Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii niweze kuchangia Hotuba ya Waziri Mkuu. Kwanza kabisa nimshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehema ambaye ameniwezesha kusimama mbele yako, mbele ya Bunge Tukufu hili kuchangia Hotuba ya Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nianze kumpongeza Waziri Mkuu pamoja na timu yake kwa hotuba nzuri iliyojaa matumaini, iliyosheheni kila kitu. Naamini kabisa kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu ikienda kutekelezeka hii naamini kabisa kwamba, tayari sio hatuko kwenye uchumi wa kati, tuko kwenye uchumi wa juu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijikite kwenye suala zima la afya. Niipongeze Serikali yangu tukufu kwa kujenga vituo vya afya vingi nchini pamoja na zahanati. Ombi langu, hebu sasa Serikali ione namna gani itapeleka vifaa tiba na dawa katika hospitali zile ili, naamini kabisa Serikali ikishapeleka dawa na vifaa tiba naamini kabisa wananchi wetu watapata huduma stahiki na wataishi na afya njema. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niende kwenye tiba asili. Enzi za mababu zetu walikuwa wanatumia dawa hizi za asili, lakini mababu zetu wale walikuwa wanaishi miaka mingi sana tofauti na sasa. Kwa nini sasa sisi hatuwezi kuwaenzi mababu zetu kwa kutumia tiba zetu za asili?

Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii watu wanasema tunaenda kidigitali. Ushauri wangu niombe sasa tiba zetu za asili hizi zitumike. Mfano mzuri mwaka jana, nakumbuka ilikuwa mwezi wa tatu, Taifa letu lilikumbwa na ugonjwa wa corona, lakini Rais wetu Hayati Dkt. Magufuli alisimama kidedea na kutamka kwamba, taasisi za dini waombe misikitini pamoja na makanisani. Pamoja na hayo akasisitiza nyungu ziendelee na wale ambao wana fani zao za tiba za asili waendelee nazo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kweli ilifanyika vile, nadhani umeona mafanikio makubwa sana; hivyo basi, kwenye mpango huu, kwenye hotuba hii sijaona hata bajeti ya tiba ya asili. Nikuombe Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba, baada ya hotuba hiiā€¦

MHE. MARIAM D. MZUZURI: Mheshimiwa Naibu Spika, Taarifa.

T A A R I F A

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Shekilindi kuna Taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Mariam Ditopile.

MHE. MARIAM D. MZUZURI: Mheshimiwa Naibu Spika, nilipenda kumpa Taarifa muongeaji. Ni kweli kwa dhahiri tumeona mchango wa dawa za kienyeji kwenye kutibu gonjwa hili la Covid 19, hasa dawa ambayo yeye mwenyewe ndio ameibuni ya Shekilindi Bosnia Covid 19 Anti-Covid. Naomba nimpe Taarifa hiyo. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Shekilindi unaipokea Taarifa hiyo?

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, napokea Taarifa hiyo, lakini nataka nimwambie sio dawa za kienyeji ni tiba ya asili, tiba mbadala tiba ya asili. (Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niendelee kuchangia hususan katika suala hili. Dawa hii imefanya vizuri sana, imefanya vizuri kiasi kwamba, hata wataalamu wetu wa dawa hawa wa kisasa naamini wali-appreciate kwamba, dawa Hii ni safi na salama. Niombe sasa, huoni sasa umefikia wakati wa kupaisha dawa zetu? Huoni sasa umefikia wakati Serikali i-support watu wa tiba asili na tiba mbadala kwa ajili ya kunusuru Taifa letu? (Makofi)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa.

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, na nikuhakikishie dawa zetu hizi zinafanya vizuri, lakini nataka nikuhakikishie kwamba, wataalamu, watafiti nikiwemo mimi, tumegundua dawa zenye kutibu magonjwa mengi.

NAIBU SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa.

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Kwanza kabisa inatibu corona, inatibu UKIMWI, inatibu cancer, inatibu kisukari. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Asante sana. (Makofi)