Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Nami napenda kuunga mkono hoja hii ya Wizara ya Elimu. Nampongeza sana Mheshimiwa Waziri kwa kazi nzuri anayoifanya pamoja na Naibu Waziri wake, lakini vile vile na Uongozi mzima wa Wizara ya Elimu kwa kazi nzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nijibu hoja chache zinazohusiana na masuala ambayo yako chini ya Utumishi ili kuweza kutoa ufafanuzi kidogo. Hoja ya kwanza ambayo ni kuhusiana na madeni mbalimbali ya malimbikizo ya mishahara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda tu kulieleza Bunge lako Tukufu kwamba Serikali imekuwa ikiwalipa watumishi mbalimbali wakiwemo Walimu na Watumishi wengine ambao sio Walimu, madai yao mbalimbali ya malimbikizo ya mishahara. Kwa mwaka huu wa fedha kuanzia Julai, 2015 hadi 25 Mei, mwaka huu wa 2016, Serikali imeshalipa madai ya Watumishi 24,677 yenye thamani ya shilingi bilioni 22.9. Kati ya madai haya ya shilingi bilioni 22.9 Walimu 14,366 waliokuwa wakidai takribani shilingi bilioni 10.7, wameshalipwa madeni hayo ya malimbikizo ya mishahara. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa tumeshapokea madai mbalimbali ambayo yalipokelewa manually na mengine ambayo yalikokotolewa kwa mfumo wa ni automatic, tunaendelea kuhakiki madeni yenye thamani ya shilingi bilioni 11.5 na yatakapothibitika kwamba kweli madai hayo ni halisi, basi yataweza kulipwa bila shaka yoyote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile yapo madeni ya takriban shilingi bilioni 2.3 tayari yameshahakikiwa ya Walimu zaidi ya 1984 na wakati wowote yanasubiriwa kulipwa. Kwa hiyo, ni imani yangu yataweza kulipwa kwa wakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nieleze tu, kwamba tangu tuliposimika mfumo wa taarifa za kiutumishi na mishahara au Lawson mwezi Mei mwaka 2012, tumekuwa tukitekeleza ulipaji wa madai mbalimbali. Changamoto kubwa ambayo tulikuwa tukiipata, kwanza ukiangalia katika mfumo ulikuwa unakokotoa madai haya automatically, yaani kupitia mfumo. Wakati huo huo watumishi mbalimbali wenye madai au Walimu wakiwemo, wengine walikuwa wakileta pia taarifa zao manually kwa madeni yale yale na mengine unakuta yalikuwa yanaenda tofauti na madeni ambayo yalikuwa ni automatic arrears.
Kwa hiyo, hii ilikuwa inatupa taabu, unajikuta umepokea deni huku na huku pia umepokea. Kwa hiyo, ilikuwa ni lazima tuendelee na uhakiki. Nawaomba tu Walimu na Watumishi wengine wawe na subira lakini wajitahidi kuhakikisha kwamba wana-submit madai ambayo ni ya kweli na halisi. Aidha, nawaomba zaidi waajiri wazingatie hili kwa sababu hatuta- entertain manual arrears, tuna-entertain zaidi automatic arrears claims tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto nyingine ambayo imekuwa ikitupata kama Serikali na ambayo imekuwa ikisababisha madai haya ya malimbikizo ya mishahara, mfumo huu tulionao wa taarifa za malipo ya mishahara, hauwezi kukokotoa madai au malimbikizo ya mishahara ambayo yanawasilishwa, watu wanaingia kwenye payroll kuanzia tarehe 15. Bado ulikuwa haujajengewa uwezo wa kuweza kukokotoa madai ya siku kwa siku. Mtu anayeingizwa baada ya tarehe 15, labda amekaa siku 14 tu, lakini kwa sasa tunaendelea kulifanyia kazi na ni imani yangu ndani ya muda mfupi suala hili litaweza kuwa limekwisha kabisa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile ilikuwepo hoja kwamba baadhi ya Walimu na watumishi wengine wamekuwa hawaingizwi katika orodha ya malipo ya mishahara kwa wakati. Kwa takwimu nilizonazo za mwaka 2014 na 2015, tulikuwa na ajira mpya 56,816 na kati ya hizo ajira 57,036 zilishaingizwa katika mfumo wa human capital management information system na kati ya ajira hizo, ni ajira mpya 2020 peke yake ndizo tuliwarudishia waajiri ili waweze kufanya marekebisho mbali mbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, napenda