Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

Hon. Abdullah Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mahonda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. ningependa kuanza mchango wangu kwa kutoa salamu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, hivi karibuni tumepoteza Rais wetu, amefariki Rais wetu wakati yeye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Jambo hili halina rejea ndani ya nchi yetu katika historia ya nchi yetu na si jambo jepesi kwa Rais kufariki katika nchi changa kama hii ambayo wapinzani wetu wanasema hatuna mfumo wa utawala bora, lakini amefariki Rais.

Ningependa kutoa shukrani zangu za dhati kabisa kwa Serikali pamoja na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kwa kuhakikisha Katiba na mfumo mzima wa utawala bora unasimamiwa na hali yetu mpaka Rais wetu mwingine aliyekuja akashika wadhifa bila matatizo yoyote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nchi nyingi wamepata changamoto kama hizi na ikasababisha machafuko. Hili si bure, haya ni ukomavu wetu wa Serikali yetu chini ya Chama chetu Cha Mapinduzi ambayo imewezesha utaratibu na kuonesha dunia nzima kwamba, sisi ni wakomavu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimeupitia mpango pamoja na kusikiliza hotuba za hivi karibuni za Mheshimiwa Rais. Na mambo ya msingi ambayo ningependa kuyachangia ni matatu, la kwanza ukimsikiliza Mheshimiwa Rais vipaumbele vyake ni vitatu cha kwanza ni kurekebisha mfumo wa biashara. La pili ni kuimarisha zaidi mahusiano kikanda na ya kimataifa na cha tatu ni kuhakikisha miradi yetu ya mkakati inakamilika. Hayo mambo mawili ya mwanzo yakifanyika vizuri ndio yatahakikisha hili jambo la tatu, miradi ya mkakati, itakamilika kwa salama na amani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa kwasababu muda si rafiki mimi ningependa kugusia suala la kwanza kuboresha mfumo wa biashara. Ukiungalia mpango mzima na section kubwa ya kuhusu business environment utaambiwa tumepitia kitu kinaitwa blue print; kila uki-question jamani tumefika wapi, tunafanya nini, blue print implementation imefika wapi?

Mheshimiwa Spika, utaambiwa ikikamilika mambo yote hayo unayoya-raise yatakuwa sawa. Sasa wenzangu humu ndani ya Bunge walilizungumzia suala la monitoring na evaluation. Ili tuweze kurekebisha yale matatizo tuliyokuwanayo lazima tuwe na taasisi rasmi ama hapa Bungeni chini ya kamati moja au Serikalini na sehemu bora zaidi ni chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwasababu, yeye ndio kiongozi wetu katika shughuli za kila siku za Serikali. Lazima tuwe na taasisi ambayo inahakikisha quarterly tunafanya monitoring na evaluation kwa yale ambayo tumeyapanga. Bila kuboresha mfumo mzima wa kibiashara revenue hazitakuja zile ambazo tunategemea, biashara haitakua, uwekezaji hautaendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa sehemu hii ni sehemu ambayo ni nyeti sana ambayo ningependa kuunga hoja za miongoni mwa wenzetu ambao wamezungumzia kwamba, ama tufanye sehemu mbili Bunge liwe lina-monitor pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu kuhakikisha kwamba, yale ya
kimkakati, reforms tangible kwasababu, kuna projects ambazo unaona kama kitu kimejengwa hakijajengwa, lakini kuna mfumo wenyewe inabidi ubadilishwe uwe rafiki zaidi kwa ajili ya kukaribisha uwekezaji. Kwa hayo machache ningependa kushukuru kwa fursa hii na napenda kuunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)