Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. VINCENT P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, kwanza napenda niipongeze sana hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa sababu, imesheheni sehemu zote imegusa nyanja zote. Mimi nikiwa kama Mbunge wa Jimbo la Nkansi Kusini pia ni Mbunge wa Nkasi, Wilaya ya Nkasi, napenda kujikita katika upande wa kilimo kwa sababu sisi tunaotokea Rukwa, Nyanda za Juu Kusini, tusipoongelea kilimo ni shida. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Wabunge wengi wameongelea suala la kilimo humu, napenda kuwaambia hivi wameongea wengi kuhusu utafiti, wako sahihi, lakini wanaenda kutafiti nini? Kilimo ambacho wanasema wakulima wanalima wanazalisha mazao ya aina ipi? Ni quantity au quality? Wengi wamesema South Africa imeteka zao la Kongo, Zambia, sawa; tunaweza kuwa tunalima lakini tunalima mazao je, yana ushindani kwenye soko? Mbegu hizi ambazo tunawaambia watafiti waende wakatafiti, je, watakuwa wanaotafiti wana nia njema na kutuletea mbegu zilizo bora ambazo zitaleta ushindani kwenye soko? Au ndio hao wanaokuja kusema kama bwawa la umeme halifai? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tutafute watu sahihi. Mbegu zinazofaa ni aina gani ya mahindi ambayo inauzwa kwenye soko, sio bora tu kuzalisha. Kwa hiyo, unakuta Tanzania inazalisha mazao mengi, lakini mahindi yanayolimwa ni bora? Ndio yanayohitajika kwenye soko huko kwenye soko la kimataifa? Nchi Jirani zinahitaji aina ya mahindi hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunaweza tukawa tunalima mahindi, lakini sio bora kwenye soko hayapo na watafiti wakatuletea tu bora kuzalisha mahindi. Lakini ningependa hizi Wizara tatu hizi ni Wizara pacha. Wizara ya mambo ya Nje, Wizara ya Kilimo, Viwanda na Biashara hizi zinatakiwa ziende pamoja, lakini sijui kama wanakaa pamoja ili waone namna ya kuinua kilimo kwa ajili ya kuinua Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Mambo ya Nje ya Nchi inatakiwa ikae itafute masoko kule ituletee jamani Sudan wanahitaji mahindi aina fulani, kwa hiyo kwenye utafiti tuleteeni mbegu wakulima wa Wilaya ya Nkasi kusini, Rukwa, Kigoma na Njombe walime aina fulani ya mbegu ndio tutakidhi kwenye soko la kitaifa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kilimo, tunakuja kwenye suala la pembejeo, pembejeo imekuwa ni shida ni aibu mwaka huu watu wamepata hasara wakulima ambao wamejitahidi wamekuja watu feki katikati hapa wanaleta mbolea ambazo sizo hazina tija, sasa sijui kama Wizara inayorudi itatuletea majibu wale walioleta mbegu feki zingine zinatoka nje zingine zinaenda wapi, wakulima wamepata hasara kubwa mno wanatakiwa hao watu wachukuliwe hatua, wewe - imagine mkulima anatoa fedha zake anatembea kilometa 60 - 70 kumbe anakwenda kubeba mbolea feki, mbegu feki na Wizara ipo sio sahihi.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika hii speed ambayo ni legacy ya mheshimiwa Rais Hayati John Pombe Joseph Magufuli, Rais hakuweza kuyafanya haya peke yake Rais ni taasisi ambayo ipo ndani Mheshimiwa Mama Samia yupo Mheshimiwa Hayati Magufuli yupo Mheshimiwa Naibu Spika upo Wabunge wote ni legacy ya Chama Cha Mapinduzi, mendeleo yote haya yanaletwa na Chama Cha Mapinduzi pamoja na legacy ya Waheshimiwa hawa wote kwasababu ni tasisi walikuwa wanaungana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli asingeweza vyote hivi bila kuungana na Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mheshimiwa Mama Samia kwahiyo mtu anayekuja kutaka kubeza nawaomba Waheshimiwa Wabunge kwa umoja wetu tunaamini hawa ni asilimia ndogo sana hawawezi kutushinda sisi kama tulivyo kuweza kufuta legacy ya Mheshimiwa Rais ili waweze kufuta legacy ya Mheshimiwa Mama Samia Suluhu ni jembe ni mtekelezaji yeye ndiye alikuwa ni mtendaji yeye ndiye alikuwa front line pamoja na Waziri Mkuu. Hivyo hasi kama wanajaribu kubeza… (Makofi)

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, naomba kumpa taarifa.

