Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kupata nafasi hii ya kuweza kuchangia kwenye Wizara hii nyeti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niende moja kwa moja niunge mkono hoja iliyoletwa mbele yetu leo na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.
Sote tunatambua Tanzania kuna uhaba mkubwa wa Walimu hususani kwenye masoma ya Mathematics na English. Tanzania hatuna Chuo cha Ualimu kinachoandaa Walimu wa English watakaofundisha shule za msingi. Maana yake kuna 100% lack of trained English Medium Primary School Teachers.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Teachers Colleges za Primary Schools zinafundisha kwa Kiswahili. Sasa changamoto inakuja kwamba, pamoja na kuwa Wizara ya Elimu inatambua mapungufu hayo hakuna coordination na Wizara zingine kama Wizara ya Kazi.
Wizara ya Kazi ina charge $500 kutoa class B work permit regardless wewe ni Mwalimu au ni Injinia wa Dangote Cement au Barrick Gold Mine. Kinachosikitisha zaidi, Wizara ya Mambo ya Ndani yaani Uhamiaji wao wanatoza $2000 fee ya resident permit kwa hawa Walimu ambao tunawahitaji sana. Hii fee imeongezwa kutoka $600 iliyokuwa wanatozwa mwanzo mpaka $2,000 kwa sasa na hii fee ya $2,000 ni kwa miaka miwili tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kweli Taifa letu linataka kusaidia watoto wetu, napenda nishauri yafuatayo:-
(i) Hizi fee zifutwe ili kuvutia kupata Walimu bora watakaoweza kufundisha vijana wetu; na
(ii) Tuwape support ya kutosha hawa ndugu zetu wenye private schools wakati Serikali yetu inaendelea kuboresha hizi government schools kwa sababu utafiti unaonyesha private schools ndizo zinatoa elimu bora zaidi kwa sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo, naomba maslahi ya Walimu wetu yaboreshwe ili kuwapa motisha ya wao kuendelea kuwasaidia vijana wetu. Pia tuhakikishe shule za msingi wanapewa madawati ya kutosha hususani Mkoa wangu wa Iringa watoto wetu bado wanakaa chini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja.