Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Maryam Omar Said

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Pandani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. MARYAM OMAR SAID: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii na nikaweza kuchangia katika sehemu ya Bajeti ya Wizara ya Muungano na Mazingira. Zaidi nitajikita katika sehemu ya Mazingira lakini nitaenda zaidi katika sehemu ya Mazingira ya nchi kavu. Namshauri kwanza Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri, tusiangalie tu mazingira ya bahari bali tuende zaidi na mazingira ya nchi kavu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye mazingira ya nchi kavu, ni vizuri kwamba tunasema tunashajihisha sana kwamba tupande miti, lakini naomba tushajihishe kupanda miti lakini pia tushajihishe kuitunza miti hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwenyewe binafsi ni mtu ambaye kwamba jimbo langu lipo katika mazingira hatari sana la miti ambayo kwamba ni mashamba ya Serikali. Mashamba haya ya Serikali yenye kilimo cha miti ya mipira, zamani ilikuwa ni mazuri yana faida kubwa kwa wananchi wangu wa Jimbo la Pandani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini kwa sasa imekuwa ni changamoto kubwa sana ndani ya Jimbo langu la Pandani. Yale mashamba zamani yalishughulikiwa vizuri, yakafyekwa vizuri, kiasi ambacho kwamba ulikuwa unauona mti uliopo mwanzo wa kwenye heka mpaka mwisho wa heka. Lakini sasa mashamba yale yamevamiwa na miti ambayo kwamba, si rasmi na kufanya sasa mashamba yale yamegeuka kuwa mapori na kuwa sasa, yanahatarisha maisha ya wananchi wangu ndani ya Jimbo langu la Pandani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vitendo vingi vya uhalifu vinafanyika ndani ya mashamba hayo ya Serikali kutokana na mazingira yaliyopo. Tunaona sasa imefika hadi hata mwanafunzi akitoka kwenye Shehia moja kwenda kwenye Shehia nyingine, ambapo kwamba anafuata huduma ya elimu inakuwa ni mtihani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wabakaji hutumia maeneo hayo kwa kutimiza matakwa yao, kitu ambacho kwamba sasa wananchi wangu wanaishi wakiwa roho juu. Namuomba sana Waziri pamoja na Naibu Waziri. Naibu Waziri analijua hili kwasababu, ni mtu ambaye kwamba yupo jirani yangu ndani ya Jimbo langu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, afike katika maeneo yale na aniangalie kwa jicho la huruma, lakini pia ayasimamie mazingira ya Jimbo lile, katika mashamba yale ili kuondoa changamoto zile. Yale ni mashamba ya Serikali leo kama Serikali tunashajihisha kupanda miti, lakini miti yetu wenyewe hatuitunzi, hivi tunafikiria kipi ambacho kwamba kitaendelea hapo baadaye? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hata hiyo miti inayopandwa inaweza kuja baadaye ikawa changamoto pia kwa wananchi. Namuomba sana Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri hebu tuliangalie hili. Tuangalie mazingira ya bahari lakini pia tuje katika mazingira ya nchi kavu. Katika mashamba haya kumeshawahi kufanyika mauaji makubwa yaliyolitikisa Jimbo na Taifa kwa ujumla. Kijana mdogo tu, aliuliwa ndani ya mazingira haya, mara nyingi sana vinatokea vitendo vya ubakaji ndani ya mazingira haya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sitaki kuzungumza mengi na sitaki nipoteze muda, niliona kama sikulisema hili hapa sitopata nafasi kulisema pengine na wananchi wataniandama kwa hili. Wataniuliza, ulipata nafasi kwa nini hukulichangia? Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri, nakuombeni mfike katika mazingira yangu ya Jimbo na muweze kuniwekea mazingira sahihi kwa mashamba yale. Ahsante sana. (Makofi)