Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Juliana Didas Masaburi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. JULIANA D. MASABURI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi hii niweze kuchangia hotuba hii ya Mheshimiwa Waziri Mkuu. Sote tunafahamu kwamba kuna ongezeko kubwa sana nchini la mashine za kamari almaarufu kama beting za kachina na mashine hizi zinafungwa sana kwenye mikusanyiko ya masokoni, kwenye vituo vya daladala, vituo vya taksi bajaji na bodaboda. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mashine hizi za kamari sasa hivi zinaingizwa hapa nchini kama spear parts na zinakuja kuwa-assembled hapa hapa nchini kwa hiyo, nina wasiwasi kwamba TRA haina idadi Kamili za mashine hizi za kamari ambazo zipo nchini. Hii inawezesha TRA kukosa mapato yake kihalali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mashine hizi za kamari zipo hapa nchini kwenye maduka mpaka ya Mangi ambazo TRA kule kwenye maduka ya Mangi hawana ofisi zake. Kwa hiyo, inashindwa kuhakiki na inashindwa kukusanya kodi zake ipasavyo ninaushauri kwa Serikali kwenye suala hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba Serikali ifanye uhakiki upya wa kutoa leseni kwenye mashine hizi za kamari leseni kwa mashine moja moja mashine moja inapewa leseni moja hii itasaidia Serikali kupata idadi kamili za mashine zilizopo lakini na kukusanya kodi yake ipasavyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sote tunajua kama kamari ni kitu haramu na baadhi ya nchi haziruhusiwi kabisa lakini naomba kushauri Serikali pia kuweka sheria kali ambazo zitamlinda kijana zitamlinda mtoto mwanafunzi siyo tu wanavyosema kuanzia miaka 18, ningeshauri Serikali iweke hata kuanzia miaka 25 kwasababu kijana wa miaka 18 bado hajaweza kujipambanua na wanaingia kwenye huu mtego wa kamari hizi tunaenda kupoteza nguvu kazi ya Taifa. Unakuta mwanafunzi sasa hivi haendi darasani anatoka nyumbani anaenda shule lakini anaishia hapo katikati kwenye kucheza hizi kamari. Kwa hiyo, naomba Serikali iliangalie hili suala kwa umakini zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama Serikali itaona kuna haja ya kuendeleza hii kamari za mtaani lakini haikusanyi kodi yake ipasavyo. Kwa mwezi TRA inawatoza hawa wafanyabiashara ya kamali shilingi 100,000 lakini wao kwa siku wanafunga Sh.300,000 mpaka shilingi 700,000 na kwa mwezi wanafunga shilingi 9,000,000 mpaka Sh.21,000,000. Napenda kuishauri Serikali iangalie suala hili kwa makini zaidi, kwanza ni vitu ambavyo vinaenda kuharibu vizazi vyetu huko nje, kwa hiyo, kama kodi wa wachatozwe kodi kweli kweli. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, yangu ni hayo, naunga mkono hoja. (Makofi)