Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Mchango wangu utajikita katika sekta binafsi ambavyo zimechangia katika uchumi au katika pato la Taifa. Ukiangalia tathmini ya mpango wa pili wa miaka mitano unaokwisha imeeleza bayana kwamba, sekta binafsi haijafanya vizuri kwamba, mchango wako ni chini ya asilimia 50.

Mheshimiwa Naibu Spika, na ninataka nioneshe masikitiko yangu kwasababu sisi leo sio nchi tena ya ujamaa kwa hiyo, tunahitaji sekta binafsi iweze kuchangia, ili tuweze kuona mabadiliko katika uchumi wa nchi hii. Na ukiongelea sekta binafsi ni pana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tukiongelea leo, wengi wakisimama hapa wanaongelea kilimo…

MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE: Mheshimiwa Naibu Spika, Taarifa.

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: …kama kilimo kinafanya vizuri, kilimo ni sekta binafsi.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Anatropia Theonest kuna Taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Charles Mwijage.

T A A R I F A

MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda nimpe taarifa mzungumzaji. Tanzania ni nchi inayofuata siasa za ujamaa na kujitegemea. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Anatropia Theonest nunapokea taarifa hiyo?

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Sijui bado kuna nafasi za uteuzi au? (Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ninaelewa mchango wa sekta binafsi kama tukiandaa mazingira mazuri ya watu binafsi, ya wafanyabiashara kufanya kazi katika mazingira wezeshi wataweza kuchangia sana katika uchumi wa nchi yetu. Nimeainisha kuna baadhi ya changamoto nyingi ambazo huwa tunaziongea hapa na zote zinafahamika zinazoikuta sekta binafsi.

Mheshimiwa Naibu Spika, mfano mlolongo wa tozo, tozo ni nyingi kila mmoja anajua. Tunakuja usumbufu na mlolongo wa kupata vibali, kila mmoja anajua sitaki kueleza, lakini ambacho nataka nongelee specific ni upatikanaji wa mikopo. Sekta binafsi itawezaje kufanya biashara au kujiendesha bila mikopo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna changamoto ya riba kubwa ya mikopo, nilikuwa napitia Taarifa ya BOT katika mwaka wa 2027 walifanya review ya riba za benki na wakawashushia kutoka asilimia walizokuwa wanatoa, leo wako asilimia 12, tisa mpaka asilimia tano kwa mwaka 2020 review ya mikopo ambayo wanapata, lakini ukienda kwenye benki specific wananchi wafanyabiashara wakienda kuchukua mikopo wanachukua kwa shilingi ngapi? Huwezi kupata hata kwa asilimia 11. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe mfano mwingine wa kawaida; wataeleza sababu za kuweka riba kubwa waseme risk ni kubwa. Nimesoma pia kwenye ripoti anasema mikopo chechefu imeanza kupungua imetoka asilimia 11.6 imeenda mpaka asilimia 11.1 japo projection BOT wanasema ifike mpaka asilimia 5. Ni kwa nini tunakuwa na mikopo chechefu?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu riba zinakuwa juu. Watu wanakopa fedha, biashara ni ngumu, automatic wata-default. Niiombe BOT niombe kuangalia au ku-review sera yake ya fedha kuangalia namna ambavyo watawalazimisha mabenki waweze kushusha riba. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitatoa mfano mwingine, na-declare interest, ni Mbunge na mnufaika wa mikopo, lakini mfano benki zikiwakopesha Wabunge, Wabunge ambao wana mishahara mikopo yao inakatwa automatic. Yani resk ya ku-default kwa watumishi au watu walioajiriwa ni ndogo kwa nini riba hazishuki? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ni lazima hili suala tuliangalie kama tunataka ku-favor sekta binafsi ziweze kufanya vizuri, ziweze ku-access mikopo na ni lazima mikopo iweze kushuka riba. Otherwise watakuwa wanachukua fedha benki wanafanya kazi za kwenda kusaidia benki na sio kuweza kupata kipato. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini changamoto nyingine, changamoto ya vitambulisho vya NIDA. Ukienda kama mfano wilaya ninayotokea mimi, kuna mtu aliongeaongea hapa nataka nimpe taarifa; Kyerwa ninyi leo tumepata Rais wa Tanzania Kyerwa walikuwa tayari na Rais mwanamke kwa hiyo, Kyerwa wana Marais wawili wa Tanzania, mmoja Mama Samia mwingine sio mwingine ni mimi na yeye anajua. (Makofi)

MBUNGE FULANI: Hoyo hoyo!

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nikiongelea changamoto ya vitambulisho vya NIDA naihusianisha…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Anatropia, ngoja tuelewane vizuri. Ulikuwa unagombea ubunge ama urais, ili tuelewe ni urais gani unaouzungumzia?

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa nagombea ubunge. Sasa ubunge ukishafikia level kubwa wanakuita Rais, yaani unakuwa Mbunge Rais. Rais wa jimbo. (Makofi)

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Naibu Spika, Taarifa.

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nimeeleza changamoto ya NIDA. Naeleza changamoto ya NIDA…

NAIBU SPIKA: Kuna Taarifa Mheshimiwa Anatropia. Mheshimiwa Innocent Bilakwate.

T A A R I F A

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kunipa nafasi nimpe Taarifa Mchangiaji anayeendelea, Mbunge wa Jimbo la Kyerwa anaitwa Innocent Sebba Bilakwate na Mbunge huyu alimzidi huyo mchangaiji kura 15,943. Kwa hiyo, nampa Taarifa Mbunge anayetambulika ni Innocent Sebba Bilakwate, yeye ni wa kupewa tu. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Aanatropia Theonest unaipokea Taarifa kutoka kwa Mbunge wa Kyerwa?

