Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii ya kuweza kuchangia hotuba ya bajeti Ofisi ya Waziri Mkuu, kwanza nianze kabisa kwa kuunga mkono hoja hotuba nzuri ambayo imewasilishwa na Waziri wetu Mkuu ambaye imetupa matumaini kwa kipindi kilichopita utekelezaji wake na kipindi ambacho tunachokwenda cha bajeti cha mwaka 2021/2022.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na pongezi hizi tunafahamu Serikali iliyoko inatekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi, na Ilani yetu imejipambanua vizuri sana, Ilani ya 2020 – 2025 yenye ukurasa 303 kwa vitendo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo langu la Igalula Serikali kupitia hotuba ya Waziri Mkuu imewasilisha ni jinsi gani imejali katika sekta ya afya. Na katika hotuba yake imesema kwa kipindi kilichopita wameweza kujenga zahanati zaidi ya elfu moja na mia moja na kidogo. Lakini vilevile wameweza kujenga vituo vya afya zaidi ya mia nne katika nchi nzima ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini katika Jimbo langu la Igalula, Jimbo lenye wakazi zaidi ya laki tatu waliopiga kura waliojiandikisha mwaka 2020 walikuwa zaidi ya laki moja na kidogo. Lakini Jimbo langu lina zahanati 17 tu ambazo zinatoa huduma kwa wananchi zaidi ya laki tatu, ukigawa uwiano wa zahanati hizo ni zaidi ya kila zahanati inaenda kuhudumia zaidi ya watu 20,000 ambayo kwa kuzingatia Ilani yetu ya Chama Cha Mapinduzi kufikia na kufikisha huduma bora kwa wananchi wetu si sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Jimbo la Igalula ni waungwana sana wamekuwa wakiibua miradi mbalimbali ikiwemo miradi ya zahanati na shule. Na wamekuwa wakijitolea sana kwa kuwa wao ndio wanaona ndio vipaumbele vyao. Nilipochaguliwa na wananchi wa Jimbo la Igalula nimefaya ziara katika vijiji takribani 30 kati ya 58 kuangalia nini mahitaji yao na kila nilipokwenda wanahitaji shule na zahanati. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia hotuba ya Waziri wetu Mkuu ambayo amewasilisha katika Bunge hili. Niiombe Serikali, juzi wakati tunachangia mpango wakati wa majumuisho Mhehimiwa Ummy Mwalimu alisema mwaka huu atajielekeza katika kutatua na kuweka vifaa tiba katika vituo vyetu vya afya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hilo ni jambo jema zaidi, lakini niwakumbushe kuna maboma mengi ambayo yameibuliwa na wananchi wanahitaji yamalizike. Tukisema twende tukupeleke kwenye vifaa tiba kwenye kituo cha afya kimoja katika jimbo la Igalula hatuwasaidii wana Igalula. Leo hii aliyekuwa Waziri wa Ofisi ya Rais, nani hii Jafo, alikuja katika Kata ya Igalula, aliwakuta wananchi wamechangia kwa nguvu zao wodi ya mama na mtoto akavutiwa na uwekezaji ule na juhudi zile aliweza kutupatia fedha na sasa tumejenga kituo cha afya kilichopo katika Kata ya Igalula. Niwaambie kituo cha afya kimekamilika tangu mwaka 2019 mpaka leo hakijaanza kazi. Sasa lengo la Serikali ni kuongeza huduma kwa wananchi na si kuua huduma kwa wananchi. (Makofi)

Meshimiwa Naibu Spika, wameweka vigezo, kulikuwa kuna zahanati jirani wanasema tuhamishe vifaa tupeleke kwenye kituo cha afya sijajua hayo maelekezo yanatoka huku juu au wenyewe maamuzi yao. Lengo la kuongeza vifaa, vitoa huduma ni lengo la kuwasaidia wananchi, haiwezekani palikuwa na zanahati na tunasema tuna zahanati elfu moja na ushee pamoja na ile zahanati halafu unakwenda kuiua, unasema vile vifaa tuhamishie kwenye vituo vya afya, hata ukiangalia mwongozo wa afya, vifaa vya kwenye zahanati na kituo cha afya ni vitu viwili tofauti.

Mheshimiwa Spika, niiombe Serikali kupitia kituo chetu cha afya katika Kata ya Igalula tupate vifaa tiba na ile zahanati iendelee kuwepo na wananchi waendelee kupata huduma. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna maboma ambayo Serikali imeomba tuwasilishe kupitia halmashauri zetu. Niombe yale maboma yote ambayo yapo katika hatua ya umaliziaji na ni nguvu ya wananchi watu wengine, wananchi wengine baadhi ya kata na vijiji wamejenga zaidi ya miaka sita, mingine miaka minne mitano, wakiwa wanapita pale wanaangalia nguvu zao zimepotea basi Serikali kupitia bajeti hii iweze kuweka fedha ya kwenda kumalizia yale maboma ikiwemo maboma ya zahanati na shule, hivi hivi niombe Serikali iweze kutusaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna suala la miundombinu juzi wakati wanachangia hapa Wabunge wenzangu kuna mbunge mmoja alisema yeye katika Mkoa wa Dar es Salaam haitaji kilimo kwasababu hana eneo la kulima. Alisema anahitaji barabara ili aweze wanachi wake waende kutafuta kipato warudi nyumbani wakiwa salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wangu wanahitaji miundombinu ya barabara, barabara zetu za vijijini tofauti na za Dar es Salaam. Barabara zetu za vijijini wanahitaji kiwango cha changarawe ili ziweze kupitika muda wote. Tukija kwenye masuala ya sekta nitachangia zaidi kutokana na muda niseme tu itoshe ninaunga mkono hoja hotuba ya Waziri Mkuu. (Makofi)