Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Ahmed Yahya Abdulwakil

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. AHMED YAHYA ABDULWAKIL: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, asubuhi ya leo baada ya kumshukuru Mwenyezi Mungu ambaye tupo katika mfungo, mimi naheshimu sana heshima hii ya kupewa kuwa mchangiaji wa mwanzo katika wizara hii ambayo ni ya uhai wa maisha yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kikawaida sina uchangiaji mkubwa sana maisha yote na nitatumia haitozidi dakika tatu, nne mpaka tano. Kwa hiyo nitasevu muda kusudu ajaye apate nafasi ya kuongea zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitaongea upande wa Mazingira (Environment). Katika hotuba ya Mheshimiwa Rais, hapa alitumia dakika tatu, jinsi anavyojali na kuthamini mazingira. Kwa njia hii alipitia kiatu hiki kabla ya leo kufikia kuwa Rais wa Tanzania, kwa hiyo tumpongeze sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa ufadhili hapa kidogo ndiyo nataka Mheshimiwa Waziri atakapokuja ku-wind up hotuba yake, dunia imekuwa sana katika upande wa mazingira na mikutano mbalimbali inafanyika ulimwenguni kwa sababu ya kuhifadhi mazingira. Kwa hiyo, kwa upande wa Zanzibar kuna PECCA ukanda wa PECCA ni ukanda mali sana huu, ambao kwa namna moja au nyingine umeingia katika ramani ya dunia pamoja na kisiwa cha Misali. Misali kuna kisiwa, kuna bahari na kuna bustani chini ya ulimwengu ambayo si nchi nyingine ni natural. Sasa lazima yalindwe kimazingira kwa hiyo tulikuwa na wasiwasi kama nchi kwamba vipi hali ya ufadhili wa kimazingira katika hizo sehemu ambazo kubwa zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukiangalia katika uchumi, Tanzania tunakusudia kununua meli nane (8) za uvuvi; meli nne (4) Tanzania Bara na nne(4) Tanzania Visiwani.

Katika uvuvi, kuna siri kubwa sana ya kupata harvest yaani mavuno kwa kutumia matumbawe. Haya kama hayakuhifadhiwa kimazingira, mara nyingi samaki wanahama na kutakuwa hakuna pia samaki wenyewe tunaokusudia, meli itakuja na hatutavua. Sasa napenda kujua wakati Mheshimiwa Waziri akija ku-wind up, atueleze hali ya kimazingira ya matumbawe, nchi zote baina ya Zanzibar na Tanzania Bara ikoje kusudi tuweze kufaidi neema hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nyuma kuna mfuko ukiitwa, Mfuko wa Kusaidia Nchi Masikini katika Kuokoa Mazingira (LDCF). Sasa wakubwa duniani wana hiari yao kutusaidia au kutosaidia hali ikoje katika kupambana na hali hii na ufadhili, ili kusudi tuweze kuishi katika ustahi mazingira mazuri kwa nchi yetu? Ahsante sana. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana Ahmed, lakini jina lako huwa linanipa tabu kidogo, unauhusiano gani na Mzee Abdulwakil?

MHE. AHMED YAHYA ABDULWAKIL: Mheshimiwa Spika, jina langu kamilifu naitwa Ahmed Yahya Abdulwakil Mbunge wa Kohani. Tunao uhusiano wa kijomba wa huko nyumbani. (Makofi/Kicheko)

SPIKA: Ahsante sana Ahmed.

MHE. AHMED YAHYA ABDULWAKIL: Sikutaka kuweka sawa ehe! Kusudi watu wakatishika, hamna! (Kicheko)

SPIKA: Kiti changu kimekuwa kikipata tabu kidogo. Nashukuru kwa ufafanuzi huo, Ndugu yangu Ahmed.