Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Amour Khamis Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana niwapongeza sana viongozi wa Wizara hii Mama Mheshimiwa Prof. Ndalichako na mwenzake na hii ni Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia ambayo tunategemea sana kwamba mambo yake yangekwenda kwa Sayansi na Teknolojia na ninaamini wangeanza na walimu na kwasababu ni mwalimu naomba nianze na walimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Elimu ni Wizara muhimu sana katika nchi yeyote ndio tuliitegemea ilete mabadiliko yote ndani ya nchi kwasababu wao ndio wana deal na elimu na elimu ndio maendeleo. Lakini ninasikitika sana na walimu kwamba wamewekwa nyuma sana kwa hiyo ninaiomba hii Wizara na Serikali kwa ujumla waangalie walimu kwa jicho la huruma sana kwasababu mwalimu anafanya kazi nyingi sana akiwepo shule ana lea mwalimu, anafundisha, anatoa kazi, anazisimamia yote haya ingekuwa ni mtu mwingine mkubwa mkubwa basi yote haya angepangiwa allowances kwamba labda akisahihisha kuna allowance akitoa homework kuna allowance akitoa home text ana allowance lakini akitoa termina test ana allowance akitoa examination ana allowance. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwasababu ni walimu bado halijafikiriwa jambo hili naomba sana walimu wafikiriwe sana kazi wanayoifanya ni ngumu mno. Nafikiria hata kuwaombea hawa kwamba wangekuwa na wao wanapewa afya, yaani huduma za Afya bure ingependeza sana, na ninaiomba sana Wizara ya Elimu iwatumie sana Walimu. Ninakumbuka mwaka 2009 kuna mwalimu ndio amegundua mchanga fulani pale uliokuwa unapelekwa Kenya kwamba ule ndio mchanga ambao una dhahabu, Mheshimiwa Dkt. Magufuli Hayati Mwenyezi Mungu amrehemu akhera alipo huko amekuja kuuzuia baadaye.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ninaamini sana kama tungewatumia walimu vizuri basi hata wanafunzi wa darasa la sita leo wangeweza kutusaidia sana katika tafiti mbalimbali hata ulinzi wa yale madini kwa mfano madini yanayoibiwa kule basi walimu wangeandaa wanafunzi hata wakienda kucheza mchezo fulani tu pale wakawa wamevaa nguo tofauti za wanafunzi basi wakagundua kuna madini yanaibiwa na nani anaiba, Watoto wangesema, lakini kwasababu bado walimu hatujawatumia vizuri naomba sana Wizara ya Elimu iangalie jambo hili..

Mheshimiwa Naibu Spika, ni juzi tu hapa wiki iliyopita amekuja mama mmoja alinieleza kwamba anatoka Arusha yule mama alilalamika sana kwamba wamezuiwa yale mahitaji yao yaani increment zao zimezuiwa sijui kupandishwa madaraja yamezuiwa kwa muda wa miaka sita. Anashukuru sasa kwamba wanakwenda kupandishwa madaraja ila wao wamestaafu wamestaafu mwaka jana mwezi Novemba sasa anahofu kwamba yale madaraja wao hayatawahusu na ile arrear yao ya haya madaraja wanayotaka kupandishwa sijui itakuwaje. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini yote haya ni kwasababu tulimchukulia mwalimu ni mfanyakazi tu peke yake. Kwa hiyo, ilivyokuja kwamba wafanyakazi wote zimezuiwa increment na mwalimu tukamzuia, kumbe mwalimu ni zaidi ya mfanyakazi sisi wote humu tumekuja humu kwasababu walimu wametutengeneza leo tumekuwepo hapa kwasababu walimu wametengeneza future zetu lakini sisi tuliotengenezewa future hatuangali nani wametutengenezea future hizi. Kwa hiyo, naomba sana Wizara ya Elimu iwaangalie sana walimu sio vibaya walimu sasa kununuliwa hadi vile viatu vya kuingia shule sio tatizo hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninamuomba Waziri wa Elimu aangalie pia suala la masomo haya kila unapofungua kwenye mtandao mtu anapotaka kujiunga na chuo anaambiwa awe na mfano awe na credit nne lakini non- religious subject. Nilikuwa ninamuomba Waziri afikirie kwamba sisi pamoja na uhai wetu wote duniani hapa ipo siku tutaondoka duniani, na kwasababu tutaondoka duniani kila mtu anategemea kwamba kuwe na watu nyuma watakaosema mwanga wa bwana uwashiwe kule akhera sijui kuyasema vizuri haya maneno lakini sisi tunaomba dua ziombwe hawa watakaotuombe dua ni nani ikiwa leo mwanafunzi anaambiwa somo lako hili la dini halitazingatiwa katika udahili wa vyuo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli hili somo la dini halitamsaidia kule anakokwenda kwamba atasoma chemistry lakini halitamwongezea halita mchupisha amepata A ya chemisty amepata A ya biology amepata A ya physics lakini ameshindwa kupata B nyingine amekuja kupata D ya Bible knowledge na Islamic knowledge si itamsaidia kuingia advance, atakwenda kusomea chemistry lakini hapa imemsaidia lakini in-directly kwamba huyu mtoto umemfanya asome dini kwa hiyo kesho atakuwa padri kesho kutwa atakuwa shekhe atakuwa mwalimu wa Madrasa kwasababu ya elimu ile ile. (Makofi)

Mheshimiwa Niabu Spika, kwa hiyo sasa hivi mwanafunzi hasomi tena dini kwasababu anaona Serikali haizingatii hiyo credit yake. Kwa hiyo ninamuomba sana Waziri ninaiomba sana Serikali ifikirie jambo hili ni jambo kubwa na kwasababu sisi Watanzania wote kila mtu ana dini yake ninamuomba sana aangalie sana juu ya kurudisha ile hadhi ya somo la dini katika udahili wa vyuo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninamuomba pia Waziri afikirie namna ya kujenga uzalendo wa watanzania kwa kupitia Wizara hii ya Elimu leo watu wengi tumesoma lakini matatizo yameongezeka ukiangalia huku mara mtu anakwambia sijui nini kimeibiwa sijui hichi kimeibiwa tatizo nini, tatizo ni kwamba kila mtu hapendelei kwamba nchi ipate nini, anapendelea yeye mwenyewe apate nini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mtu atakuwa na madaraka miaka mitano, sita, kumi yeye akiwa na madaraka ndani ya siku tano ni tajiriā€¦ (Makofi)

NAIBU SPIKA: Kengele imeshagonga Mheshimiwa ahsante sana.

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK: Mheshimiwa Naibu Spika, Naunga mkono hoja ninashukuru sana. (Makofi)