja na solution ya kuhakikisha kwamba wanatengeneza mfumo mpya ambao utasaidia kupunguza adha ya ongezeko la bili la maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, siyo hivyo tu, niiombe Wizara iweze kuwapatia mafunzo maalum wale wasimamizi kule chini. Hii itawasaidia kutumia miradi hii ya maji ambayo inapelekwa kule na inatumia gharama kubwa ili waone namna gani sasa wanaweza kuanza kusambaza katika miji ya watu na ili wakazi wa maeneo yale waweze kunufaika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niishie hapo, ahsante sana, naunga mkono hoja. (Makofi