Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

Hon. Eng. Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi hii ya kuchangia Mpango wa Tatu wa Maendeleo kwa Miaka Mitano wa Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, leo nitachangia vitu vikubwa viwili, na kwa kuanzia nitaanza na suala zima la monitoring and evaluation yaani ufuatiliaji na tathmini. Nimejaribu kusoma Mpango wa Tatu wa Maendeleo, umeeleza vizuri sana kwamba Mpango wa Pili wa Maendeleo haukutekelezwa ipasavyo. Na miongoni mwa sababu kuu ni kwa sababu hakukuweko na mpango Madhubuti wa ufuatiliaji na tathmini. Na imeelezwa pia mpango wa pili ulichelewa kuanza, umeanza miaka miwili baadaye.

Mheshimiwa Spika, lakini Mpango wa Tatu pia umeeleza kwamba idara mbalimbali za Serikali Kuu na Serikali za Mitaa zilitengeneza namna zao zenyewe za kufanya tathmini na ufuatiliaji bila kufuata mipango yetu mizuri iende kufanya kazi na kuleta matunda tarajiwa. Ni lazima tujipange vizuri katika ufuatiliaji na tathmini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukiangalia nchi zetu za jirani, South Africa ina taasisi maalum ya tathmini na ufuatiliaji ndani ya Ofisi ya Rais. Na ukiangalia Uganda, wana taasisi maalum ya ufuatiliaji ndani ya Ofisi ya Waziri Mkuu. Ukiangalia Ghana ina Wizara maalum ya ufuatiliaji.

Mheshimiwa Spika, lakini Tanzania tathmini na ufuatiliaji umepewa vi-sub sectors katika Wizara sita tofauti; Wizara ya Fedha imo, Ofisi ya Waziri Mkuu imo, TAMISEMI imo, Utumishi imo, National Audit imo na NBS. Wote wanafanya ufuatiliaji na tathmini bila kuwa na heading entity. Nani ana- lead evaluation and monitoring katika Tanzania yetu; hayupo. Naomba niishauri Serikali, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, ilibebe suala zima la ufuatiliaji na tathmini ili tuweze kupata matunda tarajiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kaka yangu, Mheshimiwa Reuben juzi alizungumza suala zima la kuwepo na Sheria ya Ufuatiliaji na Tathmini. Naungana naye mkono asilimia 200. Lakini vilevile ni lazima tuanze na sera nzuri zenye miongozo ya kuhakikisha ufuatiliaji na tathmini inafanyika katika mikakati yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala zima la kuwa na sera na sheria litatusaidia sana kuhakikisha miradi yetu inakwenda kusimamiwa ipasavyo, lakini pia itazuia kukubali mifumo holela ya mataifa yanayotupa udhamini. Kila anayetupa udhamini anakuja na mfumo wake wa tathmini. Sisi kama nchi hatuwezi kukubali kupokea mifumo holela kwasababu tu tunapewa pesa, ni lazima tuwe na taasisi imara ambayo itasimamia ufuatiliaji na tathmini na siyo ku-accept kila mfumo kutoka nchi za nje. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niseme kwamba Nchini kwetu Tanzania tunafanya vizuri mno katika suala zima la monitoring, lakini tathmini za kina hazifanyiki. Mara nyingi tunafanya vikao vingi, tunaandika ripoti nyingi lakini tathmini za kina hazipo. Kwa hiyo, ni lazima tukubali kutengeneza taasisi imara ambayo itasimamia na kubuni mifumo sahihi ya ufuatiliaji na tathmini. Bila namna hiyo, bila kufanya hivyo hatuwezi kutoka. Na ndiyo ule utelezi aliousema dada yangu, Mheshimiwa Jesca. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia suala la ushirikishwaji wa wanawake katika Mpango wa Maendeleo wa Taifa letu. Naomba ku-refer Mheshimiwa Rais wetu, mama Samia Suluhu alipokuwa anazungumza na Naibu Waziri wa Michezo alipomwambia kwamba wanawake nao wakanufaike na vipaji vyao katika Sekta ile ya Michezo. Ilinisababisha kufikiri kwamba kumbe mpaka leo bado katika Taifa letu kuna idara ambazo sera zake sio gender inclusive, maana yake ilikuwa hivyo.

Mheshimiwa Spika, bado katika taifa letu kuna idara ambazo sera zake sio gender inclusive, this is maana yake lilikuwa hivyo, lakini ukikumbuka Mkukuta ulishaweka wazi ikielekeza wizara zote kwamba zikawe na sera ambazo zina- include ushirikishwaji wa wanawake. Sasa kama mpaka leo hazipo maana yake ni nini? Wawawake wanakuwa wakiweka pembeni katika mpango wa …

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante Mheshimiwa Aisha, Ahsante sana; Mheshimiwa Tumaini.

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Spika,ahsante, naunga mkono hoja.