Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nachukua nafasi hii nikushukuru sana kwa kunipa hii nafasi. Kipekee namshukuru sana Profesa pamoja na timu yake ya Wizara ya Elimu kwa kazi nzuri ambayo wanaifanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi leo naenda kujikita kwenye mfumo wa elimu. Nimefanya uchambuzi wa mfumo wa elimu na nimejikita kwenye zaidi ya nchi 15 ambazo nimefanya uchambuzi. Nimepitia mfumo wa elimu wa Tanzania, Japan, America, UK, Kenya, China na vile vile nimepitia mfumo wa elimu wa Zanzibar. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nina hoja takriban nne ambazo ningependa kuziwasilisha. Baada ya kupitia mifumo yote hii ya elimu, hoja ya kwanza niliyogundua inaleta utofauti kati ya elimu yetu na elimu nyingine duniani ni suala la muda wa kuanza Darasa la Kwanza na pili suala la umri wa kuanza darasa la kwanza. Vile vile ni aina ya elimu ambayo tunaitoa katika ngazi ya vyuo vikuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya pili ambayo nimeigundua baada ya kupitia mifumo mbalimbali ya elimu duniani ikiwepo ya Zanzibar na ya Tanzania, kuona ni stage gani ambayo elimu yetu inatakiwa iwe academic, lakini ni stage gani ambayo elimu yetu inatakiwa iwe technical na ni stage gani ambayo tunahitaji kuwa na mixture ya technical na academic? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya tatu ambayo nimepitia nikagundua ni suala la miundo ya mitaala. Katika miundo ya mitaala nimegundua vitu viwili; ya kwanza, ukipitia mitaala yetu kuna tatizo kubwa sana la masaa ya kukaa darasani na vile vile masaa ya kufanya practical, (field work).

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine nimeangalia mfumo wa assessment. Katika mfumo huu nilichojifunza, hususan mfumo wetu wa Tanzania, unawaandaa vijana kuwa na exam fear ambayo ni mbaya sana. Katika hili wasiwasi wangu uliopo ni kwamba tumeweka uzito mkubwa sana kwenye mitihani. Unakuta mitihani ya mwisho ina takriban asilimia 70 lakini yale mazoezi ambayo yanaenda kumjengea uwezo yana asilimia 30. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya mwisho ni hoja ambayo Waziri wa Elimu alisema kwamba wanakuja na mfumo wa ku-review sera yetu ya elimu ya Taifa, lakini vile vile kupitia mitaala yetu ya Elimu ya Taifa. Hoja yangu ni kwamba wakati Wizara inajipanga kwenda kufanya mapitio ya hii sera, nadhani ni muda muafaka sasa wa kujikita kikamilifu kuhakikisha kwamba tunakuwa na comprehensive review ya sera. Tuwe na muda wa kutosha katika ku-review and then tuje tujikite katika ku-review mitaala. Maana yake ni nini?

