Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia uzima kuweza kusimama tena ndani ya Bunge lako tukufu.

Mheshimiwa Spika, nitachangia mambo machache kulingana na umuhimu wenyewe wa Wizara, Ofisi ya Waziri Mkuu, lakini mambo mengine ninaweza kushauri kwenye Wizara nyingine za kisekta..

Mheshimiwa Spika, nitaanza na suala la ajira, sote tunajua kwamba, suala la ajira bado ni changamoto kubwa sana kwenye Taifa letu. Tukitazama wahitimu wa kada mbalimbali kwa mwaka na idadi ya ajira zinazotolewa ni vitu viwili tofauti, lakini pamoja na kwamba, Serikali imekuwa na mikakati mbalimbali namna ya kuwasaidia vijana, imekuja na Habari ya Mfuko wa Vijana bado haijaweza kumaliza changamoto hiyo.

Mheshimiwa Spika, lakini pamoja na mfuko uliopo ambao uko chini ya TAMISEMI ambao unazungumzia asilimia 4 kwa vijana, asilimia 4 kwa wanawake na asilimia 2 kwa watu wenye ulemavu ni vizuri suala hilo likaangaliwa upya. Najua kuanza hatua moja inatufanya turudi na turekebishe makosa yetu.

Mheshimiwa Spika, kwanza changamoto inaanzia kwenye asilimia mbili ya watu wenye ulemavu. Watu wenye ulemavu wako wa aina tofauti na hapa kumekuwa na shida sana kwenye hili jambo. Kwa kuwa, Wizara hii pamoja na kwamba, tulipitisha hiyo asilimia 2 ni vizuri tukaangalia sera yetu kwasababu, lengo ni kuwasaidia watu wenye ulemavu na lengo ni kuwasaidia vijana pamoja na wanawake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitakuwa na ushauri kidogo, leo tuna VETA na tuna vyuo vya ufundi, wale watu wakishamaliza pale wamepewa knowledge shida yao inakuwa ni suala la capital. Na kwasababu, kumekuwa na changamoto kwa vijana wengi ambao wanamaliza vyuo hawana uwezo wowote wa kwenda kufanya biashara wa kwenda kufanya jambo lolote kwa hiyo, inakuwa ni changamoto kurudisha ile fedha ambayo wamekopa. Ni kweli wanajikusanya huko wanaona namna gani ambayo wanaweza wakajisaidia ili wakakope, wanakopeshwa. Kurudisha fedha ile inakuwa ni ngumu, lakini hali tukiangalia halmashauri zetu ni mbaya sasa hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu ni nini kwenye jambo hili; wale watu wanaokuwa wamemaliza vyuo vya ufundi au waliotoka VETA tayari wamepewa ujuzi na ninazungumza leo ni kwa mara ya tatu ndani ya Bunge. Wale watu wakipewa mkopo na tutoke kwenye asilimia 4 tufikiri zaidi ikiwezekana vijana peke yake wapewe asilimia 10. Lengo ni kwamba, kwasababu, wameshapewa ujuzi wakienda kule kwasababu wana uwezo wa kujiajiri wao wenyewe wanaajiri vijana wengine kupitia kazi ambazo wamezifanya. Kutakuwa na tija na lengo ambalo tulikuwa tunafikiri kuwa-empower vijana wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini hata wanawake. Wanawake sasa wamejitoa wameamua kuingia kwenye ujasiriamali na shughuli mbalimbali, tukizungumzia asilimia 4 ni wanawake wangapi ambao wanapewa huo mkopo?

Mheshimiwa Spika, na kwa bahati mbaya hata hiyo asilimia 4 kuna halmashauri zinashindwa kuwapa wanawake kwa sababu ya hali iliyopo kwenye halmashauri zetu. Kwa hiyo, ni vizuri ikiwezekana itoke TAMISEMI tukaona namna bora ambavyo tunaweza ku-control jambo hili, ili tuweze kuwasaidia wanawake ambao tuliwalenga pamoja na vijana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitakuja kidogo kwenye kilimo kwasababu, nitakuja kluchangia kwenye Wizara ya Kilimo. Tunapozungumzia uwekezaji, tunapozungumzia viwanda, tunapozungumzia uchumi wa kati huwezi kuacha sekta ya kilimo Tanzania kuizungumzia ili kufikia uchumi wa kati. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo nitazungumzia palepale ambapo nazungumza kila siku, ili kuboresha kilimo chetu na kiwe kilimo chenye tija lazima tuwekeze kwenye utafiti. Nategemea leo tunapozungumzia kilimo cha Tanzania cha kwanza tuangalie vyuo vyetu vya utafiti viko vingapi, lakini tunapeleka fedha kiasi gani? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo hata tukija na njia mbadala kwamba, tunahitaji mazao ambayo yatakuwa labda mbadala wa mahindi, kwa mfano Nyanda za Juu Kusini. Kabla ya kufanya hivyo mmefanya utafiti kiasi gani wa udongo? Mmefanya utafiti kiasi gani juu ya mbegu ambazo zinapelekwa kwa ajili ya kilimo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa mbadala wa mahindi kwa mfano nyanda za Juu Kusini kabla ya kufanya hivyo mmefanya utafiti kiasi gani wa udogo, mmefanya utafiti kiasi gani juu ya mbegu ambazo zinapelekwa kwa ajili ya kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, natambua kwamba mwaka uliopita ni asilimia 20 tu ya mbegu bora ambazo zilipelekwa kwa wakulima wetu. Ukipeleka mbegu ambazo si bora kwa hali ya kawaida unategemea mazao yake yatakuwaje? Kama tutawekeza kwenye utafiti lazima pia tutatafiti ni zao gani ambazo linaweza likasaidia Taifa, ni zao gani ambalo linaweza kupandwa kulingana na aina ya udongo ambayo tumepata majibu kutoka kwa watafiti.

