Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maji

Hon. Dr. Alfred James Kimea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maji

MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA: Mheshimiwa
Spika,nakushukuru kwa nafasi hii. Pili, nimpongeze Waziri, Naibu Waziri na Katibu Mkuu wa Wizara hii ya Maji, kwa namna wanavyopambana kuona namna gani wanatatua changamoto ya maji kwenye nchi hii.

Mheshimiwa Spika, tunafahamu umuhimu wa maji kwenye jamii zetu. Tunafahamu kwamba kama tunataka jamii au nchi yenye watu wenye afya nzuri tunahitaji maji safi. Kama tunahitaji kuinua kiwango cha elimu wanafunzi wote wa kike na wakiume waweze kwenda kuhudhuria masomo vizuri tunahitaji maji.

Mheshimiwa Spika, kama Mheshimiwa tunahitaji kuinua kiwango cha uchumi wa nchi yetu, kuzuia magonjwa yasiwasumbue watu na tukapoteza fedha nyingi kwenye kutibu magonjwa, tunahitaji maji safi.

Mheshimiwa Spika, nafahamu juhudi kubwa ambazo Serikali inazifanya kutatua changamoto ya maji na zipo takwimu zinazoonyesha kiwango gani cha maji kinapatikana sasa hivi, lakini kwa uhalisia zaidi ya asilimia 50 bado watu hawana access ya maji safi na salama. Ushauri wangu ni nini? Serikali inabidi sasa itoe kipaumbele kikubwa kwenye Sekta ya Maji.

Mheshimiwa Spika, research zinaonyesha kwamba kutatua changamoto ya maji, kuleta maji safi na salama si kwamba tu muhimu kwa afya, lakini pia tunaona zitanyanyua kiwango cha uchumi kama nilivyosema hapo mwanzo. Pia itasabisha kuwe na Taifa la watu wenye furaha kwa ajili tunapata maji safi, watu wanaoga vizuri kabla ya kwenda kazini asubuhi, kwa hiyo maji ni muhimu sana.


Mheshimiwa Spika, statistics zinasema tuki-invest shilingi moja kwenye Sekta ya Maji pamoja na Usafi wa Mazingira inaweza kuiletea ongezeko la uchumi kwa shilingi 12. Investment ya shilingi moja inaweza kuletea pato la Taifa ongezeko la shilingi 12. Kwa hiyo naomba tujitajidi kuongeza investment kwenye sekta ya maji.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu kwa Serikali ni huu; kama tulivyofanya investment kubwa kwenye standard gauge, tulivyofanya investment kubwa kwenye umeme, tunaona tunajenga bwawa la umeme, kwa nini sasa tusiwe na mradi mkubwa wa kimkakati nchi hii ili kutatua tatizo la Maji Tanzania nzima.

Mheshimiwa Spika, tunaweza tusiwe na fedha za kufanya hivyo, lakini tunaweza tukakopa fedha nje ya nchi au ndani ya nchi kwenye vyanzo mbalimbali kama vile Government Bond tuka-invest kwenye changamoto ya maji ili tuweze kutatua tatizo la maji kwa sasa hivi na hata miaka hamsini ijayo. Halafu tutaendelea kulipa deni hilo pole pole lakini tukiwa na uhakika kwamba changamoto ya maji imekwisha kabisa kwenye nchi hii.

Mheshimiwa Spika, mradi mkubwa ambao uta- identify tatizo la maji lipo kiasi gani nchi nzima. Mradi mkubwa ambao uta-identify vyanzo vya maji, tumetajiwa Ziwa Victoria, Tanganyika na Maziwa mengine, Mito na kila mahali. Mradi ambao utasambaza maji nchi nzima, tuji-commit sehemu hii tutaendelea kulipa deni lakini tukiwa tunajua kabisa changamoto ya maji imeisha kwenye nchi hii.

Mheshimiwa Spika, naomba nirudi Jimboni kwangu Korogwe. Nashukuru Mheshimiwa Waziri kaka yangu Aweso kwa commitment yake kubwa kuhakikisha anatusaidia kutatua changamoto ya maji pale Korogwe. Korogwe ina changamoto moja, changamoto iliyokuwepo Korogwe kwanza kuna mradi unaoitwa HTM, huu ni mradi wa miaka mingi, mradi huu unasabisha wakati wowote tunapoomba fedha kwa ajili ya maendeleo ya maji, kutatua changamoto ya maji, tunaambiwa mna Mradi wa HTM. Kwa hiyo, tunaomba Mheshimiwa Waziri ahakikishe anatuleta maji kwenye Mji wa Korogwe bila kuangalia hii HTM. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunamshukuru Waziri kwa sababu kwenye bajeti hii angalau tumepewa hela kidogo, lakini tunaona itatatua angalau changamoto ya maji Korogwe. Nilimwomba milioni 700 kwa ajili ya Kata ya Bagamoyo lakini kwa mwanzo ameniletea milioni 200. Naomba Mheshimiwa Waziri aweze kutumalizia hizo milioni zilizobaki ili kuweza kutatua changamoto ya Maji Korogwe. Tuna imani sana na Mheshimiwa Waziri, tunamwamini na tunajua atatatua changamoto ya maji Korogwe na Tanzania nzima. Mungu ambariki sana.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuchangia Wizara hii na naunga mkono hoja. (Makofi)