Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Madini

Hon. Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Madini

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa dakika hizi tano ningependa kuongelea mambo makubwa mawili. Jambo la kwanza ni ushiriki wa Watanzania kwenye ajira zinazohusiana na migodi na madini na jambo la pili, ukiacha ajira ni ushiriki wako katika manunuzi na uuzaji wa bidhaa kwenye migodi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunao Watanzania wengi, tasnia ya madini imeanza kushamiri kuanzia miaka ya mwaka 1999/ 2000 wako Watanzania wengi wamehudumu kwenye sekta ya madini lakini hawatambuliki au hawajulikani wapo wapi. Ni mmoja wa wadau ambao tumefanya kazi kwenye sekta ya madini, nilikuwa naiomba sana Serikali itengeneze Kanzidata inayoeleweka itawatambua watumishi waliofanyakazi kwenye Sekta ya Madini. Na hii itasaidia kupunguza idadi ya watu wanaojiita ma-expert au wazungu ambao wanakuja kufanya kazi ambazo Watanzania wanaweza kufanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo hii tumeshudia Watanzania wachache wanapata nafasi za juu Serikalini I mean sio Serikalini. Wanapata nafasi za juu kwenye migodi kwasababu Watanzania wale wamehudumu kwa muda mrefu. Tofauti na maeneo mengine ukihudumu kwa muda mrefu kwenye sekta za madini uwezo wako unakuwa ni mkubwa kiasi kwamba una uwezo wa kufanyakazi ndani ya Tanzania, ndani ya Afrika hata Duniani kwa ujumla. Kwasababu eneo hili utaalam wake hauna tofauti kwenye maeneo mengine ambayo kuna migodi mikubwa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimuombe sana waziri na hili ni tatizo la muda mrefu tumekuwa tunalipigia kelele kwa zaidi ya miaka sita, miaka sana, miaka nane hakuna Kanzidata ya pamoja inayowatambua wataalam hawa waliofanya kazi muda mrefu. Lakini sio tu Kanzidata, iwafuatilie haki zao watu ambao wanasifa za kufanya kazi kwenye managerial position katika migodi kwasababu wakati mwingine wanaondolewa kwa hila.

Mheshimiwa Spika, kwa mfano; migodi ina system inaitwa blacklisting ukifanya kosa kidogo wanakuweka kwenye kitabu cheusi hutafanyakazi sehemu yoyote ile duniani. Vigezo vya blacklisting vinatokana na wale ambao wanakuja na hiyo migodi, mtu amekutwa na sigara kwenye mfuko wake wa suruali unakuwa blacklisted, umesomeshwa kwa gharama kubwa, wewe ni geologist, wewe ni operator huwezi kuajiriwa mahali popote. Tunataka Mheshimiwa Waziri uwalinde Watanzania; kwa kuhakikisha vigezo vya blacklisting vina-qualify na mazingira na utamaduni wa Kitanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niende kwenye Watanzania wanaoweza kutoa huduma na bidhaa kwenye migodi yetu hasa wawekezaji. Wapo Watanzania wengi wenye uwezo, wenye fedha tena hata zaidi ya wale ambao wana supply kwenye migodi.

Mheshimiwa Spika, Tanzania tunazalisha bidhaa nyingi, tuki-customize, tukishusha chini viwango vya bidhaa zinazotakiwa kuwa supplied hasa vyakula, wakati mwingine apples zinapatikana Muheza Tanga lakini yule supplier anazitoa South Africa, hakuna sababu! Wamekuja Tanzania, you are in Rome, act like Romans. Wamekuja Tanzania watakuwa ma-apple ya Kitanzania na Watanzania wapo ambao wanaweza ku-supply kwenye migodi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimuombe sana Mheshimiwa Waziri ili kulinda maslahi ya watu hawa ambao wanaweza ku-supply, best practice tulifanya wakati nahudumu kwenye Mgodi wa Buzwagi na hasa kwenye hili suala wanaloliita CSR na mambo ya local content. Kule mkienda kuwatafuta katika level ya ward (kata), mkaingia kwenye level ya wilaya, mkapanda mkoa mpaka taifa, dhana ya local content itatekelezwa vizuri lakini tukisema tu-generalize useme leo mchicha uchukuliwe Tanzania nzima au ukachukuliwe Dar es Salaam ni lazima utawaacha wazawa wa Shinyanga kwa sababu uwezo wa kuzalisha hauwezi kuwa sawa na wa maeneo mengine. Kwa hiyo, nimuombe sana Mheshimiwa Waziri kusimamia dhana hii ya local content tuwawezeshe na tuwape fursa Watanzania wanaoweza ku-supply kwenye migodi yetu.

