Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, private secondary schools wasifanye mchujo wa watoto kwa maana ya slow learners. Private schools wameweka pass mark yao tofauti na Serikali. Huanza mchujo kuanzia kidato cha pili hadi form IV terms za mwanzo. Hata kama watoto wakifikia kiwango cha “pass mark” ya Serikali kama hajavuka cha shule wanazosoma (private) huondolewa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo lao matokeo ya mwisho final exams results wapate division I wengi na division II wachache basi, hawataki division III, IV na 0. Wanataka soko la shule zao liwe juu kwamba wanafaulisha sana. Huu ni unyanyasaji na ubaguzi wa hali ya juu, ukemewe kwa nguvu zote. Binadamu tumepishana, wengine fast learners na wengine slow learners lakini wote uelewa wao ni sawa. Ni mbaya sana inaleta pia usumbufu kwa wazazi, huitwa na kuambiwa mhamishe mtoto wako kwa vile hataweza ku-cope na wenzake. Hii ni mbaya, mbaya kabisa.