NAIBU SPIKA: Ngoja Mheshimiwa Sophia nitakupa fursa, subiri.

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, haya Ahsante.

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge kanuni zetu zinataka mtu akiwa anazungumza ndio anapewa taarifa lakini mzungumzaji haachi kuzungumza mpaka niwe nimemwita wa taarifa unatakiwa uendelee kuchangia mpaka nimpe fursa huyo anayesema taarifa.

MHE. VINCENT P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, hongera sana.

NAIBU SPIKA: Sasa nikupe nafasi Mheshimiwa Mwakagenda japo kuwa mwanzoni ulisema mwongozo, mwongozo pia hauruhusiwi kuombwa wakati kuna mtu anazungumza, mtu akiwa anazungumza unaweza kuomba vitu viwili moja ni taarifa cha pili utaratibu kama kuna kanuni inavunjwa, Mheshimiwa Sophia Mwakagenda.

T A A R I F A

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante tunaendelea kujifunza bado nashukuru kwa kunielewesha, naomba nimpe taarifa mzungumzaji anayeongea kwamba sasa hivi tunazungumzia Wizara ya Waziri Mkuu tunaichangia hiyo na kutoa maoni yetu, na hakuna mtu yeyote hapa ndani ya Bunge ambaye hataki maendeleo ya Taifa hili. Kwa hiyo, nataka ajielekeze zaidi kwenye hotuba na kuweza kuijadili hiyo sote tunataka Tanzania iliyo bora, ahsante. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Vincent Mbogo unaipokea taarifa hiyo.

MHE. VINCENT P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, siipokei yeye jana ameisifia Standard gauge amemsifia Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa hiyo legacy bado inaendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana napenda nijikite tena kwenye upande wa Kilimo, kilimo upande wetu kimekuwa kwenye hali ngumu kutokana na hizi Wizara tatu…

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

MHE. VINCENT P. MBOGO: …hizi Wizara tatu zingeweza kujikita kwa pamoja, moja isiteleze… …(Makofi)

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mbogo kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Ngassa.

T A A R I F A

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante napenda kumpa taarifa mzungumzaji Mheshimiwa Mbogo hiyo Stigler’s Gorge anayoiongelea ndio ile Waziri wa Nishati amesema itawekewa maji tarehe 15 Mwezi 11 ahsante. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Vincent Mbogo unaipokea taarifa hiyo.

MHE. VINCENT P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, naipokea kwa mikono miwili ahsante sana. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Sekunde tano malizia mchango wako.

MHE. VINCENT P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana napenda kwenda kujikita kwenye upande wa uvuvi ziwa Tanganyika, ziwa lile bado halijatumika ipasavyo ukanda ule mapato yanapotea wavuvi wanakwenda kuvua nchi za jirani hawaji kuvua huku kwasababu ya mazingira sio rafiki na tozo, tozo ni nyingi mno mazingira sio rafiki na wavuvi, mabwawa yote, maziwa yote hata nchi za jirani kwa Tanzania nzima. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Bahari ya Hindi wanaziwa wanavulia Mombasa, ziwa Tanganyika wanakwenda Kongo, Burundi kwahiyo tunapoteza mapato, naomba Wizara ikija hapa ijikite namna ya kutengeneza mazingira rafiki itakavyoweza kuwarudisha wavuvi tuweze kupata mapato Tanzania. Pamoja Wizara ya uvuvi itenge maeneo ya uwekezaji ijenge uvuvi, ahsante sana. (Makofi)