Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kuniona na kunipa fursa hii nichangie kwenye mjadala huu.

Mheshimiwa Spika, nianze kwanza kabisa kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais wetu Samia Suluhu Hassan kwa jinsi ambavyo ameanza kazi yake vizuri, amerejesha amani na matumaini mapya kwa watu wengi. Lakini pia kwa kuzingatia kwamba ametuambia tunaendeleza yale yaliyoanzishwa chini ya uongozi wa Mheshimiwa Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, na tunaamini pia kwamba kwa jinsi ambavyo tunmfahamu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, ataongeza hata ile kasi ambayo tunaipokea.

Mheshimiwa Spika, nataka niseme kwamba kielelezo kikubwa cha kuonesha kwamba kweli Mheshimiwa Rais wetu anatekeleza kama anavyoahidi ni timu ya Mawaziri aliyoweka kumsaidia yeye, akiwemo Mheshimiwa Waziri Mkuu ambaye amekuwa ni kichocheo kikubwa na naamini kwamba ataendelea na kasi ileile, ataendelea kumsaidia Mheshimiwa Rais kwa namna hiyo lakini pia na Mheshimiwa Makamu wa Rais aliyechaguliwa, naamini wote ni watu poa kabisa, siyo poa, ni bomba kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo naamini tukiangalia timu iliyopo mtu anapokwenda kwenye kiwanja cha mpira unaangalia kwamba amebeba timu gani na yeye ameingia kwenye uwanja huu akiwa amebeba timu ya Yanga au ya Simba? Ya Yanga tuseme, lakini itabadilika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nataka niseme hivi; nampongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa uwasilishaji wake mzuri, wa kina na unaoeleweka, ripoti ambayo imeandaliwa kweli kitaalam na ina-cover kila kitu ambacho mtu unataka kuona. Lakini nimpongeze zaidi kwa jinsi ambavyo amesimamia shughuli za Serikali kwa miaka hii yote ya Awamu ya Tano na mwaka huu ambao tumeanza na jinsi ambavyo amejitoa kutembea kwenye maeneo mbalimbali, na nina matumaini kwamba kule kuona kwake kumesaidia sana kusukuma utekelezaji wa miradi na mikakati ambayo ilikuwa imewekwa mbele yake.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka nimpongeze na niseme kwamba tunaamini na mimi naamini kwamba hatasahau kutembelea Vunjo. Na ninaamini pia kwamba Mheshimiwa Rais kule Vunjo hatujaona viongozi wa kitaifa wa kubwa kwa miaka mingi, takribani miaka saba – naamini tutaanza kuwaona pia kule wajue kwamba kule pia sisi CCM tumejipanga vizuri na tumejipanga kwa safu ambayo italeta maendeleo kwa jimbo letu sana sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakupongeza wewe na Naibu Spika kwa jinsi ambavyo mnatuweka pamoja na kutupa fursa na kujua ni yupi aseme saa ngapi na kadhalika. Nawapongeza sana, naamini naona ufahari sana.

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kusema kwamba huu utani wa darasa la saba na maprofesa siyo mzuri sana. Kule nilikotoka mtu anajulikana kwa kazi na umuhimu wake na wote tuna kazi moja ya Ubunge, hatujuani kwa elimu tulizonazo na elimu tulizonazo hazina maana yoyote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunapofika hapa tupeane heshima kwamba wewe uko darasa la saba au gumbaru umetoka huko we don’t care unajua kusoma na unaweza kuchangia vitu vizuri. Naamini kwamba sisi kila mtu ana nafasi yake lakini tusianze kuingiza utani, utani huo ni mzuri lakini, hasa Mheshimiwa Musukuma akiwepo…

SPIKA: Haya, sasa endelea na hoja Mheshimiwa Dkt. Kimei.

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Endelea na hoja iliyopo Mezani.

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, niache Mheshimiwa.

SPIKA: Ukiwachokoza nawajua hawa, endelea tu Mheshimiwa Dkt. Kimei. Ukiwachokoza darasa la saba utatafuta mlango wa kupitia.

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, nawafahamu, nawafahamu sana. Nawafahamu na ninawapenda sana lakini…

SPIKA: Maana yuko Rafiki yangu mmoja, Mheshimiwa Dkt. Mwakyembe, alikosa kuona mlango wa kupitia baada ya kuwagusa darasa la saba. Ndiyo maana nasita, usije ukawagusa huko Vnjo watakuvunja mguu, endelea tu na hoja ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, darasa la saba waache.

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Niseme hivi; kuna jambo moja ambalo linatakiwa liangaliwe kwa ujumla, hasa kwenye hii nyanja ambayo inahusiana na mambo ya uajiri wa wafanyakazi serikalini na kadhalika. Ni suala zima la kutathmini skimu ya mishahara ili kuiweka bayana ili mtu kama ni profesa atake kukaa kwenye uprofesa wake. Lakini ukweli ni kwamba mtu anafuata pale penye maslahi, lakini kuna wengine tunakuja hapa kwa sababu tunataka kutekeleza mambo fulani fulani kwenye maeneo yetu.

Mheshimiwa Spika, na ninataka kusema kwamba ninashauri kwamba skimu ya mishahara iangaliwe ili stadi zile ambazo ni rare professions na kadhalika na ambao tunataka wabaki kule kwenye specialties zao waweze kufanya utafiti, walete innovation, wasaidie nchi hii kwenda forward professionally, tuweze kuwabakiza kule zaidi kuliko kuwatoa na kuwaleta kwenye siasa na kuwavutia kwa sababu huku kuna maslahi mazuri mengine, lakini naamini kwamba tutaangalia hili ili mambo yawe vizuri zaidi na watu wakae kwenye professions. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninataka kuchangia kwenye maeneo matatu; eneo la kwanza kabisa ni eneo la utawla bora, utawala bora unaendana na span of control. Sasa imekuwa kwamba kuna halmashauri nyingine ambazo ni kubwa sana, zinaweza zisiwe kubwa sana kwa maeneo lakini kwa wingi wa watu.