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niendelee. Ukiona mtu anajaribu kuji-justify anajua hajiamini na ha-deserve. (Makofi)

WABUNGE FULANI: Hoyo hoyo hoyo!

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, naongelea changamoto ya NIDA nikihusianisha na vikwazo wanavyopata sekta sekta binafsi. Na nitaongelea specific Kyerwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na nieleze nitakuja hapa nitatumia kanuni kuomba nitoe maelezo binafsi ya Mbunge juu ya changamoto ya watu wa Kyerwa ya ukosefu wa vitambulisho vya NIDA. Hawawezi kupata mikopo kwasababu, ukienda kujaza fomu ni lazima uweke namba ya kitambulisho cha NIDA. Hawawezi kupata bima za afya, wale watu wanafanyaje? Na ile ni mikoa ambayo inapatikana mpakani kila siku unaambiwa wewe ni raia, wewe sio raia; hapo unafanyaje biashara katika mazingira hayo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niombe Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kuwa, ni msimamizi wa jumla aiangalie Kyerwa kwa jicho la upekee hasa suala la vitambulisho vya NIDA. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tukitoka hapa nitaeleza kitu kingine. Leo kila mmoja mwenye simu tulioko humu ndani kama kuna server inaweza ikawekwa hapa unaweza ukafanya tathmini ni watu wangapi wanafanya miamala. Leo miamala ya fedha haifanyiki kama luxury, sio starehe, ni biashara. Watu wanafanya biashara, tuko ndani hapa biashara inaendelea, lakini tukirudi kwenye swali bank charges za hiyo miamala ya fedha ni kiasi gani? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, amekuwa analisemea mara nyingi sana. Kwamba, nikitumia simu yangu nimefanya muamala hapa, sija-consume, sijatumia huduma yoyote ya benki wala mtumishi ni kwa nini nakatwa fedha nyingi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hiyo pia ipo kwenye miamala ya simu. Nimesoma kwenye ripoti ya BOT wamesema hivi, kwenye sera yao wamesema, kuna miamala takribani wamesema milioni 145 ambayo imefanyika katika interval tofauti ikihusisha amount zaidi ya five billion, lakini pia imehusisha watu zaidi ya milioni 22, unaona kwamba, ni idadi kubwa ya watu wanafanya biashara ya mitandao ya simu. Kwa hiyo, niiombe Serikali, nimuombe Waziri Mkuu kuangalia namna gani wanaweza kushusha zile charges za simu ili watu wengi waweze kufanya biashara ili iweze kupunguza gharama ya ufanyaji wa biashara. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimekuwa mara nyingi nikiongelea hapa ninasema hivi kama Taifa tumekuwa tukitumia new industrialized nation kama modal. Zile tiger nations kama modal ambazo zimejikwamua kutoka kwenye nchi za ulimwengu wa tatu kuwa ulimwengu wa pili na leo ni nchi zilizoendelea, sisi kama Tanzania tumekuwa tukifanya nini? Miradi mingi ambayo tumekuwa tukiifanya ni kiradi isiyogusa watu wengi, ameeleza Mbunge mmoja hapa, lakini pia modal tunazozitumia ni sahihi?

Mheshimiwa Naibu Spika, humu ndani kulikuwepo na sera wakati fulani wanasema sasa ni kilimo kwanza, wana magari yako branded kila kitu kilimo kwanza, lakini leo tunasema viwanda. Hivi kuna viwanda bila kilimo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani nataraji nione nguvu kubwa ikiwekezwa kwenye kilimo, lakini kwenye taarifa ambayo amewasilisha kwenye mpango aliowasilisha Waziri wa Fedha ameeleza kwamba, kilimo kimeshuka. Tena nimesoma kitu ambacho kimenisikitisha amesema hivi, ameeleza kwamba, kilimo kimeshuka kwasababu sitaweza kuiona kwa haraka, kimeshuka kwasababu watu wamewaza alternative; yaani watu wameamua kuwekeza kwenye vitu vingine, lakini hii nchi leo zaidi ya watu asilimia 80 wana-rely kwenye kilimo. Ina maana kama tunashindwa kuwezesha kilimo na viwanda itakuwa ni mjadala tu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nisipoongelea kahawa kwa watu wa Kyerwa hawatanielewa. Hii ni zaidi ya mara 15 na katika mijadala yangu nitaongelea kahawa. Ninaongelea kahawa kwasababu, kuna shida, kungekuwa hakuna tatizo nisingeongelea kahawa; bado kuna changamoto ya soko bado kuna changamoto ya vyama vya ushirika. Na hapa nitamgusa ambaye anahusika na uwekezaji na hiyo niseme ni changamoto nimesoma kwenye bajeti Fungu Namba 11 lililoanzishwa kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji limetengewa bilioni 7 ambayo wamesema ni asilimia 0.02 kwenye bajeti kuu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunataka leo twende kwenye uchumi wa kati sasa, sio kati chini, lakini Wizara au fungu la uwekezaji bado lina bajeti ndogo. Nadhani hata kamati wameeleza, wameeleza vizuri kabisa kwamba, hili fungu liwekewe hata fedha ya maendeleo, hilo fungu liwezeshwe ili liweze kufanya kazi nzuri. Kama tunataka kwenda kwenye uchumi wa kati tunavyofika 2025 basi hayo maneno yawe reflected kwenye vitendo. Kwenye vitendo sio kuongea hap ani fedha iende na ionekane ikiwa inaenda. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mwisho kabisa japo sio kwa umuhimu ni kuwashukuru ndugu zangu. Mungu awabariki, karibu Kyerwa baba. (Makofi/Kicheko)