Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Awali ya yote, nimshukuru Mwenyezi Mungu kunijalia uzima na afya hata kurudi tena jioni hii na kuanza kuchangia hoja hii.

Mheshimiwa Spika, kwanza napongeza kusainiwa kwa hati tano za makubaliano ya kuondoa hoja za Muungano zilizopatiwa ufumbuzi mfano kushirikishwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwenye masuala ya kitaifa na kikanda. Suala hili tunashukuru sana kwamba limeondoa kero hizi na sasa hivi hivi tuko katika Muungano wa uhu na haki ambao hauwezi kupingika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nizungumzie kuhusu kuratibu masuala ya kiuchumi na kijamii hasa suala hili la TASAF Awamu hii ya Tatu. TASAF Awamu hii ya Tatu kuna jambo hawajalitekeleza na kipindi kile tulichopita walikuwa wanafanya semina kule Zanzibar na wanashirikisha Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya pamoja na viongozi wengine lakini pia walitushirikisha na sisi Wabunge wa Zanzibar tunapewa semina na kupata mafunzo elekezi ili kwenda kuwafanyia wajasiriamali. Kwa hiyo, naomba hizi semina zifanyike tena kwa hii awamu ya tatu na washirikishe viongozi kama vile walivyoshirikisha mwanzo.

Mheshimiwa Spika, nizungumzie suala la mazingira. Kule kwetu katika Mkoa wetu wa Kusini kuna Kijiji kinaitwa Marumbi. Kijiji kile kutokana na tabianchi maji yakajaa hadi kufikia kubomoa makaburi kwa sababu kule wanazikia maeneo pwani. Kwa hiyo, kutokana na tabianchi maji yalipanda juu na kuvunja makaburi yale. Serikali yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilichukua hatua lakini sehemu nyingine bado maji yanachimbuka. Kwa hiyo, naomba suala hili lifanyiwe kazi tena na kama kuna uwezekano Mheshimiwa Waziri tuungane twende katika Mkoa wa Kusini Kijiji cha Marumbi akaone hiki nachokiongelea ikiwa ni pamoja na upandaji wa koko. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niendelee kuchangia kuhusu suala la Bodi ya Mkopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu. Suala la mikopo ya elimu ya juu watoto wetu wanapokuwa wanataka mikopo hili suala linakuwa kubwa na linakuwa zito, wanahangaika kwa kuwaona kwa macho yetu mpaka wakaipata ile mikopo basi wanakuwa wako hoi. Kwa hiyo, naomba Bodi hii ifanye kazi zake vizuri, watoto wanapotaka mikopo ili kwenda kujisomea basi wafanyiwe kiurahisi. Wanapokwenda kule benki wasihangaike wapate pesa zao za mikopo na waende wakafanyie kazi.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja asilimia mia. Ahsante sana. (Makofi)