Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

3

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. ALLY J. MAKOA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi hii lakini niwapongeze Mheshimiwa Jafo na Mheshimiwa Chande kwa wasilisho lililo zuri kabisa kwenye bajeti yao. Nilikuwa naomba nichangie eneo dogo la mazingira wewe unafahamu mji wa Kondoa umekatiza mto mkubwa pale, sasa mto ule umehama kutoka njia yake ya asili kwenda mto mkondo mdogo.

Mheshimiwa Spika, huu ni msimu wa pili madhara yanayotokea kwenye mto ule ni makubwa sana nilikuwa naomba Wizara iweke fungu kwa ajili ya kuurudisha ule mto kwenye mkondo wake wa asili. Kwasababu madhara ambayo yanatokea kwa hivi sasa kwanza maji ni mengi yana-force kuingia kwenye mkondo mdogo, mashamba ya watu yanaendelea kumegwa na maji yanaelekea kwenye nyumba za watu, kama hatujaudhibiti kwa kwa wakati mto ule maeneo ambayo yanakwenda kuathirika ni pamoja na shule za msingi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, shule ya msingi Mpalangwi eneo lote la kanisa la Katholic makaburi yaliyopo kule pamoja na Chuo cha Bustani, kwasababu mto wenyewe ule ni mdogo sana maji yanatafuta njia mbadala ya kupita, kwa sasa kwasababu ni mkondo mdogo maji yanaingia mashambani yanakwenda kuharibu mazao ya wananchi. Lakini sio hiyo tu miundombinu ya TANESCO pia ipo mashakani kwasababu zipo nguzo ambazo tayari na zenyewe zimekwisha kufikiwa na maji.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nilikuwa naomba watenge fedha kwa ajili ya kurejesha ule mto katika chanzo chake cha asili. Aidha, Mheshimiwa Waziri aagize watu wa NEMC waende wakafanye tathmini mapema ili kuweza kuurejesha ule mto katika chanzo chake cha asili. Hasara nyingine inayojitokeza barabara ile inayotoka Iboni kuelekea Bolisa mpaka Gubali inakuwa haipitiki kwasababu Serikali itakuja kuingia gharama kubwa ya kujenga madaraja makubwa.

Mheshimiwa Spika, msimu wa mvua uliopita daraja ambalo lilijengwa na gharama kubwa na Serikali lilisombwa na maji zima zima kama lilivyo likahamishwa zaidi ya mita 200, kwa hiyo, pale fedha ya Serikali ilipotea kabla daraja halikuanza kujengwa, ni kwasababu ya nguvu ya maji ambayo ilikuwa inatoka kwenye mto mkubwa kwenda kwenye mto mdogo. Nilikuwa naomba tu eneo hili ili kuokoa hata shughuli za kiuchumi za wananchi wa kata ya Kondoa Mjini na Kata ya Bolisa kuelekea kata ya Kolo Gubadi zile barabara ili ziwe salama inabidi mto huu urejeshwe kwenye mkondo wake wa asili.

Mheshimiwa Spika, baada ya kuyasema hayo ninakushukuru sana kwa nafasi hii ahsante sana naunga mkono hoja. (Makofi)