Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa kwa kunipa nafasi nichangie hoja ambayo hiko mbele yetu. Katika halmashauri ambayo inakusanya mapato mapato madogo ni Halmashauri ya Manispaa ya Lindi. Jana nilikuwa nasikia Mheshimiwa Zungu kwake anakusanya bilioni 60 lakini ukiangalia kwenye halmashauri yetu tunakusanya bilioni moja na milioni mia tatu tu Lindi Manispaa ina majimbo mawili na majimbo hayo yana changamoto kubwa sana. Kwa hiyo, ningeiomba Serikali kutusaidia kwasababu tayari tumeshaandika andiko mradi kwa ajili ya miradi ya kimkakati ya ujenzi wa soko kuu lakini ujenzi wa stendi kuu ya mabasi.

Mheshimiwa Spika, soko ambalo linatumika sasa lilijengwa tangia mwaka 1950 ni muda mrefu sana soko limekuwa chakavu mno, hata mapato yanayoingia kutoka katika soko lile ni mapato madogo sana tunakila namna ya kuona Serikali ni kwa namna gani mnaweza mkatusaidia halmashauri ya Manispaa ya Lindi kuhakikisha kwamba tunapata fedha za kuwekeza katika miradi hii ya kimkakati ili kuongeza mapato yetu ya halmashuri ili tuweze kuhudumia wananchi wa halmashauri.

Mheshimiwa Spika, suala la ujenzi wa barabara Waheshimiwa Wabunge wengi wameongelea suala zima la TARURA ninajua kwamba Serikali inaendelea kuboresha majiji miji pamoja na manispaa. Bahati mbaya sana miaka miwili mfululizo katika Manispaa ya Lindi hatujabahatika kupata fedha za kujenga barabara zetu.

Kwa hiyo, ninaiyomba Serikali itusaidie kuhakikisha kwamba kipindi hiki cha fedha tunapata fedha kwa ajili ya kuboresha Manispaa yetu ya Lindi na ukizingatia kwamba tuna changamoto kubwa za barabara na mvua zilizonyesha miaka miwili mfululizo ni mvua kubwa sana uharibifu mkubwa sana wa barabara upo katika maeneo yetu na barabara hizi kushindwa kutumika. kwa hiyo ninaiyomba Serikali iangalie katika hoja hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niongelee swala la Watendaji wetu wa Kata, watendaji hawa ndio wasimamizi wa shughuli za maendeleo katika kata zetu lakini ndio wanaosimamia kukusanya mapato yetu katika kata zetu. Kuna changamoto kubwa sana katika eneo hili, ninaiomba Serikali kuhakikisha kwamba tunaboresha ofisi zao za kata na ofisi hizi zilizokuwepo ambazo wanadandiadandia tu hata vifaa vya kufanyia kazi hawana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ninaomba sana Serikali kuhakikisha kwamba tunaboresha ofisi za Watendaji wa Kata lakini kuboresha vifaa vya kufanyia kazi ikiwemo pikipiki na vifaa vingine vya ofisi ili iwe rahisi wao kupita katika maeneo mbalimbali na kuhakikisha kwamba wanaendelea kukusanya mapato na Serikali tuendelee kupata mapato yetu ili tuweze kumudu kuwahudumia wananchi wetu katika maeneo yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo ninajua muda mdogo naunga mkono hoja ahsante sana. (Makofi/ Vigelegele)