Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kukushukuru kwa kiti chako kuniona walau niwe miongoni mwa wachingiaji wa hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora. Mimi naomba nichangie maeneo mawili; moja umuhimu wa dhamana ya utumishi katika Serikali yetu, lakini la pili nakisi ya imani ya wananchi wetu katika utumishi wa umma. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli tunapozungumzia utumishi ni dhana ambayo inahitaji tafsiri mpya na hasa ukizingatia katika Taifa ambalo sekta binafsi imeajiri watu wengi ambao wanautumikia umma kiasi ambacho tafsiri ya utumishi umma inakosa maana ama inayumba yumba hapa katikati. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, utakuta watu wengi katika sekta binafsi wanatumikia umma kuliko watumishi wenyewe, utakuta watu wanapata shida katika ofisi ya umma kiasi ambacho wanapata huduma bora zaidi ambazo zilikuwa zinapaswa kubebwa na ofisi ya umma katika taasisi binafsi. Na ndio maana mfumuko huu wa mashirika yasiyo ya kiserikali ambayo yanahudumia watu yamechukua sana majukumu ya watumishi wetu Serikalini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nilikuwa naomba watu ambao wanaomba ajira Serikalini na wale ambao watumishi walipoko Serikalini wajue dhamana waliyonayo, kwamba wao ndio kioo cha Serikali wanapoenda kuhudumia watu wao ndi Serikali, mwananchi anapofika katika ofisi ya umma kwenda kuomba ama kusiliza shida yake yule ndio Serikali, na dhamana hii ni ya muda ni lazima watumishi wetu wafahamu kwamba hatma ya nchi yetu ipo mikononi mwa mtumishi wa umma. Lakini watumishi hawa wanahitaji pia maandalizi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ni mjumbe wa Kamati ya USEMI ya Utawala na Serikali za Mitaa kilio kikubwa cha Chuo cha Utumishi pale Magogoni ni kwamba hawana wanafunzi wa kutosha ambao ni watumishi wa Serikali. Wanafunzi wengi ambao wanasoma katika chuo hiki wanalipiwa na wazazi na wengine wanatoka majumbani. Tunapoteza lengo la msingi la chuo hiki kuwanoa na kuwafundisha watumishi wa Serikali hili kuboresha utumishi wao kwa umma wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni ambalo nilikuwa naomba kuchangia ni dhana ya uzalendo; kwa wenzetu kazi za kujitolea ndio msingi wa uzalendo katika Taifa lao. Sisi hapa pia tuna vijana wengi ambao wanajitolea kwenye sekta mbalimbali hasa elimu, lakini vijana hawa ajira inapotoka miongozo ya utumishi haiwatambui. Sasa ni wakati, wakati tunaboresha teknolojia, watu sasa hivi wana apply kazi kwa mitandao tuwe na vigezo vya kuangalia vijana ambao wanajitolea katika mazingira mbalimbali na kujitolea kuwe sehemu ya mahitaji ama sehemu ya masharti ya watu ambao wanaweza wakapata added advantage pale wanapoomba kazi Serikalini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wetu wana malalamiko mengi hasa watumishi wa umma, kuna wengi ambao walisimamishwa kinyume cha sheria wakati ule wa mjadala wa vyeti fake na wafanyakazi hewa na baadae wakarejeshwa kwenye ajira zao. Lakini naomba kuchukua nafasi hii kuwasikitika mpaka sasa wengine hawajalipwa malimbikizo yao na wengine waliachishwa kazi barua zimetoka za kuwarudisha kazini, hawarejeshwa kazini mpaka sasa hivi. Nilikuwa naomba kutumia nafasi hii kutoa rai kwa ndugu zetu wa Utumishi, kuona ni jinsi gani wanaenda kuhakikisha kwamba wale watumishi ambao waliondolewa kimakosa basi wahakikishe kwamba malimbikizo yao ya mishahara yanaenda kurejeshwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ambalo linazungumzia suala malimbikizo ya mshahara ni watumishi wale wahanga 2,000 wa Ilovo. Wakati tunabinafsisha mashirika ya umma, kuna Watanzania wengi waliachishwa kazi na malimbikizo yao mpaka leo hawajalipwa na wengine walilipwa pungufu na hawajui mahali pakwenda kulalamika PSRC wanasema watalipwa na mwajiri, mwajiri anasema watalipwa na Hazina. Kwa hiyo watu hawa bado wana kilio kikubwa naomba sana Wizara ya Utumishi iwaangalie hasa hawa wahanga 2,000 kule Ilovo ambao mpaka sasa hivi wana kesi mahakamani lakini kuna wengine ambao hawana kesi mahakamani wanaagaikia malipo yao.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana.

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono hoja.