T A A R I F A

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Taarifa.

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, nataka nimpe taarifa Mheshimiwa Mbunge anaendelea kuchangia kwamba siyo tu Watanzania wana uwezo wa kupeleka apples na vitu vingine, lakini wapo Watanzania wana uwezo wa ku-supply chemicals na vifaa vikubwa kwenye migodi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niombe Mheshimiwa achukue taarifa hii kwamba Watanzania wapo wengi wenye uwezo thabiti na wanakidhi mahitaji ya kuweza kufanya supply na kukidhi masharti yote kwenye migodi hii mikubwa. Ahsante. (Makofi)

SPIKA: Taarifa hiyo Salome.

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Spika, naipokea taarifa ya Mheshimiwa Saashisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimemaliza dhana ya local content, nije kwenye suala la CSR. Migodi mingi wawekezaji wakubwa wakitupa hizi pesa za CSR wanadhani ni hisani; wanazileta pesa hizi halafu wanatupangia namna ya kuzitumia. Tunazo Halmashauri zetu kuanzia level ya kijiji, kata mpaka manispaa, tunavyo vipaumbele ambavyo vimepangwa na wataalam na wananchi, kama wanatupa pesa za CSR, wapeleke kwenye Baraza la Madiwani.

Mheshimiwa Spika, Baraza la Madiwani wanavyo vipaumbele, wala hawana haja ya kuchakata kwa sababu mwisho wa siku wasije wakatushauri tutengeneze bwawa la samaki Shinyanga Mwendakulima au Ibadakuli wakati pale asili yake ni semi desert. Kwa hiyo, walete kwenye level ya halmashauri, kule wana vipaumbele vyao, sisi tutatekeleza, tukishakamilisha mradi wenyewe wafanye shughuli ya kufanya malipo na kusimamia viwango vya ubora. (Makofi)

T A A R I F A

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Musukuma, taarifa.

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Napenda kumpa taarifa mjomba wangu Salome, nilikuwa nimeacha kumsalimia kwa sababu dishi liliyumba lakini leo mjomba wangu marahaba.

SPIKA: Lakini ninyi mnaopelekewa hizo hela za CSR, Mheshimiwa Musukuma wewe mweyewe umelalamika leo asubuhi zikija kule supervision peke yake wanakula milioni 600, mwingine amelalamika milioni 200, kwa hiyo maana yake zinakuwa squandered. Kwa hiyo, kupeleka huko halmashauri peke yake bado sio dawa.

Mheshimiwa Salome Makamba, dakika zako zilishaisha.

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Spika, nimalizie. Umeongea vizuri sana na hoja yangu nilikuwa nataka nii-cement kwa kusema wasipewe pesa, waende wakachukue miradi ya vipaumbele kwenye halmashauri. Ikishatekelezwa kama ni ujenzi wa barabara certificate itoke, mgodi upelekewe certificate ufanye malipo. Wasipewe pesa zikaingizwa mle kwa sababu kuna risk ya re-allocation, mis-use, corruption na risk zingine. Wasipewe cash money isipokuwa watekeleze miradi ya vipaumbele kama ilivyofanyika kwenye D and OD kama ilivyotekelezwa kuanzia ngazo ya vijiji. Malipo yafanywe na mgodi siyo mgodi ndiyo unapanga halafu shule ya milioni 20 unajenga kwa milioni 50 wanakuja baadaye kusema wametekeleza CSR, CSR sio hisani ni haki ya Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. (Makofi)