Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, nikushukuru wewe binafsi, lakini katika mambo ambayo Watanzania hawatamsahau Hayati Magufuli ni pamoja na mapinduzi makubwa ya fikra. Yapo mambo tunayosema yanaonekana kwa kuona, lakini jambo kubwa ni mapinduzi ya fikra za Watanzania. Ndio maana come rain come fire, kamwe hatuwezi kuwabadilisha Watanzania vile wanavyomwamini Hayati Dkt. Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nieleze kwa habari ya mapato. Tunapozungumzia utelekelezaji wa miradi ya maedeleo ni lazima tuangalie pia suala zima la mapato, suala la mapato ni jambo mtambuka na sio kazi peke yake ya Wizara ya Fedha na TRA. Naomba nieleze hapa ili tuone namna gani tunaweza kupata fedha kwa ajili ya miradi yetu ya maendeleo. Wengi tunasema barabara, maji, umeme, kama tutasimamia vizuri na kama tutakusanya vizuri mapato, kamwe hatufanikiwa; nazungumzia suala mtambuka maana yake nini.

Mheshimiwa Spika, Wizara za kisekta zina jukumu kubwa sana kufikiri tofauti kuongeza tax base ya Taifa. Ninavyozungumzia tax base nazungumzia wigo wa mapato ili tuondokane na mazoea ya vyanzo vilevile tulivyovizoea. Mathalani unavyoongeza tija kwenye sekta ya kilimo maana yake utaongeza tax base, unavyoongeza tija kwenye viwanda na biashara unaongeza tax base, unavyoongeza tija kwenye utalii utaongeza tax base na kwa kuwa nina nafasi ya kuchangia wakati tunachambua hizi Wizara moja baada ya nyingine nitaeleza kwa undani zaidi.

Mheshimiwa Spika, eneo linguine, jambo kubwa lingine kubwa ambalo Hayati Dkt. Magufuli ambalo amelifanya ndani ya Taifa letu ni kuhamisha kwa vitengo Makao Makuu ya Nchi kuhamia Dodoma. Labda tu Waheshimiwa Wabunge nieleze kwa ufupi ya harakati za kuhamishia Serikali Dodoma. Mnamo mwaka 1966 aliyekuwa mdogo wake Hayati baba wa Taifa, Joseph Nyerere alipeleka Muswada Bungeni wakati huo wa kuitangaza Dodoma kuwa Makao ya Nchi, lakini baadaye Mkutano Mkuu wa TANU mwaka 1973 uliamua rasmi sasa Makao Makuu ya Serikali yawe Dodoma. Lakini zipo jitihada zilizofanyika na hayati Baba wa Taifa, pamoja na kuanzisha Wizara ya Ustawishaji wa Makao Makuu mwaka 1973 ambayo Waziri wake wa kwanza alikuwa Adam Sappi Mkwawa, Retired Speaker wakati huo akisaidiwa na Sir George Kahama kama Director General wa CDA.

Mheshimiwa Spika, na walifanya kazi kubwa sana; unavyioiona Area C ya leo, unavyoiona Area D ya leo, unavyoioana Uzunguni ya leo, ni kazi ya Adam Sappi Mkwawa na Sir George Kahama wakiongoza Wizara ya Ustawishaji wa Makao Makuu ya Nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo hili limechukua muda, baadaye akaja mzee Samuel Sitta, hatimaye mama Anna Abdallah alihudumu kama Waziri na baadaye mchakato uliendelea kwa sabbau ya changamoto ya vita mwaka 1978/1979 ya Nduli Idd Amin, kidogo political will ya kuhamisha Serikali ilipungua kwasabbau uchumi wa nchi yetu ulipita katika kipindi kigumu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, amekuja kutimiza ndoto za Hayati Baba wa Taifa. Leo hii sisi wote Wabunge tuliomo humu ndani ni wadau wa Makao Makuu ya Nchi. Na yapo mambo makubwa yamefanywa na Serikali ya Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Hayati sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo hii unavyoitazama Dodoma, angalia sekta ya barabara, sekta ya afya, miundombinu mbalimbali, unaiona Dodoma kwa kweli ni makao makuu kwelikweli. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini naomba nishauri jambo kwasababu Mheshimiwa Rais wetu mpendwa wa sasa wa Serikali ya Awamu ya Sita, mama yetu Samia Suluhu Hassan –na ndiyo maana kauli mbiu yake inasema kazi iendelee. Maana yake pale alipoishia Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli yeye sasa anaendeleza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa misingi hiyohiyo, leo hii kama siyo mashahidi hapa Waheshimiwa Wabunge, tumeanza kupata changamoto sasa hapa Dodoma za huduma mbalimbali, hasa huduma ya maji, ukienda umeme kidogo na maeneo mengine. Naomba nishaui Serikali; changamoto hii inaletwa na changamoto kubwa ya uratibu wa namna ya kujenga Makao Makuu ya Nchi.

