Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Assa Nelson Makanika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. ASSA N. MAKANIKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi kuweza kuchangia Wizara hii muhimu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii kuchangia sehemu moja katika Wizara hii ya Mambo ya Ndani, suala la uraia. Wizara hii ni Wizara muhimu sana katika ujenzi wa uchumi wa nchi yetu, na ni Wizara ambayo hakika ikilegalega kidogo tu inaweza ikatikisa misingi ya uchumi wa nchi.

Mheshimiwa Spika, Wizara hii ina-deal na mambo ya home affairs. Na ukiweza kuangalia raia yeyote yule katika nchi yoyote ili, ili aweze kujenga uchumi wa nchi hiyo, lazima aji-feel proud ya nchi husika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwezi Januari, tarehe 26, vyombo vya ulinzi na usalama viliendesha operesheni moja pale maeneo ya Mabwepande. Katika operesheni ile kweli inawezekana kukawa kuna moja wapo ya watu ambao ni wahalifu na watu ambao siyo raia wa nchi yetu ambao wanaweza kuwa waliingia katika nchi yetu kimakosa.

Mheshimiwa Spika, lakini katika operesheni ile namna ilivyoendeshwa, hususan kwa watu wetu wa Kigoma, kwa kweli haikuwa inatuonesha pride kusikia kama na sisi ni sehemu ya nchi hii. Kulikuwa kuna maswali mengi ambayo yalikuwa yakiulizwa, nikiwa mmoja wapo wa mashuhuda. Wananchi wa Mkoa wa Kigoma kutoka sehemu mbalimbali walinipigia simu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilifika pale Dar es Salaam, Oysterbay, nilivyofika pale moja wapo ya maswali yaliyokuwa yakiulizwa yalikuwa yanatwezwa na kuonesha kwamba watu fulani wana haki kamili ya kuwa raia wa nchi hii na wengine ni Daraja B. Jambo ambalo siyo jema katika kujenga uchumi wa nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo niombe sana – Mheshimiwa Waziri nilikupigia simu na tukazungumza sana, asilimia 80 ya watu waliokamatwa katika operesheni ile walikuwa ni watu wa Kigoma, na sana maswali waliyokuwa wakiulizwa wanatwezwa utu wao, maana utaambiwa sema namba nne, sema namba tano, kana kwamba ni vitu ambavyo mtu anaji-feel inferior sana.

Mheshimiwa Spika, niiombe Serikali yangu, niiombe Serikali Sikivu iweze kuangalia historia ya ujirani mwema na nchi hizi husika haiwezi ikaondoa uraia wa watu wa Kigoma. Sisi tumekuwa ni majirani na nchi hizo. Ni vyema zaidi Serikali iangalie approach nyingine ya kuweza kutu-treat sisi watu wa Kigoma ili tuji-feel tuna hatimiliki ya nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niombe kitu kimoja, kwa kupitisha tu kidogo katika historia ambayo tunayo na muunganiko wa nchi jirani; sisi tuna historia ambayo inatusema kana kwamba tumekuwa hata katika historia ya kiuongozi. Ukiangalia mwaka 1888 Mjerumani amekuja kutawala hapa kwetu, sisi Kigoma ilikuwa ndiyo makao makuu yake akitawala Rwanda na Burundi, lakini makao makuu ikiwa ni Kigoma. Sasa ukisema historia ituhukumu sisi mtakuwa mnatuonea. Hayo ni masuala ya Mwenyezi Mungu, niombe na sisi tuweze kumiliki haki sawa katika nchi hii.

Mheshimiwa Spika, kwa mfano, tuna historia ambayo haiwezi kufutika, mfano vijiji vyetu vingi vinafanana. Ukiangalia pale kwetu Kigoma tuna Kijiji kinaitwa Kalinzi, lakini ukienda hata Ngara kuna Kijiji kinaitwa Inkarinzi; ukienda hata Burundi, kuna Kijiji pia kinaitwa Karinzi. Hiyo naonesha ni namna gani historia yetu inavyofanana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hata hapohapo kwetu Kigoma, mojawapo tuna Vijiji vinaitwa Mnanira, hata ukienda Burundi pia kipo Kijiji cha Mnanira; ukienda Rwanda kipo Kijiji cha Mnanira. Sasa historia hii isije ikawa ni mhukumu kwetu. Hivyo, nimuombe Mheshimiwa Waziri aweze kuangalia hii Idara ya Uhamiaji iweze kuangalia namna ya kutu-treat sisi watu wa Kigoma ili na sisi tuji-feel kwamba ni sehemu ya nchi hii.

Mheshimiwa Spika, nitoe ushauri mdogo sana; ukija ukaangalia suala hili la uraia linaua sana na kudororesha hali ya uchumi katika Mkoa wetu wa Kigoma. Nilikuwa nikiongea na Rafiki yangu mmoja, yeye ni mtu wa Ubelgiji, na nimesoma naye, lakini akawa anashangaa sana, anasema Ubelgiji imejengwa na mali inayotoka katika nchi Jirani ya watu wa Kigoma, Nchi ya Kongo, lakini sisi hiyo mali inapita katika anga la watu wa Kigoma, lakini kulingana na changamoto ya uraia katika Mkoa wetu wa Kigoma…

SPIKA: Mheshimiwa Makanika, kengele imeshalia.

MHE. ASSA N. MAKANIKA: Mheshimiwa Spika, naomba kuunga mkono hoja, lakini niseme tu ya kwamba Serikali iangalie suala hilo kwa umakini, nitaweka mchango wangu kwa njia ya maandishi kumalizia hili. Ahsante.