Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ASKOFU JASEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii ya kuchangia. Kwanza nikupongeze jana kwenye futari ya CRDB ulipendeza sana na nikaona umeanza kuitwa Ukti, keep it up utafika mahali pazuri sana. Lakini watu wengi sana waliochangia nataka nipate nafasi ya kuchangia hii hoja ya Wizara ya Elimu watu wengi sana waliochangia wamezungumza kwa habari ya curriculum au mitaala. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na mawazo ya watu wengi walikuwa wanachangia wakisema kwamba ni muhimu sana mitaala ya elimu hii kubadilishwa ili iwe skill basic curriculum na sikatai, lakini lipo jambo la muhimu sana ambalo ningependa ku-discuss it is a matter of national concern siyo jambo la tu Wizara ya Elimu peke yake lakini is a matter of national concern na hili jambo lina athiri Wizara ya Elimu directly as far less curriculum is concern.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba ninukuu mchangiaji wa jana aliyechangia anaitwa Mheshimiwa Nusrat Hanje alichangia jambo ambalo nanukuu alitoa kwenye Sera ya Elimu ya mwaka 2014 ambayo inasema kwamba lengo la elimu au objective ya elimu ni kumpa mtu maarifa, ustadi, umahiri, uwezo na mtazamo changa katika kuchangia maendeleo ya nchi. Hivyo ndivyo sera ya elimu ya mwaka 2014 inavyosema. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaanza kuona kwamba objective ya elimu ni kumfanya mtu awe na maarifa awe na ustadi, awe mahiri, awe na uwezo na awe na mtazamo chanya katika kuchangia maendeleo ya nchi. Kwa hiyo, objective ya elimu ni maendeleo ya nchi sasa lipo jambo ambalo ni serious sana ambalo ningefikiri mtu yeyote msomi aliye kwenye Bunge hili anatakiwa aisaidie hii nchi na kizazi kijacho. Kama lengo la elimu ni kumsaidia anayepata elimu ni kuzalisha mtu ambaye ana uwezo wa kuchangia kwenye maendeleo ya nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, then maendeleo ya nchi ni nini, ni muhimu sana nchi hii iwe na maono ya miaka mingi kuhusiana na mambo yanayohusiana na Taifa hili. Niliwahi kuchangia nikasema without vision people perish pasipo maono watu kuangamia. Mataifa mengi sana yaliyoendelea yana vision ya nchi zao unakuta kwa mfano miaka kama 10 iliyopita Wamarekani walikuwa na a hundred years of the new American wa Finland walikuwa na forty years of the Finland development na nchi nyingine, lakini sisi nchi yetu inakuwa haina vision tulikuwa na Mpango wa Maendeleo wa Mkapa ambao unaisha mwaka 2025.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sasa hivi tuna Ilani za Uchaguzi tu na mipango ya muda mfupi miaka mitano, mipango hiyo inaifanya nchi idumae sana kwanini nasema hivyo, nasema hivyo kwasababu panapokuwa na mpango wa muda mrefu kwa mfano Tanzania tukasema tuwe na mpango wa miaka 50 wa maendeleo na tuna kitu gani tunakiita maendeleo, tunaweza kusema kwa mfano maendeleo kwetu sisi kila mtu awe na maji safi na salama, maendeleo kwetu sisi ndani ya miaka 50 kila nyumba ya mtu iwe na umeme, maendeleo sisi ndani ya miaka 50 asiwepo Mtanzania hata mmoja anayekaa kwenye nyumba ya majani.

