Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 –Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 –Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, Nakushukuru kunipa nafasi nichangie wizara hii ya muhimu ya Katiba na Sheria. Mwaka 2018/2019 kwa niaba ya Wabunge wenzagu wanaotetea haki za mtoto wa kike, nilishika shilingi ya waziri ndani ya Bunge hili nikimtaka waziri kufuata maelekezo ya Mahakama ya Rufaani kuleta mabadiliko ya Sheria ya Ndoa; kwa kubadilisha Kifungu cha 13 na 17 ambacho kina mruhusu mzazi kumuozesha mtoto chini umri wa miaka 18, Waziri alitoa majibu ambayo kwa kweli sikuridhika nayo lakini kwasababu wengi wape, walishinda. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mama Samia Suluhu Hassan, amejipambanua kwamba ni mwanamke anayetetea haki, demokrasia, utu na usawa. Namtaka waziri, atekeleze hukumu iliyotolewa mwaka 2017, Kesi Na. 204 kati ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Attorney General. Ambayo mahakama ya Rufaa the sealing ilielekeza ndani ya mwaka mmoja, sheria hii iletwe ndani ya Bunge, Vifungu hivi vifutwe na mtoto wa kike apate haki sawa ya kuamua kuhusu ndoa yake akiwa na miaka 18. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kumuozesha mtoto wa kike chini ya miaka 18 si tu inamuhatarisha maisha yake ni unyanyasaji wa kijinsia, kwasababu hawezi kusimama mahakamani kama haitaki ndoa ile iko chini ya umri. Inamletea madhara ya uzazi anaweza kuzaa Watoto njiti, anaweza kupata fistula; walijitetea Serikali kwamba haya ni mambo ya kidini lakini kipekee kabisa nitoe nukuu ya Baraza la Ulamaa lililokaa mwaka 2019 walisema; “Uislamu umezingatia kuwa hili mwanamke aweze kuolewa ni lazima awe tayari kiakili na kimwili. Hatuwezi kuwanyanyasa Watoto wa kike kwa kuwaozesha katika umri mdogo kuna tofauti kubwa sana kati ya umri wa kufanya mapenzi na umri wa kuhimili mikiki mikiki ya ndoa.” (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, namtaka waziri alete marekebisho haya kudhirihishia sisi Bunge tunaheshimu utawala wa Sheria, tunaheshimu Mihimili mingine kwa kutekeleza maelekezo ya Mahakama. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunayo changamoto kubwa ya Sheria ambayo imetungwa ndani ya miaka mitano. Sheria katika mwenendo wa makosa ya jinai inayohusiana na mambo ya plea bargain yaani kumpa mamlaka Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali kufanya makubaliano na watuhumiwa na kulipwa fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tulipinga ndani ya Bunge hili kuhusiana na sheria hii, kwasababu kwanza; Mahabusu umemuweka ndani, umemuweka kwenye mazingira magumu, amepoteza rasilimali, amepoteza uwezo wa kutafuta fedha, halafu unamuita unamwambia njoo tukubaliane unilipe kiasi kidogo ili nikuachie. Hakuna usawa katika makubaliano hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, yalifanyika, ilitekelezwa sheria ile, fedha zikakusanywa kilichotokea kwa mara ya kwanza na cha kushangaza Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ilivamiwa na fedha zikaibiwa hatujui ziliibiwa shilingi ngapi! hatujui fedha zilikwenda wapi! Mpaka leo hakuna kinachoendelea wamekaa kimya na hakuna anayewajibika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tulifuata Sheria ya Plea Bargain mzizi wake ulikuwa ni Marekani, India waka-adopt mfumo ule, Tanzania tukauchukua tukauingiza Bungeni. Lakini wenzetu walioanzisha Wamarekani waligundua, kwenda ku-negotiate na mtuhumiwa aliyeko mahabusu aliyepoteza kila kitu mpaka utu wake, kwenda ku-negotiate siyo haki. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wamekwenda mbali sasa hivi ni lazima watuhumiwa wafikishwe mahakamani, kama DPP anataka kufanya makubaliano na mtuhumiwa waende mahakamani, mahakama ijiridhishe kwamba makubaliano yale yanazingatia kwamba mtuhumiwa yule hajalazimishwa na hakuna mazingira ya mashinikizo mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kama tunataka kwenda suala ya plea bargain nimuombe Mheshimiwa Prof. Kabudi turudishe hapa hii sheria, isiwe wanajifungia chumbani mtuhumiwa na Mwendesha Mashtaka wa Serikali wanakubaliana wanakwenda kufanya plea bargain. Iwe ni kati ya mtuhumiwa, mahakama na DPP wakubaliane ionekane uwanja wa makubaliano ulikuwa sawa ndio mtuhumiwa aweze ku-bargain. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tena naomba nishauri twende mbali zaidi, twende tukafanye evaluation ya utekelezaji wa sheria ya plea bargain tangu tumeitekeleza. Wote hapa tuna smart phone mnaona twites za watu ambao wamefanya plea bargain, mambo ya kinyama yanayofanyika kwenye hizo magereza mpaka wale watu wanakubaliana kulipa zile fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, iundwe tume Maalum, kwa ajili ya kwenda kufanya uchunguzi na kupima ufanisi wa sheria hii. Watu wamenyanyaswa, watu wamenyang’anywa mali zao, wameporwa kupitia plea bargain, fedha zetu zimepotea hizo ambazo zimeshatolewa kwenye plea bargain, iundwe Tume Maalum kuangalia ufanisi wa sheria hii ambayo tumeitunga ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na twende mbali zaidi nimuombe Mheshimiwa Prof. Kabudi anapokuja kuhitimisha atueleze fedha zetu za plea bargain zimepoteaje! Attorney General akafanye uchunguzi kwanza zile pesa zilikuwa shilingi ngapi? Ambazo zilifanyika kwenye plea bargain. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, umenipunguzia muda wangu mpaka dakika tano na naheshimu Kiti chako. Naomba niende kumalizia hoja moja tu. Au umeniongeza mama! (Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimalizie hoja moja ya Katiba mpya; Mama amesema vizuri na amesema kwa kututia matumaini kwamba tusubiri kidogo, sisi wengine ni wasukuma kidogo hatuelewi maana yake ndio mpaka amalize au nini.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kikubwa ninachotaka kusisitiza na kumuomba mama yetu suala la Katiba Mpya yeye alikuwa ni Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Katiba. Anajua shauku ya Watanzania kwenye Katiba Mpya. Anajua gharama zilizotumika kuhakikisha Katiba imefikia ilipofikia na pengine ipo hatua za mwisho kabisa. Tunaheshimu kauli yake basi kidogo hii ya Mheshimiwa mama yetu Mama Samia Suluhu Hassan angalau basi isitufikishe kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Kwa sababu hapo ndipo tunapoanzia kuchefuana, tusifike huko, ajitahidi kidogo hii iwe ndani ya hii miaka miwili akishakuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi basi asimamie ilani yenu ya Chama Cha Mapinduzi. Nakushukuru sana. (Makofi/Kicheko)