Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa fursa hii ya kuchangia kwenye mjadala huu ambao ni muhimu sana kwasababu ya jukumu la Wizara hii katika kuendeleza nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Profesa Ndalichako, na Naibu wake pamoja na uongozi mzima wa Wizara kwa kazi nzuri kwenye mazingira ambayo ni magumu na kwenye changamoto nyingi.

Mheshimiwa Spika, kwasababu uchumi wowote unapobadilika haraka sana sekta ya elimu inatakiwa na yenyewe iweze kujibadilisha na kuwa bunifu ili iweze kutengeneza wahitimu ambao wanakidhi mahitaji ya wakati huo. Sasa tukiangalia na tukijaribu kufikiria kwamba tuko wapi na tunakwenda wapi katika dunia hii, utajikuta kwamba sekta hii inatakiwa ibadilike sana kwa namna ambavyo tunakwenda mbele.

Mheshimiwa Spika, sekta ya viwanda ilivyobadilika, industrial revolution ilivyoingia, tija kwenye kilimo iliongezeka sana na hivyo bei za vyakula zikashuka kwa hiyo faida kwenye kilimo ikashuka pia. Kwa hiyo, watu wakaamua kukimbilia mijini wakapata kazi kwasababu viwanda vile vilikuwa vinazalisha ajira.

Mheshimiwa Spika, lakini sasa hivi viwanda havizalishi ajira. Bahati mbaya ukienda kiwanda chochote kikubwa utakuta kwamba robots wame-automate na artificial intelligence utakuta kwamba pengine ma-robot yanafanya kazi. Hata kule kwenye mabenki yetu sasa hivi unakuta kwamba watu hawaajiri, walikuwa wanaajiri watu 400 sasa hivi hawaajiri kwasababu tunatumia sim banking na vitu kama hivyo ambavyo vina-replace employment ya watu.

Mheshimiwa Spika, sasa tunapokwenda hii karne siyo ya viwanda ambavyo ni labor intensive, ni kadri sasa ya TEHAMA na hii TEHAMA inatupeleka mbali sana tukijifikiria vizuri. Tukijifikiria vizuri tutafanya mambo mengine na ni kweli kwamba vyuo hivi ambavyo tumekuwa tunazungumza toka asubuhi kwamba tuviboreshe, tufanye hiki na kile, tukichunguza vyuo hivi vya ufundi vya kuwasaidia vijana wetu wapate maarifa na ujuzi waweze kutenda kazi na waweze kujiajiri.

Mheshimiwa Spika, pengine kwanza havifai kwenye karne hii, havina karakana na vifaa vya kufundishia vitu ambavyo vinahitajika kwenye uchumi wa kisasa, kwenye uchumi huu ambao sasa hivi ndiyo tunakwenda. Na mtu akisema kwamba hatujui tunakokwenda ni mtu ambaye haoni kwasababu ukweli ni kwamba tunakokwenda ni tofauti. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sekta zinazozalisha ajira ni sekta za huduma; mawasiliano, kwa sekta kama za usafiri, uchukuzi, afya itazalisha utalii, itazalisha utawala, sales and marketing, lakini ukiangalia upande huu wa viwanda hawatazalisha kwasababu automation imefika mbali sana na tija imekwenda mbali sana.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka niseme kwamba tunapoangalia hivi vyuo kuvipa uwezo lazima na walimu wale wapite kwenye mafunzo tofauti na waweze ku-identify ni kitu gani ambacho watafundisha ili tuweze kuwasaidia watu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niseme kitu ambacho nakiona ni kwamba vyuo vilivyo kila kata kuna vyuo. Sasa vyuo hivi usipofanya vikawa-specialized hutaweza kuvi-equip na vile vitu ambavyo vinahitajika; hutaweza. Kwa hiyo, lazima viwe specialized na vitangazwe kwa wananchi wajue kwamba nikienda Bukoba ntapata chuo ambacho kinatengeneza watu wanaojifunza kutengeneza simu, au nikienda Lindi kule ntapata watu ambao wanaweza wakatengeneza au kuhudumia mashine za oil and gas, and so forth. Kwa hiyo, ni lazima tuvifanye viwe specialized kidogo angalau kuwe na specialization kidogo ili tujue ni vipi na viko wapi.