Mheshimiwa Naibu Spika, maana yangu ni kwamba tunahitaji kuwa na sera ambayo itakuja ku-inform hiyo curriculum ambayo tunaitaka, lakini tunahitaji kuwa na sera ambayo itakuwa customized kulingana na case studies mbalimbali tulizokutana nazo katika nchi mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu kwa Serikali baada ya kutoa hoja zangu hizo takriban tano, la kwanza, kama nilivyotangulia kusema, naomba nimshauri Waziri kuwa suala la mapitio ya Sera ya Elimu ni suala la msingi sana. Naomba tunavyopitia Sera ya Elimu ya Taifa, tufanye harmonization na wenzetu wa Zanzibar. Zanzibar elimu ya msingi wanaenda miaka sita, lakini tuna labour mobility ya kutoka Zanzibar kuja Bara, Bara kwenda Zanzibar. Ni muda muafaka sasa tufanye harmonization ya hii mifumo yetu ya elimu ili kuhakikisha kwamba tunapokuwa na wenzetu wa Zanzibar tunaongea lugha moja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Serikali ilifanyie kazi. Tunahitaji kuwa na mfumo mmoja wa elimu kwa sababu Bara na Zanzibar ni nchi moja, nasi hatuna restrictions zozote kwenye masuala ya elimu. Kwa hiyo, hilo naomba tulifanyie kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, ni suala la kuondoa ile tunaita exam fear. Katika kuondoa exam fear mimi nina hoja ifuatayo: Nimefanya kazi vyuo vikuu. Nimefundisha Chuo Kikuu cha Dodoma muda mrefu na pia nimefundisha Chuo cha Mipango muda mrefu. Kitu nilichojifunza na nimekisema, nadhani kuna tatizo kwenye curriculum zetu. Tumeweka weight kubwa sana kwenye mitihani ya mwisho ambayo inatengeneza exam fear. Mwanafunzi anahangaika ili aweze kupata A na B, badala ahangaike kupata competency. Nataka kushauri kwamba katika hili naomba sasa unapopitia mitaala na sera, punguza weight ya mitihani, peleka weight kwenye practicals, vijana tuwa-expose kwenye mazingira ya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la nne, naishauri Serikali tuanzishe kitu kinaitwa integrated education system. Tuje na combination ya academic na technical. Wabunge wengi wameelezea. Mheshimiwa Waziri wewe unafahamu, tumesoma huko nyuma kwenye shule ambapo tulikuwa tunafundishwa sayansikimu, elimu ya kilimo na vitu vingine, lakini ile elimu ilikufa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunapotaka kuandaa vijana waweze kujitegemea, ni muda muafaka sasa kuhakikisha kwamba tuna-impart hizi competences kuanzia huko chini shule ya msingi, sekondari na ile inawajengea palatability ya kupenda, kwamba baadaye niende nikasomee mambo ya kilimo, baadaye nikasomee ufundi na kadhalika. Huwezi kujenga palatability ya mtu akiwa level ya juu, unataka aende akasomee ufundi VETA. Tunahitaji ku-instill kuanzia chini shule za msingi na sekondari ili wale vijana anapotoka pale anasema mimi nataka niwe fundi wa bomba.

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Kuna taarifa, sijajua inatoka wapi? Mheshimiwa Mwita Getere.

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, hapa. Nilitaka nimpe msemaji hapa…

NAIBU SPIKA: Ngoja ngoja. Kulikuwa na taarifa kutoka pale, ndiye niliyemwita. Kwa hiyo, wewe subiri kidogo.

Mheshimiwa Mwita Getere.

T A A R I F A

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nataka kumpa taarifa Mheshimiwa anayeongea kwamba rushwa siyo lazima iwe kwenye pesa peke yake. Corruption of mind ni jambo kubwa sana katika nchi za Kiafrika na hasa Tanzania. Kuna haja gani ya kutomwekea mtoto maarifa ya kufundishwa namna ya kufuga kuku, namna ya kufuga ng’ombe, namna ya kulima, ukamshindilia ma-pai, ma-triangle na mambo mengi ambayo watoto wengi wanaotoka primary siyo kwamba wote wanaenda sekondari, wengi wanabaki vijijini. Wanaobaki vijijini wanabaki na nini?

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mwita Getere, tafadhali naomba ukae kidogo. (Kicheko)

Waheshimiwa Wabunge, taarifa tunazozitoa inabidi ziendane na Kanuni zetu. Mbunge anayeruhusiwa kusema kuhusu taarifa ni pale ambapo Mbunge mwenzake halafu kuna jambo anataka kumpa taarifa iliyo sahihi. Pengine kile anachokisema kimekaa namna fulani hivi. Sasa nimeona Wabunge wanasimama kusema taarifa, wakati anataka kuchangia yeye wazo lake. Sasa hiyo ni kinyume na kanuni zetu, ndiyo maana huwa kuna nafasi ya kuchangia. Usiwe na wazo lako unataka kumpa mwenzako ili na yeye alifanye wazo lake, hapana. Unampa taarifa kwenye kile kile anachokizungumza.