Mheshimiwa Spika, sasa kama halmashauri ni kubwa sana, zaidi ya watu laki tatu, inakuwa ni ngumu sana kusema kweli halmashauri ile kutenda kwa kuwafikia watu ambao tunataka tuwafikie kwa karibu, tuwapelekee elimu ya uwezeshaji na tuwasaidie kwa kuwaonesha kwa vitendo. Lazima halmashauri hizi zinagaliwe ili kama zinaweza zikapangwa kivingine zipangwe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, namshukuru Mheshimiwa Rais Hayati wetu, mpendwa wetu, JPM, alipokuja kwetu alisema kwa mfano tuwe na Halmashauri ya Himo, alikubaliana na hilo. Na ninaamini kwasababu naunga mkono mambo mengi nasema Mungu atujalie na Mheshimiwa Rais wetu mpya, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan aweze kukubali pia twende na Halmashauri yetu ya Vunjo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pili, nataka nizungumzie suala la Kamati ya UKIMWI kudhibiti UKIMWI. Naomba hii ijiongeze kidogo na kuhusu la gonjwa la COVID, ninaomba hii Kamati iingize masuala hayo kwenye mchakato wake ili tuweze kujua tunapoendelea huko mbele na tuweze kudhibiti, siyo tu UKIMWI, kwasababu UKIMWI naamini tumeshaanza kuu-contain na mtu ambaye kweli amejipeleka hovyohovyo natumaini ni... lakini ukweli UKIMWI kwenye rate ya three to five percent siyo mbaya, at least tunaweza tukadhibiti. Lakini naamini kwenye magojwa haya mapya yanayojitokeza, hasa COVID, pia tuangalie.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hayo, niseme kwamba kwenye suala zima la COVID Private Sector Foundation ilitoa mchango wake, ilifanya utafiti wkae kuhusiana na athari na ninaamini kwambs Serikali itaendelea kusoma na kuona mapendekezo gani yalifanyika hususan kwenye sekta ya utalii, kwamba sekta ya utalii iliathirika sana na ukiwaambia kwamba walipe tozo zile walizokuwa walipe NGOs fees ambazo ni fixed, waendelee kulipa wakati hawajawa na watalii, zitakufa. Hawataweza kuendelea. Kwa hiyo, tukasema kwamba wale waangaliwe kwa namba yao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na siyo sekta ya utalii tu, na sekta nyingine pia zimeathirika lakini ile ripoti najua ilikuja Serikalini na tunaomba kwamba Serikali iisome tena ione kama inaweza ikaitumia ili kuweza kupunguza makali ya gonjwa hili. Kama kwetu halipo limekuwa nje kwa hiyo, limeathiri wale wateja wet, na kadhalika. Lakini nataka kusema kwamba ni lazima tuangalie namna ya kusaidia watu.

Mheshimiwa Spika, suala la uwezeshaji. Uwezeshaji naamini kila Mbunge hapa amejipanga kwa namna moja kwasababu hii miundombinu tunayoijenga haitakuwa na maana kama haitatumiwa kuzalisha, na ndiyo sababu moja nasema lazima tuangalie kwamba tumejenga barabara, ni kitu gani kimetokea hapo kwenye barabara.

Mheshimiwa Spika, kulikuwa na Central Corridor Programme ambayo ilikuwa isaidie ku-develop vitu fulani fulani along the central corridor ya railway na ile railway baadaye iweze kuwa na tija zaidi na watu wengi wanavutiwa na jambo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, uwezeshaji ni jambo la msingi lakini kuna masuala ambayo lazima tuyaangalie. Kwanza ishu ya finance kama alivyosema mwenznagu, kwamba mtaji ni kitu kikubwa. Sasa mitaji tunayotegemea, kwa mfano ukiwa kwenye halmashauri, haijawa revolving fund, mtu anachukua mkopo lakini ukiuliza ni mingapi imerejeshwa kwenye halmashauri wale waliokopa utakuta kwamba urejeshaji ni very low.

Mheshimiwa Spika, ndiyo sababu inakuwa kila mwaka lazima uingize hela mpya na ukiuliza leo hela ya kukopesha ni ngapi watakwambia ni ile waliyopokea mwaka huu, hawakwambii ukichanganya na ile ambayo tumekopesha mwaka jana ikarudi na hii ambayo leo imetolewa tunaweza tukakopesha mara tano, haijatokea namna hiyo.

Mheshimiwa Spika, ni kwasababu kuna weakness kwenye level ya halmashauri kutoa ile mikopo, ile mikopo inatolewa na watu ambao kwanza ni wale maafisa maendeleo wako wachache, hawana staff wa ku-follow up, hawashirikishi sana watu wa kwenye vijiji. Kwa hiyo, ikiwa kama mtu amechukua mkopo ijulikane anatumia kwa njia ya uzalishaji na kadhalika, kwa hiyo inatokea kwamba yule mtu anayechukua hela hawezi hata kuitumia vizuri na anakuwa hajaandaliwa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naamini kwamba ni vizuri hizi hela halmashauri…

SPIKA: Ahsante Mheshimiwa Dkt. Kimei, tunakushukuru sana.

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)