tu kusema kwamba tayari ajira zaidi ya 57,036 zimeingizwa katika mfumo. Vile vile, nitumie nafasi hii kuwakumbusha waajiri kuhakikishia wanawaingiza waajiriwa wapya mapema katika mfumo huu wa payroll pindi wanapokuwa wamepangiwa katika maeneo yao ya kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja nyingine ambayo ilitolewa ni kuhusu kuweka posho ya kufundishia au kuirudisha pamoja na posho ya mazingira magumu. Serikali inatambua ugumu wa kazi ambao wanaipata Walimu, lakini vile vile inatambua umuhimu wa kada hii muhimu. Kwa kutambua hilo, tunayo nia ya kuboresha maslahi mbalimbali ya watumishi ikiwemo Walimu na kuhakikisha kwamba tunawapa mishahara ambayo kwa kweli itakuwa imeboreshwa. Lengo letu ni kwamba badala ya kulipa posho zaidi, tutahakikisha kwamba tunaboresha mishahara. Tumeshaanza zoezi la tathmini ya kazi pamoja na upangaji wa madaraja au job evaluation na kama ambavyo nilieleza katika bajeti yetu, zoezi hili litakamilika ifikapo mwezi Februari, mwaka kesho 2017.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii itakuwa siyo kwa ajili ya kada ya Walimu tu, bali Serikali nzima kwa ujumla wake kwenye watumishi wa Umma. Tutaoanisha na kuwiainisha mishahara pamoja na posho mbalimbali au marupurupu mbalimbali ambayo wanayapata. Tutaangalia pia aina ya kazi; kama ambavyo nilieleza, siyo kwa Walimu tu, tunatambua umuhimu lakini na wenyewe pia wataangaliwa kuona namna gani wataboreshewa. Unakuta kuna Mtumishi X, mwenye sifa sawa, elimu sawa, uzoefu sawa kazini labda mmoja ni Mwanasheria EWURA, mwingine ni Mwanasheria kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali lakini unajikuta wanapishana mishahara wengine mara tano mpaka hata mara kumi. Tukasema hili haliwezekani. Kwa hiyo, naomba Waheshimiwa Wabunge tuvute subira, eneo hili tunalipa kipaumbele kikubwa na Walimu tutawazingatia katika uboreshaji wa mishahara yao na maslahi mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ambalo limesemewa sana na Waheshimiwa Wabunge ni suala zima la upandishaji wa madaraja kwa Walimu. Serikali imeshawapandisha Walimu 85,533 madaraja yao katika mwaka huu tu wa fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia idadi hii ni takriban asilimia 28.5 ya Walimu wote waliopo katika Utumishi wa Umma. Vile vile, tumekuwa tukiendelea kuboresha maslahi ya Walimu, lakini vile vile kwa kupitia Muundo wa Utumishi wa Walimu wa mwaka 2014 tuliweza kufungulia ukomo wa kupanda vyeo kwa Walimu na Halmashauri mbalimbali zimekuwa zikianza kuwapandisha madaraja waliofikia ukomo na wale ambao walikuwa hawajafikia ukomo. Natambua Halmashauri mbalimbali wanaendelea na vikao kuona ni kwa namna gani basi wanaweza kuhakikisha kwamba watumishi hawa wanaweza kupandishwa madaraja yao kwa wakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja nyingine ambayo imekuwa ikisumbua sana na ambayo inaendana na upandishwaji wa madaraja, unakuta watumishi wengine na Walimu wanapandishwa madaraja lakini mishahara yao wanakuwa hawajarekebishiwa kupata mishahara mipya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka huu wa fedha ambao tunaumalizia, tumeweza kurekebisha mishahara ya Walimu 57,898 ambao walipandishwa madaraja katika mwaka huu wa fedha. Aidha, katika idadi hiyo kama nilivyoeleza Walimu 4,927 tumekuwa tukihakiki taarifa zao na wakati wowote kuanzia sasa wataweza kurekebishiwa mishahara yao. Vile vile, kwa ambao walipandishwa madaraja, lakini vielelezo vyao vimekuwa havijitoshelezi ni Walimu 23,314.
Kwa hiyo, naomba waajiri mbalimbali waendelee kufuatilia kuhakikisha kwamba Walimu hawa wanaweza kurekebishiwa mishahara yao kwa wakati kwa sababu sisi kama Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, tulishakasimu mamlaka kule kule chini kwa waajiri kwa ajili ya kuboresha huduma na kuisogeza huduma karibu zaidi na watumishi hawa.