Mheshimiwa Spika, kuna kitu kinaendelea cha mazoea sana, ukiangalia kwenye shina moja labda nitolee mfano zao la mahindi, wanachukua kile kifuniko cha maji au kisoda wanapimia mbolea wanaweka pale, nani alifanya utafiti kwamba lile tundu linafaa kwa kile kizibo kimoja kuweka mbole? Lakini wananchi wengi wanatumia ni kwasababu ukiangalia hata Maafisa wa ugani wetu ni wangapi wanafika kule kwa wakulima wetu kuwapa elimu na kwamba wamefanya utafiti ni kiasi gani kinafaa kutumika kwenye shina moja la mahindi.

Mheshimiwa Spika, bado ninarudi Ofisi ya Waziri Mkuu. Pamoja na kwamba Wizara zote zinaweza kuzungumzia kulingana na sekta zao ni vizuri kuangalia uchumi wa kati wa Taifa hili tunaenda kuangalia kwenye vitu gani? Leo tunazungumzia uchumi wa kati ukienda kwa Mtanzania mmoja mmoja wa chini kabisa kwa mfano kule Nkasi ukimwambia tupo kwenye uchumi wa kati atakushangaa uchumi wa kati upo wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunataka hii hali Mheshimiwa Waziri Mkuu hizi takwimu ambazo tunasoma kwenye vitabu zikaonekane kwa wananchi moja kwa moja kwenye uhalisia wa maisha yao ya kila siku na hapa tutakuwa tunazungumzia lugha moja. Ni kweli kwamba yawezekana wataalam wetu wanatuambia hivyo, lakini nataka uhalisia.

Mheshimiwa Spika, kwa hali ya kawaida hata mimi Aida ukiniambia kwamba uchumi wa kati, bado najiuliza uchumi wa kati ninaangalia nini? Vigezo gani ambavyo naviona kwangu kwamba kweli tumefikia kwenye uchumi wa kati. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wakati nataka kwenda kuzungumzia habari ya Tume Huru nataka nimkumbushe Mheshimiwa Waziri Mkuu, pamoja na kwamba nimezungumza mara kadhaa…

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, taarifa.

T A A R I F A

SPIKA: Mheshimiwa Getere

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, Ahsante naomba nimpe taarifa Mbunge ya Nkasi, anasema uchumi wa kati umekujaje aende akaangalie vigezo vya IMF na World Bank, kwamba uchumi wa kati unapatikana kwa capital income per capital income na GDP; kwa hiyo angalia tu hivyo vigezo mama utajua kwamba vinaendaje Mheshimiwa Mbunge. (Makofi)

SPIKA: Taarifa hiyo unaipokea Mheshimiwa Aida.

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, naomba niendelee. Sisi hatujazoea kukaririshwa tumezoea kuona na kuyaishi maisha yenyewe ya uchumi wa kati; kwa hiyo hatuwezi kuelewana lugha zipo tofauti kidogo.

Mheshimiwa Spika, naomba niendelee kumkumbusha Mheshimiwa Waziri Mkuu kwamba tumekuwa na ahadi ya muda mrefu kuhusu suala la MV Liemba kwenye ziwa Tanganyika. Ni vizuri wakati unahitimisha; kumekuwa na kelele nyingi kwamba yawezekana wale watu wamejitoa, sijui mkataba umefanya nini, ni vizuri mkaja hapa mkatueleza hatua ya MV Liemba imefikia wapi na nini kinaendelea ili na sisi tupate kujua watu tunaotokea kwenye Ziwa Tanganyika.