Mheshimiwa Naibu Spika, maendeleo kwetu sisi asiwepo Mtanzania kijana mwenye uwezo wa kusoma shule akashindwa kwenda chuo kikuu ndani ya miaka 50, maendeleo kwetu sisi kila barabara iwe ya TARURA iwe barabara ya TANROADS iwe la lami, tukaya-define haya maendeleo kwamba kiongozi anayekuja kwenye power atutimizie hayo maendeleo ndani ya miaka 50 na tutaona ubora wa kiongozi ni kwa jinsi gani anayatimiza hayo maendeleo yetu kwa muda mfupi kuliko muda ambao tumejipangia sisi wenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwenye sera ya Elimu nitakuja kwasababu lengo langu ni kuongea sera ya elimu, lakini shinda inayotusumbua sasa hivi tunahitaji Rais mwenye maono ina maana sisi kama nchi hatuna maono. Kwa hiyo, Rais anapoingia madarakani anatimiza maono yake namna ambavyo yeye anatafsiri maendeleo tunajikuta tunaendelea lakini kwa namna ambavyo kiongozi ana-passive maendeleo, lakini kusema ukweli tusingehitaji Rais mwenye maono tungehitaji nchi yenye maono ili Rais atakapoingia atimize maono ya nchi hayo ambayo sisi wenyewe tumejipangia.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kwa mfano kama tungekuwa na maono kwa mfano ndani ya miaka 50 tukasema Wizara ya Elimu tunasema ndani ya miaka 50 tutakuwa na University kila Wilaya, tukasema ndani ya miaka 50 tutakuwa na Hospitali ya Rufaa kila Wilaya kwa hiyo sasa elimu zote zingeanza kujipanga kuelekea hiyo miaka 50. Kwa hiyo, hata wanafunzi wanaosoma wangeiona vision ya nchi, vision ya nchi ni miaka 50 kwa hiyo ndani ya miaka 50 tutakuwa na university kila Wilaya kwa hiyo, kila mtu anayesoma shule angekuwa anajua maprofesa wanatakiwa ma-tutor assistant wanatakiwa, wasomi wanatakiwa kwa hiyo tungemsaidi mwanafunzi kuona mbali kwa sababu ameiona vision ya Taifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tukisema kwa mfano kwenye miaka 50 kila Wilaya iwe na Hospitali ya Rufaa kwa hiyo anayekwenda shule angeona soko la madaktari lipo nisome madaktari soko la ma-nurse lipo nisome u-nurse anayetaka kuuza vifaa vya medicine angeona naye soko lipo, tungewasaidia hata wawekezaji wetu wakawekeza kwa uzuri zaidi kwasababu wanaiona vision ya nchi, lakini sasa hivi tunakuwa hatuna vision tunakuwa na vitu vya kukimbiza.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka huu kwenye Halmashauri yangu kulikuwa na maeneo hakuna madawati wanafunzi wanafaulu tunakimbia kusema tunataka madawati na mwaka kesho tutakimbia tunataka madawati na mwaka kesho kutwa tunataka madawati, kwani hatuna statistics za kujua kwamba mwaka huu estimation za ufaulu zitakuwa kiasi hiki tukaanda madawati, tunakosa vision nikwambie jambo moja Mheshimiwa Waziri kwenye shida yetu tusipoweza ku-handle kuwa na vision kubwa ya Taifa letu maeneo mengi sana tuta-stuck kuna uwekezaji ambao mtu akiwekeza return yake inakuja baadaye sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano ukisema mtu awekeze kwenye kujenga Hospitali ukimaanisha kwamba kutoka kwenye hospitali utapata madaktari kwa hiyo wale wanaosoma wanajua wanakwenda kusoma nitakapofika form six nitachakua medicine kwasababu soko la madaktari lipo anayesoma anasema mimi ninasoma nursing kwasababu madaktari wanatakiwa kila Wilaya soko la nursing lipo.

Mheshimiwa Naibu Spika, wanaofanya biashara ya vifaa vya hospitali wataingiza vifaa wanajua ndani ya miaka 50 soko la vifaa vya hospitali lipo. Kwa hiyo hata wale wawekezaji kwenye industry ya elimu wanawekeza wakijua soko lipo. Lakini sasa hivi unasikia wote tumekimbia kwenye gesi baada ya miaka mitatu minne anakuja mwengine gesi haipo, tayari watu wameshajenga hotel wameshajenga nyumba wameshajenga hivi wanakula hasara baadaye kwenye korosho tunapiga kona tena hatuko korosho baadaye kwenye kwenye dhahabu tunapiga kona hapo kwenye dhahabu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninawaza nchi hii kama inatakiwa iendelee lazima iwe na vision ya nchi ya muda mrefu ili kiongozi anayeingia ndani ya utawala atumikie vision ambayo wananchi wameiweka sio vision yake. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana.

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana ninaunga mkono hoja. (Makofi)