Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na nianze kwa kuchangia hotuba ya bajeti ya Wizara Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora. Lakini kwa upekee nianze kutambua changamoto za watumishi hususani kundi la walimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, walimu ni sehemu ya watumishi katika nchi hii lakini kama tunawasikiliza vizuri inaweza ikawa ni miongoni mwa kundi lenye changamoto nyingi zaidi ikiwemo kama ambavyo Wabunge wengine wamechangia kucheleweshwa kupandishwa kwa madaraja ikiwemo mapunjo baada ya kustaafu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hapa nina case study mbili naomba nizitaje; katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa, kuna mwalimu anaitwa Mwalimu Hadija Salum Bugurumo alistaafu mwaka 2020; alistaafu akiwa na Daraja F, mshahara aliolipwa ni wa Daraja E, na kwa maana hiyo anadai mapunjo. Pia kuna mwalimu anaitwa Mwalimu Salma Khamis Kaisi, naye kadhalika alistaafu mwaka 2020 lakini alipandishwa daraja tangu mwaka 2017 na amelipwa mafao yake ya kustaafu kwa mapunjo bado wanaidai Serikali mpaka leo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa masikitiko makubwa hawa ni walimu wangu ambao wamenifundisha mimi shule ya msingi Mnazi Mmoja, Kilwa Masoko na wamesema mwanangu, mwanangu katusaidie kutusemea huko na hapa nawasemea, Serikali iwasikie. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hayo pia, kama ambavyo Wabunge wengine wamechangia kumekuwa na changamoto kubwa sana ya kupewa gharama za kusafirisha mizigo baada ya kustaafu. Walimu wangu wawili hawa ambao nimewataja kwa mfano tu kwa niaba ya wengine walio wengi nao pia wanakumbwa na kadhai hii hawajalipwa mizigo ya kustaafu bado. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya eneo hilo, nizungumzie pia mazingira ya ufundishaji kwa walimu. Kada zingine hapa Tanzania kumekuwa na namna fulani fulani hivi ya kufikiriwa kimotisha motisha zipo kada ambazo wanalipwa kinachoitwa ration allowance, zipo kada wanalipwa on call allowance kwa maana ya kada ya sekta ya afya, ambayo hiyo on call allowance kwa sababu ya ule muda wa ziada mtumishi wa sekta ya afya anapoitwa kwa ajili ya kwenda kutoa huduma. Lakini walimu hawajafikiriwa, huko nyuma tulipata kuambiwa kwamba kulikuwa na kitu kinachoitwa teaching allowance na hii ilizingatia mazingira ya walimu yalivyokuwa magumu katika kuandaa somo lenyewe, kufundisha na kufuatilia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ualimu hauishii kufundisha tu darasani unaandaa scheme of work ya mwaka mzima kama si kwa muhula mzima, ukitoka hapo unaanda lesson plan, ukitoka hapo unaandaa lesson notes, ukitoka hapo unasahihisha kazi na kufuatilia mwafunzi mmoja baada ya mwingine, lakini pia work load ni kubwa. Mwalimu anatakiwa afundishwe wanafunzi 40 mpaka 45 kwa darasa moja. Walimu wetu hawa wanafundisha wanafunzi mpaka 200 kwa darasa moja hii ni work load kubwa wafikiriwe na wao kupata teaching allowance wapate motisha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie suala la watumishi nitumie lugha kwamba wametelekezwa, hawa walikuwa ni watumishi waandamizi wakapata nafasi za kuteuliwa na mamlaka zao, mamlaka zao za uteuzi baada ya kuwaacha katika nafasi hizo hawajarudishwa bado katika utumishi wa umma na ndio maana nimetumia lugha ya wametelekezwa. (Makofi)

Naomba Ofisi ya Rais Utumishi iwafikirie watumishi hawa kwa sababu na wao ni watumishi kama watumishi wengine na wana haki ya kufikiriwa, hawajapata pension zao, hawajapata maslahi yao yoyote, wamebaki kama walivyo kama wakiwa ndani ya nchi yao, hii sio sawa Ofisi ya Rais iwafikirie hawa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho niseme kwamba wale watumishi ambao walifikia nafasi za uteuzi kama vile Wakurugenzi, Ma-DAS na wengine na wakaingia katika mchakato wa uchaguzi, baadhi hawakutoka katika sekta nje ya utumishi wa umma tunafahamu ambao wametoka katika utumishi wa umma na bado wameendelea kutelekezwa miezi tisa kama wenzangu wamezungumza.

Mheshimiwa Naibu Spika, na hapa nina case study moja ya mtumishi ambaye alikuwa Mtendaji wa Kata Manispaa ya Kinondoni na baadae akawa DAS - Mbeya na baadae akaenda kugombea mpaka leo hajarudishwa katika utumishi wa umma. Tunaomba Serikali iwafikirie hawa ili tusiandae kundi kubwa la huko mbele ya safari ambao watakuwa ni wa kuipinga Serikali ambayo kwa kweli walihitumikia kwa uadilifu mkubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)