Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutoa mchango wangu kwa maandishi ili na mimi niweze kushauri Serikali katika kuboresha sekta hii muhimu ya elimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Wizara ya Elimu itoe fursa kwa watu binafsi wenye uwezo kuwekeza katika elimu ya ufundi VETA. Hii itasaidia kuipunguzia mzigo Serikali unaotokana na ufinyu wa bajeti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mimba za wanafunzi, Wizara ilete Muswada Bungeni utakaoonesha jinsi ya kuwabana na kuwawajibisha wale wanaohusika na mimba hizo. Pia Serikali iweke mtaala maalum kwa wasichana wanaozalia shuleni ili tusije wapa haki ya kusoma na kujikuta tunakandamiza haki ya watoto waliozaliwa mfano haki ya kunyonya, kuwa karibu na wazazi lakini pia tusijeleta mzigo mkubwa wa kulea kwa bibi watakaokuwa wakilea watoto hao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tujitahidi kutoa motisha kwa Walimu ili kuwapa morali katika utendaji kazi wao. Natoa mifano michache ya baadhi ya Walimu niliokutana nao katika Wilaya ya Kyerwa kwenye moja ya ziara zangu. Walimu hawa walipandishwa vyeo miaka miwili iliyopita lakini mpaka leo hawajaongezewa mishahara. Nafahamu changamoto ya bajeti inayoikabili Serikali yetu ila nashauri tusiwapelekee barua za kuwapandisha vyeo kama hatuna uhakika na malipo yao. Baadhi ya Walimu hao ni kama ifuatavyo:-
(1) Rutaihwa Kazoba
(2) Geofrey Kamondo
(3) Rugeiyamu Damian
(4) Selestine Tibanyendera Ishengoma
(5) Erick Twesige Anacleth
(6) Philbert Jeremiah Kazoba
(7) Tabu Herman
(8) Ndyamukama Cylidion
(9) Heavenlight Baguma
(10) Frida Buyoga
(11) Onesmo Alphonce
(12) Philbert Kinyamaishwa
(13) Diomedes Kajungu
(14) Yohatam Samwel
(15) Diomedes Kajungu
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema awali hao ni baadhi ya Walimu waliopo katika Wilaya ya Kyerwa ambao nilipofanya ziara yangu ya kiutendaji niligundua hao na wengine wengi ambao majina yao sijayataja wamepandishwa vyeo kwa takribani miaka miwili sasa na mpaka leo hawajaongezwa mishahara. Naomba Mheshimiwa Waziri ufuatilie matatizo haya katika Wilaya ya Kyerwa na upatapo nafasi naomba unijibu hoja zangu hizi kwa maandishi ili niweze kupeleka mrejesho kwao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, napenda kumwomba Waziri ashirikiane na Wizara ya TAMISEMI ili kuweza kusukuma vipaumbele ambavyo kimsingi Wizara hii mnakutana navyo moja kwa moja katika kutekeleza Sera ya Elimu nchini. Nakutakia kila la kheri katika kutekeleza majukumu yako, ahsante.