Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Joseph Anania Tadayo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. JOSEPH A. TADAYO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kupata nafasi hii ya mwisho kuchangia. Mchango wangu ni mfupi sana.

Mheshimiwa Spika, awali ya yote niungane na wote ambao wamepongeza kazi nzuri iliyofanywa na Wizara hii pamoja na changamoto nyingi ambazo tunazifahamu zinazoikabili Wizara hii lakini kwa kweli kazi ni nzuri na hata ukisoma takwimu crime rate yetu sio mbaya kama nchi zingine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili niungane pia na wote waliozungumza juu ya suala la hali mbaya ya miundombinu ya vitendeakazi na majengo ya polisi hata Jimboni kwangu Mwanga tuna tatizo hilo kiasi ambacho askari wetu wakati mwingine, nilipita siku moja pale kituoni nikakuta wanachangishana kupiga rangi kwenye jengo la polisi jambo ambalo lina moyo mzuri kwa kweli nawapongeza lakini tunahitaji kuwasaidia kwasabbau kimsingi sio kazi yao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lingine nishauri sasa kuhusu masuala yote yanayohusiana na ujenzi katika majeshi yetu. Kwa bahati ni kwamba Wizara hii ina nafasi ya kuwa na nguvukazi yenye ujuzi mbalimbali ambao ni wenzetu wale wafungwa. Iko teknolojia ya matofali haya ya hydra form ambayo National Housing wanafanya vizuri sana.

Mheshimiwa Spika, nina hakika kabisa tukiipeleka hii teknolojia kwenye maeneo ya megereza yetu na kwa ujumla kwenye majeshi mbalimbali ambayo iko chini ya Wizara hii wana uwezo wa kutengeneza matofali na tukamaliza kabisa tatizo la ujenzi wa nyumba za askari pamoja na maeneo mbalimbali ya maofisi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lingine ambalo pengine hata sisi tunaweza tukashirikiana ni kwamba hata tunapozungumzia hizi fedha za CSR kwenye wawekezaji mbalimbali ni vizuri pia tukakumbuka vituop vyetu vya polisi kwenye mambo ya furniture n.k. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lingine ambalo nilipenda kuzungumzia ni juu ya suala la majanga ya moto. Mwishoni mwa mwaka jana Jimbo langu lilipata tatizo la kuunguliwa na shule inaitwa Nyerere Sekondari, moto ambao ulitokea karibu mara tatu mfululizo ukaunguza mabweni mawili kwa kiasi kikubwa sana. Vyombo vyetu vya ulinzi na usalama viliitikia kwa haraka sana, navipongeza. Lakini nadhani tunahitaki kwenda mbele kidogo kwenye tatizo hili iwe ni sehemu ya kuwaelimisha wanafunzi wetu shuleni na kuwapatia vifaa vya kuzimia moto. Endapo wale wanafuzni wangekuwa na elimu ya kutosha ya kupambana na moto halafu wakawa na vifaa vya kisasa, nina hakika majanga haya yangeweza yakadhibitiwa kwa kiasi kikubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama tuliweza kukimbia mchaka mchaka kila asubuhi tukiwa wanafuzni sidhani kama leo tukiamua kwamba kila Jumamosi tuna zoezi la kudhibiti moto, la kuzima moto kwa wanafunzi wetu sidhani kama itashindikana. Naamini itawezekana na tutaweza kuzuia haya majanga kwa sababu hata tungekuwa na magari mengi bado janga linapotokea ni vizuri wasije kuzima moto ila moto udhibitiwe, usitokee au usiendelee pale ambapo umeanza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mchango wangu ni mfupi tu. Naomba kuunga mkono hoja ya Wizara hii. Ahsante sana. (Makofi)