Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii niweze kutoa mchango wangu kwenye Wizara hii ya Elimu ambayo ni muhimu sana. Awali ya yote namshukuru na kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Elimu kwa namna ambavyo amewasilisha bajeti yake hapa ili sasa sisi Wabunge tuweze kutoa mchango wetu na maoni yetu.

Mheshimiwa Spika, nitajikita zaidi kwenye Bodi ya Mikopo. Nachukua fursa hii kuipongeza sana Serikali kwa namna ambavyo iliona ni muhimu kuhakikisha mtoto yeyote wa Kitanzania ambaye atakuwa hana uwezo wa kulipia elimu ya juu, basi Serikali ikatengeneza mkakati maalum wa kutengeneza funds ambapo tulipata chombo cha Bodi ya Mikopo ili kuratibu hili zoezi la utoaji mikopo kwa vijana wetu wa Kitanzania. Hili lilikuwa ni jambo jema na lengo lilikuwa na nia njema, lakini namna ya utoaji wa hii mikopo ndipo kwenye changamoto. Hapa ndipo tulipo-create crisis. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mikopo hii namna ambavyo inatolewa haikuzingatia nini kama Taifa tunahitaji hasa kwa sasa hivi? Pia haijafanya utafiti. Mheshimiwa Mpina hapa amesema asubuhi, hivi wenzetu wa Wizara ya Elimu mnafanya utafiti kuona sokoni ni nini kinahitajika? Mheshimiwa Waziri wa Elimu, asubuhi umekuja hapa umetueleza kuwa tumeongeza sasa Bodi ya Mikopo kutoka 4.6 billion sasa hivi zitakwenda kwenye five billion. Ni jambo jema, lakini zinakwenda kufanya nini? Zinakwenda kusaidia vijana wa aina gani? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wenzetu wa Bodi ya Mikopo walikuja kutupa mtiririko wa namna ya hizi fedha zimetumika so far. Kwenye kada ya sayansi ya jamii na sanaa, maana yake Bachelor of Art, 64.9 percent; Uhandisi 5.3 percent; Afya 4.7%; Sayansi ya kilimo, inaendelea kushuka 1.8, Uhandisi wa Mafuta na Gesi ndiyo kabisa, 0.10 na mengineyo.

Mheshimiwa Spika, hapa ndipo tulipo-create crisis. Kama mikopo hii yote; 64 percent ya hii mikopo inakwenda ku-fund vijana ambao wana degree ambazo ziko mitaani, sasa hivi soko liko saturated. Nikawa najiuliza, hivi Wizara ya Elimu hatujaliona hili? Sasa hivi na hizo five billion tunaenda bado ku-create hawa vijana wa Bachelor of Arts ambao bado tunaenda ku-create degrees ambazo hazihitajiki kwenye soko la elimu? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimezidi kujiuliza, what’s wrong na vyuo vyetu vya kati? Vyuo vya ufundi, ndio doers, hawa ndio wanaoingia kule field. Tulishauri hapa Mheshimiwa Waziri, nchi za wenzetu ambazo zinaendelea sasa hivi China inakua kwa asilimia 10, lakini bado wameona umuhimu wa kuhakikisha wanarudi kwenye vyuo vya kati. Kwa sababu mmesema kigezo kikubwa ni mtoto kutokuwa na uwezo wa kujilipia.

Je, hivi vyuo vya kati hakuna watoto wa masikini wanaohitaji hii mikopo? Hawa ndio doers Mheshimiwa Waziri. Ukienda Kituo cha Afya, tuna daktari mmoja, lakini wale wasaidizi karibia watu 30 wote ni wa elimu ya kati. Who is funding these people? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, engineer pale anatengeneza daraja, tunahitaji ma-engineer wangapi? Ni engineer mmoja na watu wenye ujuzi wa kati. Who is funding these people? Nina uhakika tungekwenda huko, I am not arguing what, tupunguze kiasi. Kama tutapeleka at least three billion, at least hizi two billion zije huku ziwasaidie watoto wa uchumi wa kati kuendeleza uchumi wa kati. Moja, hawa watoto wataweza kulipa hii mikopo kwa sababu, hizo taaluma zao ndizo zinahitajika huku. Pili, wataweza hata kuongeza pato la Taifa kwa sababu, wataweza kulipia mikopo na kujikimu na shughuli zao za kilasiku na kutunza familia zao. Kwa hiyo, focus yetu… (Makofi)

SPIKA: Waheshimiwa ambao mlikuwa mnachangia hapa, mnaona Mbunge mzoefu anavyokwenda? Yeye amechagua Bodi ya Mikopo na anavyoiona Bodi ya Mikopo na analysis yake. Dakika saba siyo nyingi, huwezi kuongea vitu vitano. Endelea Mheshimiwa Rose. (Makofi)

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Bado narudi kwenye umuhimu wa hivi vyuo vya kati. Tulikuwa na CBE, Mipango, Chuo cha Tengeru; sasa hivi kaka yangu amesema hata Chuo cha Mwanza, kile cha Uvuvi, sasa hivi watu wote wanakwenda kwenye degree. Why are we expect na hivi vyeti wakati tunahitaji hivi vyuo vya kati?

Mheshimiwa Spika, namwomba Mheshimiwa Waziri, hii Bodi ya Mikopo ije na sura na mikakati ambayo Watanzania tunaitaka. We can not be doing the same thing over and over and expect different results. Kama hawa watoto wa art ndio wamejaa kule na mwakani tena Bachelor of Art zimejaa mtaani, manung’uniko lazima yataendelea na tuna-create bomu ambalo kuja kulizima itakuwa ni kazi sana Mheshimwa Waziri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri, ushauri wangu kwa Serikali utakuwa kama ifuatavyo: Moja, kama tume-create special window kwa ajili ya kilimo, why not education? Sasa hivi tutakapokuja hapa iwe ni Bodi ya Mikopo not Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu. Tuzi-involve na sekta nyingine kama banks ili nao waje wawe na michango katika kuendeleza elimu yetu nchini.

Mheshimiwa Spika, la mwisho,…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Natamani nikuongeze muda, lakini…

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Spika, hili ni la mwisho.

NAIBU SPIKA: Bahati mbaya.

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Spika, kwa kumalizia, tulikuwa na new formula ya capitation kwenye kutoa ruzuku shuleni. Mheshimiwa Dada Grace amesema pale asubuhi, hali ni mbaya, tulishajulishwa ianze kutumika, imekwama wapi Mheshimiwa Waziri? Ni kwenu Wizarani au Wizara ya Fedha? Hii ndiyo ilikuwa more practical inajibu zile shule ambazo ziko mbali na shule ambazo zina uhitaji maalum ili waweze kupata pesa zaidi.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, nashukuru sana kwa kunipa nafasi. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Rose Tweve. Anastahili makofi makubwa zaidi ya hayo. (Makofi)

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)