Mheshimiwa Spika, lakini nikihesabu kule kwangu kuna Vyuo viwili; Mshiri na kingine kiko kule Mwika, hakina hata walimu, hata hao ambao tunasema kwamba ni wa kale ambao sidhani kama wanaweza waka-cope na skills zinazohitajika, bado hawapo hata hao walimu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka niombe kwamba pengine, kwanza hiyo kanzidata ya walimu wa vyuo hivi vya ufundi na stadi mbalimbali ijulikane ili waweze kuwa allocated properly. Hayo majengo ambayo yamekaa idle hayaendeshi kozi zozote kwasababu ya kukosa walimu yaweze kutumika lakini cha msingi ni kwamba wapate training, wapelekwe hata nje.

Mheshimiwa Spika, hata tukikaribisha Wachina na Wahindi wakaja wakatuonesha wao wanafanyaje na wanakwendaje kwasababu nchi nyingi sasa zinajikita kwenye upande wa training ya mambo haya ya hudua na kutengeneza vitu vya kisasa, siyo kutengeneza magari ya, hata magari manual siku hizi hakuna kabisa.

Mheshimiwa Spika, sasa niseme hivi; kwasababu watu wa ku-train ni wengi sana hebu tufikirie wazo moja. Kwa mfano tunasema mambo ya soft skills hizi za watu kuwa na tabia ya kuweza kujituma, kuweza kuheshimu kazi na kadhalika, zinapatikana zaidi kule JKT.

Mheshimiwa Spika, ukienda JKU sasa hivi ukaweza kupiga mark time pale vizuri halafu jioni ukafundishwa skills zozote hizi ambazo tutakuwa tumesema Ruvu wafundishe hiki na hiki, ukifundishwa hivyo ukimaliza pale baada ya miezi mitatu au sita unakwenda unaajiriwa na utakuwa na heshima na utakuwa mwaminifu na utafanya kazi vizuri kwasababu umejifunza discipline na skills kwa namna ambayo itasaidia sana watu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi nafikiri hiyo ndiyo njia ambayo inaweza ikafanya kwa haraka sana watu ambao wanamaliza form six, hata wanaomaliza university wanaambiwa piteni kule mtapata skills kwa ujumla kwa haraka zaidi na kule kuna vifaa vya kufanyia majaribio na kadhalika. Kwa hiyo, hicho ni kitu ambacho mimi nafikiri kingekuwa cha msingi.

Mheshimiwa Spika, lakini pia niseme kwamba tukizingatia kwamba kuna haja ya kuwa wabunifu kwenye hii nyanja ya TEHAMA, kuna haja ya vyuo vyetu hivi vikuu sasa hivi viwe na vitengo. Kila chuo at least kiwe na kitengo cha incubation ambapo mtu akiwa na wazo lake anakwenda kwenye kitivo au kitengo kile cha chuo kikuu, wanamsaidia kuboresha na kumuonesha namna gani anaweza aka-implement.

Mheshimiwa Spika, wanaweza wakamuonesha pia kwamba pengine mashine za namna hii zinapatikana TEMDO, zinapatikana wapi, hebu tukusaidie, wanamsaidia kina-take off wanamuachia anaendelea na watu wataajiriwa wengi.

Mheshimiwa Spika, lakini kwa namna hii ambayo tunaona naona kuna shida sana; ijasiriamali haufundishwi darasani, unafundishwa kwenye field. Mtu kama umemaliza kama usipopata on job training hutaweza. Sasa hivi vyuo vina watu, walimu wako wengi ambao wana-retire, maprofesa wana-retire, wajasiriamali wengi nao wana-retire.

Mheshimiwa Spika, kwa nini tusiwapeleke tukawaombe waanzishe hivi vitengo ili watu waweze kupata skills zao wakajifunza. Kuna mmoja alisema kwa nini akina Dewji hawaandiki vitabu. Watu wamejifunza kutoka kwa akina Dewji waka-implement mambo ambayo yataleta tija katika nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, nafikiri kwamba kule kwenye jimbo letu, na nitafurahi sana kama kweli tutaweza kupata specialization ya mambo ya…

SPIKA: Mheshimiwa Dkt. Kimei, muda hauko upande wako.

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

SPIKA: Nakushukuru sana, ahsante sana.

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana, naunga mkono hoja kwa asilimia 100; ahsante. (Makofi)