Mheshimiwa Dkt. Pius Chaya, taarifa kutoka kwa Mheshimiwa…

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Hamna Taarifa juu ya taarifa. Kwa hiyo, uwe unasubiri kidogo, tutaenda vizuri tu, hamna shida.

Mheshimiwa Dkt. Chaya unapokea taarifa ya Mheshimiwa Getere?

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Napokea Taarifa ya Mheshimiwa Mbunge na nadhani alikuwa anaunga mkono hoja na mawazo ambayo nilikuwa nayatoa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine ambacho ningependa kuishauri Serikali ni upande wa vyuo vikuu.

NAIBU SPIKA: Kuna taarifa nyingine. Sasa kwa utaratibu kwa sababu tunajifunza, akishazungumza mmoja akitoa taarifa, lazima mzungumzaji azungumze ndiyo mwingine anaomba tena taarifa. Kwa hiyo, kwa sasa kwa sababu hilo tulikuwa hatujalielewa vizuri, nitakupa nafasi Mheshimiwa Saashisha, lakini kwa kawaida ukikaa chini namna hiyo, akishasimama kuzungumza akaongea, unaomba upya taarifa.

Mheshimiwa Saashisha.

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ahsante pia kwa mwongozo mzuri. Nataka kumpa msemaji taarifa kwamba hapo awali kabla ya mwaka 1919 Wizara ya Elimu ilikuwa na mfumo rasmi kabisa wa shule za msingi za ufundi na kwetu kule Hai tulikuwa na shule tano zenye muundo huo. Yaani watoto wakiwa shule ya msingi walikuwa wanafundishwa pia masomo ya ufundi na kulikuwa na walimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, mpaka ninavyozungumza sasa hivi, shule ya msingi ya ufundi Mshara kuna walimu ambao waliandaliwa kwa ajili ya mitaala hii kufundisha rasmi masomo ya ufundi. Tatizo ni kwamba shule hizi zimeachwa hazijaendelezwa. Kwa hiyo, nampa taarifa kwamba kulikuwa na mfumo huu, ila umelala. (Kicheko/Makofi)

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, nawakumbusha kwenye vishkwambi vyenu zimo Kanuni mle. Tuzipitie vizuri. Huko tunakoelekea kwenye hili Bunge ni mwisho mwisho wa kujifunza Kanuni. Baadaye itakuwa ni mtu kaa chini, sogea kidogo, futa ulichosema. Sasa hivi tunaenda taratibu.

Mheshimiwa Dkt. Chaya malizia mchango wako.

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakubali vile vile taarifa ya Mheshimiwa Mbunge na bado naendelea kuishauri Serikali kwamba tunahitaji kuhuisha mitaala yetu hususan katika ngazi ya shule za msingi na sekondari.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho upande wa vyuo vikuu. Kwa uzoefu wangu ambao nimekaa kwenye vyuo vikuu, unakuta kwa mfano wale wanaosoma certificate, diploma, na degree tuna wa-subject kwenye kufanya research. Mwanafunzi gani wa certificate anaweza kufanya research ikatumika katika maisha yetu? Mwanafunzi gani katika level ya diploma anaweza akafanya research ikatumika katika maisha yetu?

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kushauri, Wizara ya Elimu, mje na mfumo unaoitwa capstone project system; huu mfumo unaweza ukatumika kwa ngazi za chini ambao unawajengea uwezo wale watu, tunawa-expose kwenye mazingira ya kazi, wanakuja na ubunifu, innovations. Unaweza ukamchukua mtu ukampeleka kwa mfano TANESCO, anaenda kubuni mradi fulani na ile inakuwa na weight kubwa kama nilivyotangulia kusema huko. Badala ya kuweka weight kubwa kwenye mitihani tunatengeneza fear of exams. Tupeleke weight kubwa kwenye hizi capstone projects ambazo zitasaidia kuwajengea competences na skills. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema haya, namwomba Waziri, katika Jimbo langu la Manyoni Mashariki sina Chuo cha VETA na nina vijana wengi sana waliomaliza sekondari wanahitaji kuwa na Chuo cha VETA.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema haya, naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)