Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Mwanakhamis Kassim Said

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Magomeni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. MWANAKHAMIS KASSIM SAID: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii ya kuweza kuchangia Wizara hii ya Muungano.

Mheshimiwa Spika, niende moja kwa moja kwenye mchango wangu. Leo tunazungumza ni mwaka 57 wa Muungano wetu na tunasema Muungano huu tutaulinda na tutautetea na ndipo tunapozungumza tunasema mbili zatosha, tatu za nini. Leo toka tulivyoanza kuchangia Muungano huu Wazanzibar ndiyo tumepangwa kuchangia. Kwa kweli inasikitisha na inaumiza kwa sababu huu Muungano siyo wa Wazanzibar peke yetu ni Muungano wa Tanzania nzima. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini ukizungumza hapa ukisema leo ni miaka 57 Muungano huu asilimia kubwa sisi viongozi wenyewe hatuujui na tunashindwa kuuzungumzia, zaidi tukizungumzia Muungano tutauzungumzia kisiasa, kumbe Muungano huu ni tunu ya nchi yetu; ni moyo wa nchi yetu; ni mishipa ya nchi yetu. Sisi tunasema tunatoka Zanzibar lakini na sisi vitovu vyetu vipo huku. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi baba ni Mpemba, mama ni Mzaramo. Tunapouzungumzia Muungano lazima tuuzungumzie Muungano wa Watanzania; tuzungumzie Muungano wa wanyonge na tumzungumzie mtu wa chini.

Leo unapokwenda mikoani; utamkuta mwananchi kutoka Mtambwe lakini yupo Shinyanga na Shinyanga kule amewekeza kiwanda cha mchele lakini kuuzungumza Muungano kusema hajui, kwa sababu gani? Ni kwa sababu hatupewi elimu, wala wananchi hawapewi elimu kuhusu Muungano wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo unapokwenda mikoani, utamkuta mwananchi kutoka Mtambwe, lakini yupo Shinyanga; na kule amewekeza kiwanda cha mchele, lakini kuuzungumza Muungano, kuusemea hajui. Kwa sababu gani? Kwa sababu hatupewi elimu, wala wananchi hawapewi elimu ya Muungano wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, namwomba Mheshimiwa Waziri, kwenye utalii tunapeperusha vipeperushi vya utalii. Kwa nini na Muungano tusipeleke vipeperushi wananchi wakaufahamu Muungano huu? Tumenyamaza zaidi! Leo tunanyanyuka kuzungumza Habari za Muungano, tunashindwa. Tunazungumza zaidi kisiasa, lakini kuuzungumza ile ilivyo, tunashindwa. Wapi tunafaidika, hatupajui; wapi tunakosea, hatujui; wapi tunapokwenda, hatujui. Tutayazungumza yale madogo madogo, lakini na makubwa yapo yanaumiza.

Mheshimiwa Spika, jimboni kwangu, Jimbo la Magomeni kuna wanawake hawana uwezo wa kwenda China, China yao ni Kariakoo, wanakwenda kuchukua madera, khanga, viatu wanaleta Zanzibar. Utakuta amekwenda na mwananchi kutoka Mwanza, atachuka mzigo wake ule atakwenda kuuza Mwanza, lakini mwanamke anayetoka Zanzibar Magomeni, anateseka akifika bandarini. Muungano huo, miaka 57, tunaomba mambo haya mdogo madogo yaondolewe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa hivi sisi ni wamoja, ni ndugu, ni wazaliwa wa damu moja na tumbo moja, wa baba mmoja. Wameshapita viongozi wengi katika nchi hii, lakini bado wanasema wataulinda na watautetea kwa nguvu zote. Nasi tunasema tutaulinda na tutautetea kwa nguvu zote. Tunasema mbili zatosha, tatu za nini? Hatuoni haya, hatuoni aibu wala hatujuti, tunasema Muungano utaendelea kwa yeyote atakayekuja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikitoka hapo, Mheshimiwa Marehemu Dkt. Omary Ali Juma alikuwa ni Makamu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Alikuwa Waziri Kiongozi miaka minane, akawa Makamu wa Rais miaka saba. Alizikwa vizuri, kwa heshima zote, tunashukuru; lakini leo ukienda kwenye kaburi la Marehemu Dkt. Omary, inauma sana. Kwa kweli inatusikitisha. Mheshimiwa Dkt. Omary aliitumikia nchi hii kwa nguvu zake zote, hakuna ambalo hakujua. Alikuwa ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Spika, leo Mheshimiwa Dkt. Omary kaburi lake lina uzio wa waya toka laipozikwa hadi leo. Maana kaburi lile utasema siyo Makamu wa Rais, kama nililozikwa mie tu, nikaenda nikazikwa, nikawekewa kuti, watu wakaondoka. Kwa kweli inauma. Viongozi wetu waliopita tunawaacha. Tunawadhalilisha. Hii inauma, inakera. Wao wameanza, imefikia hivyo, wengine itakuwaje? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sina zaidi, naunga mkono hoja. (Makofi)