Mheshimiwa Spika, leo hii utaona watu wa RUWASA wana bajeti yao, watu wa TARURA wana bajetyi yao, Jiji la Dodoma lina bajeti yake. Kwa hiyo, taasisi zote hizi za Serikali kila mmoja anapanga kivyake. TANROADS naye ana mipango yake, hatuwezi kutoka, hatuwezi kusogea. Na ndiyo maana leo hii utaona huna wa kumuuliza.

Mheshimiwa Spika, sasa ushauri wnagu, changamoto hii ya uratibu wa makao makuu ya nchi, nishauri jambo ikiipendeza Serikali, kwa kuwa Mheshimiwa Rais wetu aliyepo sasa anaendeleza kazi iliyoachwa na Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, ushauri wangu; ni lazima tuwe na chombo cha uratibu kinachoweza kuzifanya taasisi hizi zote za Serikali zizungumze pamoja. Kazi ni ndogo sana, zizingumze pamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa mfano, unapozungumzia suala la umeme, pamoja na uwepo wa Jiji la Dodoma, chombo hiki kitakutanisha taasisi zote hizi za Serikali hapa Dodoma, na kazi yake ni kuratibu. Sasa inategemea vile Serikai itakavyoona inafaaa.

Mheshimiwa Spika, kwa mfano wenzetu Uganda. Ukienda Uganda wana chombo ambacho wanakiita Ministry for Kampala Capital City na Waziri wake wa sasa anaitwa Bi. Betty Amongi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukienda Nairobi wenzetyu wana Nairobi Metropolitan Ministry ambayo Waziri wake wa sasa anaitwa Bw. Kamau, lengo kubwa hapa ni kufanya – na hakuna gharama, naomba nishauri Serikali – hakuna gharama ya uendeshaji wa chombo hiki, ni uratibu. Kinachoongezeka ni hawa watu kwenye chombo lakini bado taasisi zinaratibiwa kwa bajeti zao isipokuwa sasa chombo hiki kinafanya hizi taasisi zote zizungumze lugha moja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kinyume cha hapo, wakati wangunikiwa Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma tuliweza kufanya yale tuliyoyafanya. Unajua, niseme tu mtakuja kuyaona haya baadaye. Tuliona mambo yanakwenda vizuri, siyo bure, utashi wa mtu katika utendaji wa Serikali hauwezi kuwa sustainable. Na ndiyo maana nashauri hili, tuwe na mfumo mzuri kwa ajili ya kuhakikisha kweli tunakwenda kujenga Makao Makuu ya Nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika,baada ya kusema hayo, naomba nimpe elimu kidogo dada yangu, Mheshimiwa Mbunge wa Nkasi, maana mtoto akichezea wembe muache umkate. Alivyokuwa anasema Serikali anasahau kwamba kuna sheria ya asilimia 4.4.2 iliyopitishwa hapa Bungeni. Unavyosema vijana wapewe asilimia kumi zote determinant…

Mheshimiwa Spika, kumradhi, determinant…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ya pili tayari Mheshimiwa, nakushukuru sana.

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Lakini kwa Habari…

SPIKA: Ahsante sana; dakika kumi ni chache.

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, siyo mbaya naunga mkono hoja. (Makofi)