Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Ravia Idarus Faina

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Makunduchi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. RAVIA IDARUS FAINA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kupata nafasi hii. Kwanza nataka kupata ufafanuzi juu ya Serikali kwa nini haijajenga Ofisi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Zanzibar na hii inapelekea kwamba Waziri na Naibu Waziri wanapofika Zanzibar wanapata tabu sana, wapi watafikia. Kwa hiyo naiomba Serikali ilete ufafanuzi juu ya suala hili.

Mheshimiwa Spika, kwa vile muda ni mchache…

SPIKA: Hebu fafanua hilo likoje.

MHE. RAVIA IDARUS FAINA: Mheshimiwa Spika, hadi hii leo Zanzibar hakuna Ofisi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Kwa hiyo ni lini Serikali itajenga hiyo Ofisi hili Waziri na Naibu Waziri wanapokuja Zanzibar wawe na sehemu maalum ambayo wanafikia.

Mheshimiwa Spika, la pili, naomba Serikali itupatie Ofisi ya NIDA pamoja na Ofisi ya Uhamiaji Wilaya ya Kusini Unguja ambayo tunakosa huduma hiyo, ukizingatia wananchi wa Wilaya ya Kusini wanakosa huduma nzuri ambayo wanaihitaji kwa sasa hivi.

Mheshimiwa Spika, naomba nichangie kuhusu Jeshi la Polisi; hapa nisipopata ufafanuzi mzuri natarajia kushika shilingi.

Kwanza naomba nipate ufafanuzi, ni kwa nini askari polisi anasoma na ahahitimu degree yake ya kwanza na anapomaliza degree yake anapelekwa kozi ya sergent na anapata cheo cha sergent. Je, huyu ambaye kasoma diploma na form six yeye atapewa cheo gani? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Jeshi la Polisi limeweka utaratibu mzuri tu wa PGO, lakini PGO inatumika katika baadhi ya maeneo, baadhi ya maeneo haifanyi kazi. Inakuwaje Askari Polisi anakaa miaka 15 hajapata rank. Jeshi la Polisi linawapeleka askari, rank pamoja na faini, lakini cha kushangaza mpaka kufikia mwaka 2013 hawana stahiki zao ambazo wanazipata.

Mheshimiwa Spika, vilevile Askari Polisi wanapewa jukumu la kuwachukua watuhumiwa kutoka mkoa mmoja kwenda mkoa mwingine lakini hakuna stahiki zao ambazo wanapata, wanaishia kujaza fomu na hizo fomu zinabakia kwenye mafaili hadi leo hawapati stahiki zao. Hii inaleta usumbufu kwamba huyo ambaye anaenda kumchukua mtuhumiwa ni yeye mwenyewe amuhudumie mtuhumiwa, sijui pesa anaitoa wapi.

Mheshimiwa Spika, mwisho, napenda kumalizia kwa suala ambalo alichangia Mbunge mwenzangu kwamba, Askari Polisi wanahitaji kupatiwa vitendea kazi, haipendezi kuona documents muhimu za Jeshi la Polisi zinapelekwa kwenye vibanda vya kawaida tu kutolewa photocopy ili ifanyike hiyo kazi, hiyo haipendezi kwa kweli. Photocopy machine thamani yake sio kubwa kwamba askari apate tabu kwenda kutoa yeye hiyo photocopy.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)