Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ili nami niweze kuchangia mawazo yangu kwenye wizara hii muhimu ya Ofisi ya Rais TAMISEMI.

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nimpongeze Mheshimiwa Waziri Ummy Mwalimu na Manaibu wake pamoja na Katibu Mkuu na timu yake, niwapongeze hakika ni timu ya wachapakazi. Katika mchango wangu wa kwanza nitaongelea mfumo wa ukusanyaji mapato wa kielekroniki, kwa maana ya Local Government Revenue Correction Information system kwa ku-link na pos machines, ni mfumo ambao Serikali ilianzisha kwa nia njema ili kukuza mapato kwenye halmashauri zetu mwaka 2016. Umeenda kwenye processes mbalimbali ya kuziimarisha lakini bado naona kuna changamoto kubwa na gap ninayoiona kwenye huu mfumo ni namna ya ku-entertain collection ya physical cash.

Mheshimiwa Spika, dunia ya leo imeenda mbali sana, mambo ya physical cash yamepitwa na wakati, lazima tutafute namna mfumo huu utakuwa friendly tuanze kukusanya mapato yetu kwa kutumia soft money, na hii ndiyo maana unaona katika ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, halmashauri zetu walikusanya zaidi ya bilioni 18 na hazikwenda benki. Sasa kwa sababu ya ku-entertain cash, ndiyo maana unakuta bilioni 18 haziendi benki.

Mheshimiwa Spika, sasa nikushauri Mheshimiwa Waziri, kama itawapendeza, nendeni mkaupitie huu mfumo kwa undani zaidi, kwasababu umekuwa na loop holes nyingi. Mfano, anayeshika hii pos machine ni mtaalamu wa TEHAMA na huyo anauwezo wa ku-delete transaction, anapigiwa simu anaambiwa bwana hiyo haikuwa laki tano ilikuwa elfu tano na hii imepelekea kwenye Hesabu za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, bilioni nne zilifutwa. Sasa hizi bilioni nne zingeweza kufanya vitu vingapi kwa kuleta maendeleo kwa Watanzania!

Mheshimiwa Spika, na nionge with very serious note, kwenye halmashauri yangu zaidi ya milioni 400 zilitoka huko nje mpaka leo tunavutana na tunakaa tunang’ang’ana tuwapeleke polisi, tuwafunge tutawamaliza watendaji woote, wa kata na wa vijiji na wote wanaoshika pos machine, bila kuja na solution ya kuondoa physical cash tukawa na ile ambayo ni soft cash, tutawamaliza na hii defaulters itafutika, itakuwa historia tena mwaka huu mki-test, mtaona na kama mnataka muone cash management solution, nendeni kwenye benki watakupa, ni gharama ndogo tuna vijana wetu waliosomea IT watatupa ujuzi huu ni namna gani tunaweza kufanya cash management solution kwenye halmashauri zetu. (Makofi)

Mheshimiwa spika, kwa hiyo, nikuombe with due respect Mheshimiwa Waziri, nendeni mkaone namna ya kufanya jambo hili ni jambo jema sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia mchango wangu wa pili, naomba kuongelea mahusiano kati Wakurugenzi wa halmashauri, Madiwani na Wabunge.

Mheshimiwa Spika, nitaanza msemo mmoja kwa ruhusa yako ya kilatini, unasema Helius Beneficum cum servire regnire est maana yake ni kwamba, ni jambo jema sana na lenye baraka kuchagua wale ambao unawatumikia ni kutawala pamoja nao. Sisi wanasiasa tulivyoenda kuomba kura kwa wananchi wakiwepo Waheshimiwa Madiwani, Waheshimiwa Wabunge, tulichagua kuwatumikia, ambao kuwatumikia ni kutawala pamoja nao, lakini kuna baadhi ya halmashauri huu msemo umekuwa ni tofauti kabisa, na nitolee mfano wa halmashauri yangu.

Mheshimiwa Spika, nimebahatika kuhudhuria vikao vya finance mara mbili, nimekutana na mambo ya ajabu kabisa! Inafikia Mkurugenzi anasimama na kuwatukana Waheshimiwa Madiwani, anamtukana Mbunge, anaitukana Kamati za Hesabu za Serikali LAAC kwamba hawezi kumfanya kitu chochote, ameteuliwa na Rais, hii dharau ni ya kiwango cha juu haiwezi kuvumilika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na leo hii ninavyoongea Madiwani wangu walikuwa na kikao cha baraza la Madiwani wiki hii, Mkurugenzi kwa kujisikia tu akawaita anavyotaka, wao wameenda pale wanasubiri na hivi Kamati ya Usalama na Ulinzi iko pale kesho atafanya kikao, aje asije huko ndiyo tulikoenda.

