Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua nafasi hii kumpongeza Waziri, Mheshimiwa Profesa Ndalichako na Naibu wake Mheshimiwa Stella Manyanya kwa kazi nzuri zinazofanywa. Nawapongeza pia kwa kushirikiana na watendaji, wameandaa taarifa ambayo inaleta matumaini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni wazi kuwa aspect ya quantity tumefanikiwa sana na sasa tujielekeze kwenye aspect ya quality. Serikali iwekeze kwenye kuboresha namna tendo la kujifunza na ujifunzaji linavyotaka kwa kuangalia upya idadi ya wanafunzi kwa elimu ya msingi kwani wanafunzi 45 ni wengi ibadilike iwe 35; Walimu wapewe motisha ili waongeze morali; vifaa na vitabu vya kufundishia vipatikane na kuongeza idadi ya Walimu wanaopata mafunzo kazini kwa kutumia vituo vya walimu vilivyopo TRCS.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kitengo cha Udhibiti wa Ubora wa Shule (Wakaguzi wa Shule). Kitengo hiki kipewe fedha za kutosha ili waweze kukagua shule nyingi. Wadhibiti ubora wapewe mafunzo ya mara kwa mara na nyenzo za kufanyia kazi. Vilevile idadi ya shule zimeongezeka muundo wa Wadhibiti Ubora wa Elimu urekebishwe badala ya kuwa kwenye kanda wawepo kimkoa na kuwe na mawasiliano na Katibu Tawala wa Mkoa (RAS).
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
172
Mheshimiwa Mwenyekiti, ada elekezi. Nashauri Serikali ijielekeze kwenye hoja za wananchi wengi, tuboreshe shule zetu na wananchi wataacha kupeleka watoto shule binafsi. Hali hiyo ikifikiwa wamiliki wa shule watapunguza ada kwa kufuata nguvu ya soko. Serikali ijikite katika kuboresha elimu katika ngazi zote na si vinginevyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.