Mheshimiwa Spika, kwasababu ya muda naomba nizungumzie Tume Huru ya Uchaguzi, Fungu la 61. Miongoni mwa Wabunge wa CHADEMA waliotangazwa ni mimi hapa kupitia Tume hii iliyopo sasa hivi, natambua hilo. Lakini pamoja na kutambua kwamba nilitangazwa si kwamba nilikuwa Mgombea bora kuliko wagombea wengine wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), lakini ni miongoni mwa wale wachache, au mimi niliyepenya kwenye tundu la sindano. Naomba nizungumze mambo machache kwa ajili ya Taifa letu, kwa nia njema kabisa,. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunapozungumzia Tume Huru ya Uchaguzi tulianza na mchakato wa kutaka Katiba mpya ambayo ilikuwa ni maoni yetu. Natambua kwamba yalitokea yaliyotokea, lakini pamoja na hayo mlifikia hatua kubwa sana ya Katiba mpya. Ndiyo maana leo tunasema kwakuwa kelele ni nyingi na tunahitaji umoja wa Taifa letu tuangalie vipengele ambavyo bado vinashida, hasa kwenye eneo la Tume Huru ya Uchaguzi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, natambua kwamba Tume Huru ya Uchaguzi tukisema tuongeze idadi ya watu kuna gharama ya fedha, lakini kama lengo ni kuponya taifa ni vizuri tukazungumza.

Mheshimiwa Spika, wapo baadhi ya Wakurugenzi ambao sheria imekataza kabisa kwamba Msimamizi wa Uchaguzi hatakiwi kuwa kiongozi wa Chama cha Siasa, lakini sote tunajua wapo Wakurugenzi ambao walikuwa viongozi wa vyama vya siasa.

Mheshimiwa Spika, lakini hata ningekuwa mimi leo nimepewa ukurugenzi kila mtu alikuwa anajua Aida ni kada wa CHADEMA katika wagombea wa Chama cha Mapinduzi lazima nitalinda maslahi ya chama changu, na lengo ni jema tu. Naomba nitolee mfano mdogo tu wa kama yangu alikuwa Mkurugenzi hapa Dodoma, alikuwa mkurugenzi Dodoma amekwenda Jimbo la Mlimba Mheshimiwa Kunambi…

SPIKA: Unamchokoza. (Makofi)

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, aaah! nimesema ni mfano, na nia ni njema tu alikuwa Makao Makuu pale kila mtu anajua.

Mheshimiwa Spika, lakini kwa hali ya kawaida yaani ukiangalia suala hili ambalo nataka kuzungumza Mheshimiwa Waziri Mkuu kuanzia mchakato wa awali habari ya watu kunyang’anywa fomu, habari ya watu fomu zao zina matatizo. Msimamizi wa Uchaguzi hakai pale kwa ajili ya kuvizia nani amekosea kwenye fomu yake anatakiwa awepo pale kumwelekeza mgombea kwamba hapa unatakiwa kufanya hivi, ufanye hivi Uchaguzi wa mwaka 2020…

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, taarifa.

T A A R I F A

SPIKA: Taarifa, iko wapi taarifa, Nimekuona Mheshimiwa Kunambi.

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, Hakuna mashaka na Tume yetu ya Uchaguzi. Na labda nimueleze tu kama Tume yetu ya Uchaguzi isingekuwa Tume ya kutenda haki yeye asingekuwepo hapa. Nimpe tu taarifa kwamba Tume yetu ya Uchaguzi inazingatia misingi ya demokrasia. Naomba kuwasilisha. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana, Aida muda wako umekwisha, dakika moja tu ili uweze kupokea taarifa.

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, kaka yangu Mheshimiwa Kunambi anatakiwa kujua kwamba mimi sikupita bila kupingwa hilo la kwanza ajue…

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

MHE. AIDA J, KHENANI: ….lakini la pili…

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

MHE. AIDA J. KHENANI: … nataka nitoe ushauri kwenye jambo hili…

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, taarifa nipo huku…

SPIKA: Mheshimiwa Musukuma taarifa.

T A A R I F A

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na mimi nazidi kumweleza mchangiaji kwamba, ni kweli hatuna mashaka na Tume ya Uchaguzi na imetenda haki na mfano mzuri huko Kilimanjaro Mheshimiwa Anna Mghwira ni ACT, lakini tumewapiga, kwa hiyo naomba waondoe mashaka na Tume yetu. (Makofi)

SPIKA: Pokea taarifa.

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, taarifa

SPIKA: Hajajibu hamuwezi kumpa taarifa juu ya taarifa

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Ayayayaaa!

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, kwanza napenda nimwambie kaka yangu Musukuma kwamba Mheshimiwa Anna Mghwira sio ACT ni CCM lakini, tafakari ninayoiacha ninapohitimisha kila Mbunge aliyekuwa humu ndani anajua alishinda, kama alishinda alishinda kwa namna gani, ahsante. (Makofi)

SPIKA: Tatizo lenu, nikusaidieni, mimi huwa ninakaa nawasikiliza habari ya tume huru lakini hata siku moja hajawahi kusimama mtu akasema hiyo tume huru mnayosema nyinyi inafananaje? Mnasema neno Tume huru tume huru kwani iliyoko hapa sio huru…

MHE. AIDA J. KHENANI: (Alizungumza bila kutumia kipaza sauti)