Nikuombe sana Mheshimiwa Ummy ili uweze kutusaidia sisi hasa wananchi wa Jimbo la Kwela walituchaguwa wanataka wakaone tunavyo-deliver, tunavyowaletea maendeleo, hatuwezi kuwa na halmashauri ambayo ina mgogoro, Mkurugenzi ana kiburi, kama anafikia hatua ya kuweza kumtukana Mkuu wa Mkoa, anamtukana RC, anamtukana Mkuu wa Wilaya, kuna maisha hapo tena!

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, halmashauri imebaki kama kijiwe tu pale, na nikuombe, fedha ambazo umepeleka juzi, nililikufua sana mkatupelekea bilioni 2.5, kazifuatilieni fedha hizi za mradi kwa sababu pale kumebaki kama kijiweni with very serious note. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi sikuongea kwa hiyo, nilimwambia, mimi ninaenda kwenye platform yangu Bungeni nikaeleze na Tanzania nzima isikie, kwamba sitaki mchezo, wanananchi walinichaguwa na hili nimekuomba mama, tutakutana tena kwenye shilingi ya mshahara wako, ili nihakikishe limefanyiwa kazi, halmashauri yangu imerudi kati ya halmashauri ambazo zinaheshimika na Waheshimiwa Madiwani wapewe heshima yao. Hivi kweli mtu unaitukana Kamati ya Bunge, kwamba mimi niliteuliwa na Rais, mtu anayeweza kunioji ni Rais tu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na ninaomba kwa kweli tuangalie hata Walaka wa Mwaka 2011, mliwapa pawa sana wakurugenzi wakabaki kwenye loop hole ya ku-hang, mwishowe wanaanza matusi, kunidharau Mbunge, kumdharau Diwani, umedharau wananchi. Kwa hiyo, nikuombe sana, nimeongea kwa uchungu mkubwa, nadhani ndugu yangu Silinde wewe classmate wangu umenielewa, nimekueleza mara nyingi, Mkuu wa Mkoa ameleta barua nyingi RC, kumekaa kimya, nendeni mkainusuru Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niungane na wenzangu pia kuongelea jambo la TARURA, TARURA wameongea, sihami sana kwenye concept yao, twendeni tuka-review mgawanyo wa fedha hizi, huu mgawanyo umekuwa unfair! Baadhi ya halmashauri zina kilometa chache zinapewa triple au twice kuliko halmashauri zenye network kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, huu ni kuumiza wengine, kuna baadhi ya kata tangia watoe, halmashauri iache kuudumia barabara, wana maisha magumu, hawajawahi kuona hata greda. Nina Kata kama Mnangalua, Kata ya Mnokola, Kata ya Nankanga, Kata ya Kalambanzite, Kata ya Kaengesa, Kata ya Kanda, ninaweza nikazitaja kata hapa, wanalia, naombeni nendeni mka-review upya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuongeza fedha TARURA ni jambo la kwanza, lakini jambo la pili, wajitahidi kuhakikisha mgawanyo unakuwa fair kwa kila halmashauri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niombe pia nichangie kuhusu huduma ya afya, na hii ndugu yangu Silinde utakuwa unamnong’oneza hapo Mheshimiwa Waziri. Wewe tunatokea jirani pale na Tarafa yangu ya Kipeta ni jirani pale na wewe, ile Tarafa tangia uhuru haina kituo cha afya na ina wakazi wanakaribia laki moja, wala haina miundombinu yoyote ya maji, wao wako kama wapo jangwani, ni kama wana ambao wametelekezwa. Nikuombe sana, wamekuwa wakija pale Kamsamba napo huduma zinaenda kwa kusua sua kwa ndugu yangu Conchesta pale.

Mheshimiwa Spika, nikuombe sana, angalieni namna tutaanza kuisaidia hii Tarafa ya Kipeta, ipate kituo cha afya kwa haraka. Kwasababu maisha ya wananchi hawa ni hatari, juzi watu walikuwa wanakwenda pale kijijini kwenu Mkulwe, wameliwa wananchi 15 wamedumbukia kwenye mto, tumeishia kuzika wananchi wanafuata huduma ya afya huko ng’ambo. Nikuombe sana ndugu yangu tushirikiane kwa pamoja, tuhaikishe haya mambo yanaenda ili kuweza kuleta ufanisi ndani ya halmashauri yangu na Taifa la Tanzania kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, nilikuwa na hayo tu, niwaombe sana mkayafanyie kazi, hakika wananchi wangu wa Jimbo la Kwela na Waheshimiwa Madiwani wangu wao tu hawalii kilio tu cha stahiki, na kutukanwa matusi juu, na wamerudi nyuma, Mkuu wa Mkoa leo alikuwa ananipigia simu anasema, sasa tutaendaje Mheshimiwa Mbunge, nikasema hapana, wananchi walipanga mstari kutupigia kura, hili jambo lazima Serikali itatusikia na itafanya hatua ya haraka sana.

Mheshimiwa Spika, Ahsante sana. (Makofi)